Mimi napingana na hoja yako,binafsi naona shida ni mifumo yetu mibovu chini ya sheria zetu na katiba yetu ambayo imepitwa na wakati,
Trump sio kwamba leo ni Rais wa USA ni bora na upo IQ kubwa kuliko Wamarekani wote , bali mifumo ya nchi ipo imara chini ya katiba yao na sheria zao.
Kila mtu anawajibika katika majukum yake ,ukizingua unakutana na kaa la moto bila kujali cheo cha mtu.
Leo hii Trump akawa Rais wa Tz kutokana na mifumo yetu mibovu naye atapuyanga tu ,
Hivyo hivyo hakuna Rais wa nchi hii atakuja bila kutobadili katiba , sheria mbalimbali ili kuboresha mifumo akatobo ,hakuna ata leo akishuka toka mbinguni.
So leo au kesho yoyote akiwa Rais kwa mifumo yetu hii hatoboi , matatizo, shida kwa wananchi , uchumi wa nchi ,mambo yataendelea kuwa hivihivi na pengine kuwa mbaya zaidi. Hakuna cha kuupiga mwingi wala mjomba wake ukweli ndo huo.