Countrywide
JF-Expert Member
- Mar 2, 2015
- 18,200
- 27,255
Baada ya kuzunguka huko na huku hatimaye wamejua ongezeko la mshahara, lawama zimeanza na wengine kuanza kumshambulia Rais. Hii haikubaliki hata kidogo.
Raisi aliweka wazi ongezeko la mshahara kwa 23.3% ni wale wa kima cha chini, Ila kutokujua kusoma na kuelewa kwa watumishi kukafanya ionekane ni kwa watu wote.
Ni kama kuna watu walijiandaa kutoa lawama kwa Rais wetu ikiwa taarifa ilisema wazi kabisa kuwa ni kima cha chini. Hata hivyo tukirudi kwenye uhalisia kwa uchumi ulivyoyumba duniani na Tanzania tukiwemo, unawezaje kuhitaji ongezeko la 23.3%? Kwa kazi gani hasa unazofanya?
Watumishi wengi ni walimu, zaidi ya nusu(300000+) na hawa ndio waliokuwa mstari wa mbele kupotosha ongezeko ili mwisho wa siku ionekane serikali iliongopa. Shida ni nini kwenye hii kada ya ualimu? Ufahamu mdogo?
Narudia tena acheni lawama kwa Rais mara moja, na pia mshukuru hata kwa hiko kidogo mlichopata.
Raisi aliweka wazi ongezeko la mshahara kwa 23.3% ni wale wa kima cha chini, Ila kutokujua kusoma na kuelewa kwa watumishi kukafanya ionekane ni kwa watu wote.
Ni kama kuna watu walijiandaa kutoa lawama kwa Rais wetu ikiwa taarifa ilisema wazi kabisa kuwa ni kima cha chini. Hata hivyo tukirudi kwenye uhalisia kwa uchumi ulivyoyumba duniani na Tanzania tukiwemo, unawezaje kuhitaji ongezeko la 23.3%? Kwa kazi gani hasa unazofanya?
Watumishi wengi ni walimu, zaidi ya nusu(300000+) na hawa ndio waliokuwa mstari wa mbele kupotosha ongezeko ili mwisho wa siku ionekane serikali iliongopa. Shida ni nini kwenye hii kada ya ualimu? Ufahamu mdogo?
Narudia tena acheni lawama kwa Rais mara moja, na pia mshukuru hata kwa hiko kidogo mlichopata.