Yesu Anakuja
JF-Expert Member
- Apr 10, 2019
- 9,473
- 19,268
Kuna features kadhaa kuhusu matukio makubwa mawili yaliyojiri siku chache zilizopita, la kukamatwa Mheshimiwa Mbowe na viongozi wengine kadhaa wa Chadema, na kabla ya hapo, kukamatwa kwa wafuasi kadhaa wa chama hicho, matukio yaliyojiri huko Mwanza.
Kwanza, hoja za jeshi la polisi na mkuu wa mkoa Mwanza kuzuwia kongamano kwa kigezo cha korona ni utopolo. Hilo halina mjadala.
Pili, kuzuwia kongamano hilo pamoja na lile la awali ni ukiukwaji wa haki za kidemokrasia na kikatiba. Freedom of association sio fadhila bali haki ya msingi kwa kila Mtanzania. Polisi wanapaswa kutoa ulinzi kwenye matukio husika na sio kuwa waamuzi wa endapo shughuli ifanyike au la.
Tatu, kama ilivyokuwa utawala uliopita, kuna double standards, ambapo CCM "wanapeta" tu ilhali ni kosa la jinai kwa Wapinzani japo kijaribu hayohayo CCM wanaruhusiwa kuyafanya.
Nne, kukamatwa kwa Mheshimiwa Mbowe na viongozi wengine wa Chadema kunatia doa taswira nzuri iliyoanza kujengeka kuwa Mama Samia anataka siasa za maelewano badala ya siasa za chuki zilizotawala zama za Mwendazake. Kuachiwa kwa Mdude na kugeuzwa hukumu ya Mbowe ni miongoni mwa ishara zilizotupa matumaini wengi kuhusu Mama Samia.
Tano, siasa za Tanzania na zero-sum game: Unfortunately siasa za Tanzania ni aidha ishinde CCM na Wapinzani wafeli au wapinzani wafaulu na CCM washindwe. Ni vigumu mno kupata suluhu kwenye masuala muhimu ya mustakabali wa kitaifa yanayohitaji mshikamano wa pande zote mbili.
Na ndio maana kwa mazingira ya sasa ni vigumu mno kwa madai ya Katiba mpya kuwa na ufanisi kwa sababu CCM wanajiona washindi wakikwamisha mchakato huo (unfortunately kwa vile ni chama tawala wana uwezo wa kukwamisha) na wanatafsiri kuwa kukwamisha huko ni "kuwapiga bao" Wapinzani
Ufumbuzi: win-win. Katiba ni kwa ajili ya Watanzania wote. Washindi ni Watanzania, sio chama fulani. Ikishindikana, waliofeli ni Watanzania wote, sio kundi fulani.
Sita, Sambamba na hilo, confrontational politics ni ngumu japo wakati mwingine ndio only option. Katika mazingira ya sasa, sidhani kama mkutano kati ya Mama Samia na viongozi wa upinzani utakuwepo tena maana tayari "mstari umechorwa."
Saba, kwa upande mwingine, pengine Mama Samia hajatendewa haki kwenye hilo la mkutano na viongozi wa upinzani. Alikuwa na kila ruhusa ya kutamka kuwa "sihitaji kukutana na Wapinzani" na isingemuathiri kwa lolote, lakini akakubali.
Unfortunately, viongozi wa Chadema wanataka mkutano huo ufanyike mapema kadri iwezekanavyo, which is a valid point. However, kutokana na uzito wa mkutano huo, ni muhimu kuwe na maandalizi ya kutosha. On one side, hakutokuwa na tija endapo mkutano utaishia kuwa fursa ya Mama na wapinzani kunywa kahawa kisha kupiga picha pasipo kujadiliana masuala muhimu kwa taifa letu. On the other side, anayeombwa appointment, hapangiwi wala halazimishwi na mwomba appointment.
Ufumbuzi: kunahitajika ustahimilivu, assuming possibility ya mkutano huo bado ipo, though I highly doubt.
