Mtoto wa Shule
JF-Expert Member
- Nov 16, 2014
- 19,641
- 14,248
Kauli hii;Chama cha Mapinduzi kinaenda kufa rasmi mikononi mwa Rais Samia.
Rais Samia hapendwi, simpendi, hatumpendi.
Ni aibu kuona chama tawala kilichodumu miaka na miaka kwenda kumfia mgombea ambaye hata wanachama wenzake ndani ya chama hawakubali uongozi wake ila kakikundi ka watu wachache wenye mamlaka wamepitisha kimabavu.
a) Aliambiwa Mzee Mwinyi. CCM haikumfia.
b) Aliambiwa Mzee Mkapa na CCM haikumfia.
c) Aliambiwa Mzee Kikwete na CCM haikufa kipindi chake.
d) Aliambiwa Mwamba. Magufuli. "eti" kwakuwa HAKUWAHI kuwa Kiongozi wa CCM kwa ngazi yoyote ile, lakini CCM ikawa imara zaidi ya kipindi chochote kile na haikufa.
Leo mnakuja na ramli zilezile za kipuuzi na kipumbavu kwa Mwenyekiti wa CCM Taifa wa sasa Rais Samia.
CCM ITAENDELEA KUWA IMARA ZAIDI YA JUZI, JANA NA LEO CHINI YA KOMREDI SAMIA SULUHU HASSAN!!