Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,311
- 9,740
Ndugu zangu Watanzania,
Rais Samia anaendelea kujizolea sifa, kuandikwa jina lake kwa wino wa dhahabu katika mioyo ya Watanzania, kuacha alama za kukumbukwa na Watanzania kutokana na misimamo yake ya kizalendo na kibinadamu kwa Watanzania. Rais Samia kwa ujasiri, uchungu, ushupavu, uzalendo na msimamo wa hali ya juu sana amekataa kata kata kuingiza, kubariki na kuweka masuala ya upendeleo na ubaguzi katika kuwapelekea wananchi miradi ya maendeleo kwa misingi ya uchama au ubaguzi wa aina yoyote ile.
Rais Samia anatambua kuwa yeye ni Rais wa Watanzania wote, anatambua ya kuwa kila Mtanzania ana lipa kodi kwa njia tofauti tofauti, kila Mtanzania ana haki ya kuchagua chama akipendacho kulingana na sera za chama husika na kila Mtanzania ana haki ya kupelekewa huduma muhimu na serikali yake kutokana na haki asili ya kuwa Mtanzania wa kuzaliwa na anayelipa kodi.
Rais Samia anaona siyo haki wala siyo sawa wala siyo utamaduni wetu wa kuanza kupanda mbegu ya kubaguana kwa misingi ya kisiasa, anajua mbegu hii ikipandwa haitaishia hapa tu, anajua mbegu hii ikiachwa italitafuna Taifa lote vizazi na vizazi, ndio maana hayupo tayari kushiriki katika dhambi hii ya kuliangamiza Taifa.
Rais Samia amekemea na kujiuliza kwanini uwatese watoto wasio na hatia kwa kuwanyima fursa ya elimu kwa kutojengewa shule kisa tu eneo lao lina wapinzani wengi? Kosa lao nini hao watoto? Kwanini waadhibiwe kwa makosa ya wazazi wao? Kwanini uchepushe miradi kisa tu eneo hilo lina upinzani? Je hao siyo Watanzania? Je hawalipi kodi? Kama hutaki kuwapa miradi wanayostahili kwanini uende ukusanye kodi kwao? Kwanini uwabughudhi, watii sheria wakati huwatambui kuwa ni wananchi wako? Ni vipi sasa watarudisha moyo wa kuipenda serikali na chama ikiwa huonyeshi kuwajali na kuwathamini? Kwanini usiwapelekee maendeleo ili wajute kuwaunga mkono upinzani na kuanza kukuunga mkono wewe?
Kwa hakika, Rais Samia amedhihirisha usemi usemao kuwa mwenye haki akitawala na kuwa na mamlaka, nchi yote na watu wote hufurahi na kuishi kwa furaha, lakini muovu akitawala nchi hububujikwa kwa machozi na kutawala kwa vilio na mateso kwa watu. Rais Samia ni mama wa haki, ndio maana nchi ina amani, furaha, upendo, tabasamu na vicheko kila kona ya Taifa letu.
Rai kwa viongozi wote wa serikali na watumishi wa umma ni kuhakikisha ya kuwa mnatenda haki kwa watu wote pasipo ubaguzi wa aina yoyote ile na kwa misingi ya aina yoyote ile. Mama yetu na Rais wetu ni mcha Mungu na mwenye hofu ya Mungu, na hayupo tayari kushiriki au kubariki dhambi ya ubaguzi kwa misingi ya aina yoyote ile. Amedhamiria kuliungaisha Taifa letu na kujenga umoja wa kitaifa pasipo ubaguzi wala chuki, hataki ushetani na vitendo vya kishetani ndani ya utawala wake, anataka haki na usawa kwa watu wote. Anataka Taifa linalozungumza lugha moja, hataki kuwapa watu adhabu kisa tofauti za kimtazamo na kisiasa.
Huyo ndiye Rais Samia, mama wa shoka, jasiri muongoza njia, shujaa wa Afrika, nembo ya Taifa, nuru ya wanyonge, mama na kiongozi mpambanaji, komandoo wa vita, simba wa nyika, na sauti ya Afrika na mtetezi wa wanyonge anayeendelea kulipa raha, tabasamu na furaha Taifa letu. Kwa hakika, Rais Samia ni zawadi kwetu Watanzania tunayopaswa kuitunza kwa wivu mkubwa sana. Ni dhahabu itembeayo, japo vipofu wa akili na macho wanaweza wasione haraka haraka.
Kazi iendelee, mama ametufikia na kuwafikia Watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya Watanzania wanyonge wasio na sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.
