Rashda Zunde
JF-Expert Member
- May 28, 2022
- 291
- 281
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akiwa wilayani Rungwe mkoani Mbeya, amesisitiza dhamira ya serikali yake kulinda maslahi ya wakulima kwa kuhakikisha rasilimali muhimu kama ardhi na mazao ya kimkakati yanabaki kwa manufaa ya wananchi.
Akizungumzia uwekezaji katika zao la chai, Rais Samia alisema baadhi ya wawekezaji akiwemo kampuni ya Mohamed Enterprises walishindwa kufikia matarajio ya serikali ya kuwa msaada kwa wananchi baada ya kupewa nafasi ya kuwekeza. Amesema licha ya kupewa fursa ya kuendeleza viwanda vya chai, wawekezaji hao wameshindwa kuviendesha na pia wanadaiwa mishahara na stahiki za wafanyakazi wao.
Rais Samia alisisitiza kuwa serikali haiwezi kukubali kuona ardhi na viwanda vinakaa bila tija huku wakulima wakihangaika, na kwamba msimamo wa serikali ni kuhakikisha rasilimali za taifa zinatumika kwa maslahi ya wananchi, si kwa faida binafsi za wachache.
Aidha, Rais Samia amevitaka viwanda hivyo kulipa mishahara ya wafanyakazi wake.
Akizungumzia uwekezaji katika zao la chai, Rais Samia alisema baadhi ya wawekezaji akiwemo kampuni ya Mohamed Enterprises walishindwa kufikia matarajio ya serikali ya kuwa msaada kwa wananchi baada ya kupewa nafasi ya kuwekeza. Amesema licha ya kupewa fursa ya kuendeleza viwanda vya chai, wawekezaji hao wameshindwa kuviendesha na pia wanadaiwa mishahara na stahiki za wafanyakazi wao.
Rais Samia alisisitiza kuwa serikali haiwezi kukubali kuona ardhi na viwanda vinakaa bila tija huku wakulima wakihangaika, na kwamba msimamo wa serikali ni kuhakikisha rasilimali za taifa zinatumika kwa maslahi ya wananchi, si kwa faida binafsi za wachache.
Aidha, Rais Samia amevitaka viwanda hivyo kulipa mishahara ya wafanyakazi wake.