saidoo25
JF-Expert Member
- Jul 4, 2022
- 602
- 1,407
Rais Samia Suluhu Hassan amenukuliwa na magazeti mengi ya leo akitoa onyo la mwisho kwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mashimba Ndaki kutokana na usimamizi mbovu wa Wizara yake na kudaiwa huku fedha nyingi zikidaiwa kupotelea kwenye mifuko ya watu.
Naungana na Rais Samia, Mashimba ameonyesha kushindwa kwa kiwango kikubwa kutekeleza majukumu yake hasa katika maeneo kadhaa ikiwemo kusababisha kushamiri kwa migogoro ya wakulima na wafugaji kurudi upya na watu kuuana mfano Kilindi, Rufiji, Kilimanjaro, Mbeya na maeneo mengine ya nchi mambo ambayo hapo nyuma yalitulia.
Mashimba ameshindwa kusimamia Rachi za Taifa na kusababisha Serikali kupoteza mapato mengi kutokana na usimamizi mbovu wa sekta hiyo.
Pia kulikuwa na utaratibu wa kuogesha mifugo kwa dawa za ruzuku jambo hilo Waziri Mashimba ameua utaratibu huo na kusasabisha wafugaji wengi kushindwa kuongesha mifugo yao na mingi kufa kwa magonjwa.
Mashimba pia ameshindwa kusimamia sekta ya uvuvi na kusababisha samaki kupungua sana Ziwa Victoria na maeneo mengine kutokana na kushamiri kwa uvuvi haramu na kusababisha uhaba wa samaki na dagaa na kwamba anadaiwa kuwa hafanyi juhudi zozote za kudhibiti uvuvi haramu kwa kisingizio kuwa Rais amesema watu wasionewe.
Mashimba amekuwa akitumia vibaya jina la Rais kwamba ndiye ameruhusu uvuvi haramu na mifugo iendelee kutoroshwa nje ya nchi jambo ambalo sio la kweli kwani hakuna kiongozi wa Serikali aliyeapishwa kulinda rasilimali za nchi akaruhusu ziharibiwe eti kwa kisingizio cha hataki watu kuonewa wakati Sheria za nchi zinataka mali hizo zilindwe.
Naungana na Rais Samia, Mashimba ameonyesha kushindwa kwa kiwango kikubwa kutekeleza majukumu yake hasa katika maeneo kadhaa ikiwemo kusababisha kushamiri kwa migogoro ya wakulima na wafugaji kurudi upya na watu kuuana mfano Kilindi, Rufiji, Kilimanjaro, Mbeya na maeneo mengine ya nchi mambo ambayo hapo nyuma yalitulia.
Mashimba ameshindwa kusimamia Rachi za Taifa na kusababisha Serikali kupoteza mapato mengi kutokana na usimamizi mbovu wa sekta hiyo.
Pia kulikuwa na utaratibu wa kuogesha mifugo kwa dawa za ruzuku jambo hilo Waziri Mashimba ameua utaratibu huo na kusasabisha wafugaji wengi kushindwa kuongesha mifugo yao na mingi kufa kwa magonjwa.
Mashimba pia ameshindwa kusimamia sekta ya uvuvi na kusababisha samaki kupungua sana Ziwa Victoria na maeneo mengine kutokana na kushamiri kwa uvuvi haramu na kusababisha uhaba wa samaki na dagaa na kwamba anadaiwa kuwa hafanyi juhudi zozote za kudhibiti uvuvi haramu kwa kisingizio kuwa Rais amesema watu wasionewe.
Mashimba amekuwa akitumia vibaya jina la Rais kwamba ndiye ameruhusu uvuvi haramu na mifugo iendelee kutoroshwa nje ya nchi jambo ambalo sio la kweli kwani hakuna kiongozi wa Serikali aliyeapishwa kulinda rasilimali za nchi akaruhusu ziharibiwe eti kwa kisingizio cha hataki watu kuonewa wakati Sheria za nchi zinataka mali hizo zilindwe.