Rais Samia anaendelea kujizolea sifa, kuandikwa jina lake kwa wino wa dhahabu katika mioyo ya Watanzania, kuacha alama za kukumbukwa na Watanzania kutokana na misimamo yake ya kizalendo na kibinadamu kwa Watanzania. Rais Samia kwa ujasiri, uchungu, ushupavu, uzalendo na msimamo wa hali ya juu sana amekataa kata kata kuingiza, kubariki na kuweka masuala ya upendeleo na ubaguzi katika kuwapelekea wananchi miradi ya maendeleo kwa misingi ya uchama au ubaguzi wa aina yoyote ile.
Rais Samia anatambua kuwa yeye ni Rais wa Watanzania wote, anatambua ya kuwa kila Mtanzania ana lipa kodi kwa njia tofauti tofauti, kila Mtanzania ana haki ya kuchagua chama akipendacho kulingana na sera za chama husika na kila Mtanzania ana haki ya kupelekewa huduma muhimu na serikali yake kutokana na haki asili ya kuwa Mtanzania wa kuzaliwa na anayelipa kodi.
Rais Samia anaona siyo haki wala siyo sawa wala siyo utamaduni wetu wa kuanza kupanda mbegu ya kubaguana kwa misingi ya kisiasa, anajua mbegu hii ikipandwa haitaishia hapa tu, anajua mbegu hii ikiachwa italitafuna Taifa lote vizazi na vizazi, ndio maana hayupo tayari kushiriki katika dhambi hii ya kuliangamiza Taifa.
Rais Samia amekemea na kujiuliza kwanini uwatese watoto wasio na hatia kwa kuwanyima fursa ya elimu kwa kutojengewa shule kisa tu eneo lao lina wapinzani wengi? Kosa lao nini hao watoto? Kwanini waadhibiwe kwa makosa ya wazazi wao? Kwanini uchepushe miradi kisa tu eneo hilo lina upinzani? Je hao siyo Watanzania? Je hawalipi kodi? Kama hutaki kuwapa miradi wanayostahili kwanini uende ukusanye kodi kwao? Kwanini uwabughudhi, watii sheria wakati huwatambui kuwa ni wananchi wako? Ni vipi sasa watarudisha moyo wa kuipenda serikali na chama ikiwa huonyeshi kuwajali na kuwathamini? Kwanini usiwapelekee maendeleo ili wajute kuwaunga mkono upinzani na kuanza kukuunga mkono wewe?
Kwa hakika, Rais Samia amedhihirisha usemi usemao kuwa mwenye haki akitawala na kuwa na mamlaka, nchi yote na watu wote hufurahi na kuishi kwa furaha, lakini muovu akitawala nchi hububujikwa kwa machozi na kutawala kwa vilio na mateso kwa watu. Rais Samia ni mama wa haki, ndio maana nchi ina amani, furaha, upendo, tabasamu na vicheko kila kona ya Taifa letu.
Rai kwa viongozi wote wa serikali na watumishi wa umma ni kuhakikisha ya kuwa mnatenda haki kwa watu wote pasipo ubaguzi wa aina yoyote ile na kwa misingi ya aina yoyote ile. Mama yetu na Rais wetu ni mcha Mungu na mwenye hofu ya Mungu, na hayupo tayari kushiriki au kubariki dhambi ya ubaguzi kwa misingi ya aina yoyote ile. Amedhamiria kuliungaisha Taifa letu na kujenga umoja wa kitaifa pasipo ubaguzi wala chuki, hataki ushetani na vitendo vya kishetani ndani ya utawala wake, anataka haki na usawa kwa watu wote. Anataka Taifa linalozungumza lugha moja, hataki kuwapa watu adhabu kisa tofauti za kimtazamo na kisiasa.
Huyo ndiye Rais Samia, mama wa shoka, jasiri muongoza njia, shujaa wa Afrika, nembo ya Taifa, nuru ya wanyonge, mama na kiongozi mpambanaji, komandoo wa vita, simba wa nyika, na sauti ya Afrika na mtetezi wa wanyonge anayeendelea kulipa raha, tabasamu na furaha Taifa letu. Kwa hakika, Rais Samia ni zawadi kwetu Watanzania tunayopaswa kuitunza kwa wivu mkubwa sana. Ni dhahabu itembeayo, japo vipofu wa akili na macho wanaweza wasione haraka haraka.
Kazi iendelee, mama ametufikia na kuwafikia Watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya Watanzania wanyonge wasio na sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.