Nane, madai ya katiba mpya ni valid. Katiba Iliyopo ina mapungufu makubwa. Now, whether kinachohitajika ni katiba mpya au marekebisho kwenye katiba iliyopo, that's open to discussion.
However, approach ya kudai katiba ipo a bit flawed. Kws kuzingatia kuwa siasa zetu ni za zero-sum, it is virtually impossible kwa CCM kuridhia mchakato wa Katiba mpya, kwa sababu watakuwa wanajipiga bao. It essentially would fast-track safari ya wao kitoka madarakani.
Tisa, kuna kikwazo cha pili. Ni kwamba utamaduni wa siasa za Tanzania, na hata baadhi ya nchi kubwa, hutegemea sana utashi wa kiongozi aliyepo madarakani. Tumeona zama za Magufuli. Aliyotaka yawe yakawa. Aliyitaka yasiwe hayakuwa. Lakini hata Marekani, utashi wa Obama uliifanya Marekani kuwa "tofauti" na "Marekani ya Trump," na "ya Biden" ni tofauti pia. Na hili ni taifa lenye katiba imara na kongwe.
Ufumbuzi: pamoja na ugumu mwingi, only viable way ya kuwezesha mchakato wa Katiba ni kuhusisha utashi wa Mama Samia, kufanikiwa kuwavuta CCM waone kuwa ni win-win na sio zero-sum game, na suala la katiba kuwa la kitaifa zaidi kuliko "la chama kimoja."
Kumi, no si dhambi kwa Chadema kuongoza harakati za kudai Katiba mpya. However, on on side kuna kikwazo hicho cha CCM, lakini tatizo kubwa zaidi ni kwamba kuna watu watakaokwepa kuunga mkono katiba mpya kwa vile tu ni "sera ya chama flani." Ikumbukwe, zaidi ya nusu ya Watanzania si wafuasi wa chama chochote cha siasa.
Mwisho, ni jawabu la swali lililobeba kichwa cha habari. Je Mama Samia anairudisha Tanzania kwenye zama za siasa za chuki au huu ni utekelezaji wa kile alichotanabaisha mapema kuwa "ukinizingua nitakuzingua"?
Hilo moja, la pili, na linalohitaji tafakuri kubwa ni ukweli mchungu kuwa hata Mama Samia akiamua "kuachana na siasa za kistaarabu" na kuwa full tyrant, hakuna ww kumzuwia. Hakuna aliyeweza kumzuwia Mkapa kuukandamiza upinzani 1995 to 2005. Hakuna aliyeweza kumzuwia Jk kuuma na kupuliza ambapo hadharani alionekana mtu poa kwa wapinzani ilhali faraghani aliwahujumu. Na hakuna kilichoweza kumzuwia Shujaa Mwendazake kufanya siasa za chuki ambapo aliwanyanyasa wapinzani atakavyo.
Ukweli mwingine mchungu ni kwamba tangu jana ni "porojo" tu, Spaces, nk lakini hadi muda huu kinachosubiriwa ni "huruma ya serikali" kuwaachia Mheshimiwa Mbowe na wenzake. Katika mazingira haya ambayo watu ni mahiri sana wa kuongea na kujimwambafai kuliko kutenda, pengine ni muhimu kuwa na Plan B kabla ya kufanya jambo ambalo matokeo yake yanafahamika. Kwa tukio la Mwanza, ilifahamika bayana nini kingetokea, lakini ni wazi there was no plan B. Another zero-sum game?
Kuna video hapa chini inayoeleza hoja hizo zote kwa upana
chahali siku zote huwa unaongea bila kufikiri, na ni snich wa watu wanaokuamini hapa. utatangatanga nchi za watu kama nyani hadi lini bro? utafia hukohuko uskoshi bila hata kufurahia nchi yako. hadi huwa nakuonea huruma. nani asiyekujua watu uliowalisha kwenye mdomo wa mamba kwa kukuamini kuwa upo upande wao.