Synthesizer
Platinum Member
- Feb 15, 2010
- 14,932
- 28,132
Baada ya Nchimbi kuongea jinsi Nyerere alivyochukia na kukemea rushwa na kukataa kabisa kutumia nafasi yake ya uraisi kuwanufaisha watoto wake, ndugu zake na jamaa wengine wa karibu, kumekuwa na maneno mengi mitaani kwamba Makamu wa Raisi alikuwa akimpiga dongo Raisi Samia.
Watu wameenda mbali na kusema mtoto wa Samia Abdul, mkwe wake, watoto wake,shoga zake na ndugu na jamaa wa Rais Samia wamekuwa wakiufaidi uraisi wa Samia kwa namna ambayo hakuna rais amewahi kufanya hivi kwa watu wake wa karibu, na labda anaemfuata Samia ni Kikwete, ambae yuko karibu na Samia na anatajwa pia kama mnufaika wa urais wa Samia.
Na watu wanadai Rais Samia hajawahi kutoa hotuba yoyote ya kukemea, kulaani na kuahidi kushughulikia rushwa na ufisadi nchini. Kuna mtu anasema hotuba kali kuliko zote alizotoa kuhusu kukemea rushwa na ufisadi ni ele aliyosema msichote sana hadi kuvimbiwa!
Haya ni mambo mazito kusema kuhusu raisi wa nchi. Nadhani tunaenda mbali sana kuhusu raisi wetu. Kama kuna mtu ana hotuba za Raisi Samia akikemea na kufoka kuhusu rushwa na ufisadi tafadhali tuwekee hapa ili tumalize huu ubishi.
Watu wameenda mbali na kusema mtoto wa Samia Abdul, mkwe wake, watoto wake,shoga zake na ndugu na jamaa wa Rais Samia wamekuwa wakiufaidi uraisi wa Samia kwa namna ambayo hakuna rais amewahi kufanya hivi kwa watu wake wa karibu, na labda anaemfuata Samia ni Kikwete, ambae yuko karibu na Samia na anatajwa pia kama mnufaika wa urais wa Samia.
Na watu wanadai Rais Samia hajawahi kutoa hotuba yoyote ya kukemea, kulaani na kuahidi kushughulikia rushwa na ufisadi nchini. Kuna mtu anasema hotuba kali kuliko zote alizotoa kuhusu kukemea rushwa na ufisadi ni ele aliyosema msichote sana hadi kuvimbiwa!
Haya ni mambo mazito kusema kuhusu raisi wa nchi. Nadhani tunaenda mbali sana kuhusu raisi wetu. Kama kuna mtu ana hotuba za Raisi Samia akikemea na kufoka kuhusu rushwa na ufisadi tafadhali tuwekee hapa ili tumalize huu ubishi.
