Rais Magufuli Yuko sawa Kweli?

TL. Marandu

JF-Expert Member
Jul 12, 2015
3,625
5,807


Nilikuwa kabla ya Uchaguzi mkuu 2015 Nikimpenda sana Magufuli, Kiasi Tangu 2012 Nilikuwa Nikimfuatilia. Nilimheshimu sana kama mchapa Kazi asiye na Mchezo.
Wakati wa Kampeni 2015 Niliendelea kumheshimu ila Nilitaka Lowassa ashinde kwa Kuwa Niliamini Ni lazima Tanzania iwe na real Political equilibrium baada ya Miaka zaidi ya hamsini ya Utawala wa chama Kimoja.

Baada ya Uchaguzi na Jinsi Computer za Ukawa zilivyoporwa na Matokeo ya Uchaguzi wa Zanzibar Kuhujumiwa, nilitiwa kichefu chefu kiasi nilianza kumdharau kwa kutumika katika Maswala ya aibu! Lakini Nilipoona anaenda Muhimbili nusu atokwe na Machozi kwa Wamama kulala Chini, Nikaanza kuwa na Matumaini Kwake! Alipomtuma Majaliwa Pale Bandarini akamwagiza IGP ang'oke na Akina Masamaki ndio Kabisa nikasema Asante Yesu.

1)Kisha akakutana na Wazee Dar es salaam, Makonda! Nilistuka sana sana.

2)Kisha akafungia Matangazo ya TBC ya Bunge kwa hila Nikastuka sana.

3)Sakata la Kuletwa Polisi wa FFU na Mbwa bungeni Kuwapiga Wabunge Likanisononosha sana!

4)Alipomchagua Mwkonda Kuwa Mkuu wa Mkoa Nikanawa Mikono Kama Pilato, Nikaanza kutilia Mashaka Judgement zake.

5)Akakataza Mahafali ya UKAWA wakati ya CCM yanafanyika kwa Nyimbo, Uniform na Bendera za Chama, Nikaanza sasa Kumdharau.

6) Akazuia amikutano ya Vyama isipokuwa Yeye tu. Nikamdharau sana!

7) Akatimua Watoto 7000 wa Masikini Kisa hawana Vyeti au sifa Huku akiwatukana.

8) Atawaagiza NHC watupe vitu vya Mbowe Nje huku akijitapa Nikaendelea kudharau sana!

9) Akasema Jecha apewe Tuzo

10) Akamsaidia Lipumba Kuvunja Ofisi za Cuf na Kuagiza apewe Ruzuku!

11) Akaagiza Lema akamatwe Kisa Lema aliona Maono kuwa Atakufa kama hatabafilika!

12) Sasa Anamtetea Makonda Mdanganyifu, na Aliyevamia Kijambazi Kituo cha Habari!

Sasa sio Tu Kuwa Magufuli simpendi, Bali Namwona kama ni hasara kwa Taifa ni Mnafiki, Au Makonda Kuna Mambo Machafu anamfanyia na Akimfukuza anaona siri zitatoka au Atakosa wa Kumwamini Kumtendea Mambo ya hila?

Magufuli alishawahi Kusema Atauza Majengo ya Wizara Zote za Dar ili Serikali Ihamie Dodoma na anataka Kufanya hivyo Kabla ya Awamu yake ya Miaka mitano haijaisha, Isije Kuwa Lengo ni Kujipatia Kihalifu Majengo ya Wizara za Serikali zilizopo Dar!

Hivi Kweli Mtu Mwaminifu Angekuwa Rais Leo Angeruhusu Makonda hata Amtazame Usoni? Swali langu ni Kuwa Ni nini hasa Kinachowafanya wananchi wawe na imani na Rais anayemlinda Jambazi? Na Mtu anayefanya Corruption na shake up ya Kujipatia Rushwa kwa anaowayuhumu. Huu kwangu ni Wazimu na Rais wa Namna hii hatufai. Nadhani hata kama Makonda akiua mtu hadharani Huyu Mhalifu Mwenzake atamtizama tu!

Wanaccm hasa Wabunge, Msidhani hapa wanaohatibiwa ni Wapinzani! Vyama Zaidi ya Kimoja Imara ni Faida ya Kila Mbunge, Chama chako Ki!ikuonea na Kukufanyia hujuma Kama Bingine vyote Bimekufa hata kama wewe ni Mzuri kama Dhahabu Utafanya nini, Utakimbilia wapi? Kukuwepo na vyama Imara hata kukutisha wataogopa maana wanajua utahama chama na Jimbo bado utalichukua. Kama hamna Akili CCM kubalini Upinzani uuwawe, Kila Mbunge Mwenye Msimamo CCM atakuwa chini ya Rehema za Maguguli.

Mimi nadhani Kutaka CCM ife ni Upofu na Kutaka Upinzani Ufe nchini ni ujinga. Hivyo Wabunge Wote Unganeni Mumdhibiti Magufuli, kabla hamtachelewa maana Nimeshamsoma kwa Mwaka na Zaidi sasa huyu Bwana ni Kiburi, Much know na Msitegemee atabadilika kitu Bila Kumbana asiwe na Uwezo wa Kufanya hila hila zake.
 
Kasema kapewa namba binafsi ya simu ya Rais wa benki ya dunia, na kutoa ahadi kuwa atamsumbua sana kuhusu maendeleo.

Maswali: 1. hivi benki ya dunia hawana governance, na mambo yao kuamuliwa na team? Hivi misaada na mikopo ya benki ya dunia haiangalii democracy? Hivi wadau wakubwa wa benki ya dunia anawafahamu?
 
Mkuu you and I we both don't know the answer and he once said he doesn't take alcohol, who knows what if he could be taking.

Kama Rais Hata kama alimu ya Form Two hawezi Kuona hili la Makonda na Akaona ni Aibu Kubwa na Ni uhalifu wa ajabu sana na Ati anahitaji Nchi Nzima Ipige kelele ndio aelewe huyo hafai kuwa Rais
 
Duuh!!! Ndio maana kweli Gwajima kasema bado anahitajika sana hapa nchini ii kuwasemea watu wa dizaini yako,acha woga!!

Gwajima Ni rafiki yangu Lakini na Yeye alihusika Kupiga Debe ati Kikwete Amwachie Magufuli Umwenyekiti sooner! Nilishangaa sana kwa Kuwa nilishamwona Magufuli , Na hata baada ya Kutajwa na Makonda Kama Muuza Madawa Rafiki yangu Gwajima akamtetea Magufuli, Nilisikitika sana, Mimi hiyo Picha niliistukia mapema, Ilikuwa ni Siasa chafu za Kuwaandama Potential Saporters wa Lowassa 2020. Kwa kutumia Kisingizio cha Vita za Madawa. Ni kama Kuwaua Chui na Paka ukisingizia wamekula kuku wako, Paka sawa Kuku kala ila Chui ulimsingizia kumuaa lakini kesho tunakuona Umevaa koti la Ngozi ya Chui, Hii ni Fulsafa-hila ya zamani sana Half ya truth! The Guy ni Mnafiki Unafiki wake Unazidi harufu ya Maiti iliyooza.

Nikisikia Kila Mara akisema Msema kweli ni Mpenzi wa Mungu natamani Kutapika. In short Magufuli nimemdharau kama . Anafikiri kw Kufanya Mema mawili matatu tena Kwa nia ya Kujitafulia sifa basi Mshahara Tunaompa hautoshi bali Tunatakiwa Tumlipe kwa sarafu ya Uhuru wetu, Amani Yetu na Demokrasia yetu. Isitoshe zulia Jekundu analowekewa mara kadhaa halimtoshi bali anataka Tumpe Katiba yetu na Sheria zetu ndio liwe Zulia Lake. Enough is Enough!
 
Unachokiita Chuki Sisi Tunakiita Uzalendo na Msimamo safi. Kama Kupinga Mtu anayevamia Vyombo vya habari Kijambazi Usiku asiwe Kiongozi wa aina yoyote, kama hiyo kwako ni Chuki basi Unaishi Katika sayari yako nisiyoijua itakuwa Nihasara na Kukupotezea Muda wako na Muda wangu kubishana na Wewe au Kukushawishi Utuelewe.
 
Unachokiita Chuki Sisi Tunakiita Uzalendo na Msimamo safi. Kama Kupinga Mtu anayevamia Vyombo vya habari Kijambazi Usiku asiwe Kiongozi wa aina yoyote, kama hiyo kwako ni Chuki basi Unaishi Katika sayari yako nisiyoijua itakuwa Nihasara na Kukupotezea Muda wako na Muda wangu kubishana na Wewe au Kukushawishi Utuelewe.
KAMA PAMOJA NA MAMBO YOTE MAZUR ALIYOYAFANYA MAKONDA BADO UNAMUITA BINAAADAM MWENZAKO KUNGUNGUNI NA HAMNA HATA SIKU ULIOWAHI KUONA JEMA LAKE KWA JINSI MLIVO NA CHONGO SIO CHUKI NA UTAPELI WA KISIASA NINI
 
Back
Top Bottom