Rais Magufuli yashamshinda?

Rais Magufuli yashamshinda?

Hivi ni mimi tu au na wengine mpo mnaoona kama vile mambo yashamshinda huyu Magufuli?

Kuna hali fulani hivi naiona ambapo jamaa ni kama anaamka tu kila asubuhi na kutoa maamuzi ya kukurupuka kurupuka.
Yaani yeye ni amri tu....fanya hivi....fukuza huyu....twende kule...nk.

Yapo baadhi ambayo ni mazuri ambapo mtu unaona kabisa hapa nia ni nzuri lakini kuna mengine yenye ukakasi sana hadi kunifanya nianze kuhoji hekima na busara za huyo bwana!
Mbwembwe zote zile za kuhamia dodoma kumbe jamaa anahamia 2020.
Sasa sijui kulikuwa na ulazima gani wa kuhangaisha watu kiasi kile?
 
Upo na dereva anaendesha gari, wewe umekaa kiti cha pembeni yake ghafla gari linaanza kuyumba yumba, dereva anakuuliza mbona gari linayumba yumba litakuwa lina matatizo? Wewe una mjibu hapana angalia uendeshaji wako wa gari ndo utakuwa una matatizo lakini dereva ana kubishia unajua nini kinachokwenda kutokea mbele? Ni kwenda kuliangusha gari.

HUKO NDIKO TUNAKO ELEKEA.
Hii inawahusu green color bila shaka
 
Upo na dereva anaendesha gari, wewe umekaa kiti cha pembeni yake ghafla gari linaanza kuyumba yumba, dereva anakuuliza mbona gari linayumba yumba litakuwa lina matatizo? Wewe una mjibu hapana angalia uendeshaji wako wa gari ndo utakuwa una matatizo lakini dereva ana kubishia unajua nini kinachokwenda kutokea mbele? Ni kwenda kuliangusha gari.

HUKO NDIKO TUNAKO ELEKEA.
Ulishazoea ramii. Utelezi hadi unafika.
Esy come.
Mtakuja tu huku kwenye vumbi ndipo mtajua ni gari bovu au uendeshaji au wewe uliyepanda unasikia kizunguzungu.
 
Upo na dereva anaendesha gari, wewe umekaa kiti cha pembeni yake ghafla gari linaanza kuyumba yumba, dereva anakuuliza mbona gari linayumba yumba litakuwa lina matatizo? Wewe una mjibu hapana angalia uendeshaji wako wa gari ndo utakuwa una matatizo lakini dereva ana kubishia unajua nini kinachokwenda kutokea mbele? Ni kwenda kuliangusha gari.

HUKO NDIKO TUNAKO ELEKEA.
Nimekusoma mkuu
 
Mimi ni mmoja wa watu wanaoamini kuwa rais wetu huyu, mheshimiwa mtukufu Dkt. John Pombe Joseph Magufuli si kiongozi mzuri hata kidogo, hususan katika ngazi ya urais.

Hilo nimekuwa nikilisema kwa muda mrefu sasa. Nakumbuka hata ile siku alipoteuliwa kuipeperusha bendera ya CCM nilisema hivyo humu humu JF.

Kwa kiasi fulani namkubali kwenye usimamizi lakini si kwenye uongozi. Hana kabisa haiba ya kiuongozi. Pia hana sifa za kuweza kuwa kiongozi mzuri.

Ni mtu mwenye jazba. Ana jeuri. Mwenye kuongea bila kufikiria athari za maneno yake[nyakati zingine]. Wengine wanasema eti kuwa hashauriki. Kwa ufupi ni mengi sana yanasemwa juu yake kiasi kwamba mengine ni vigumu kwa watu wa mbali kama sisi kujua kama ni ya kweli au la. Hivyo kwa sisi wa mbali tunaenda na yale tuyaonayo na tuyasikiayo toka kwake yeye mwenyewe.

Sasa kwa jinsi vile mambo yanavyoenda sasa hivi kuna kila dalili huenda nchi imeshamshinda kuiongoza. Hivyo ndivyo niuonavyo mwelekeo.

Hata ndani ya chama chake ukiangalia vizuri utaona nyuso nyingi tu za manung'uniko toka kwa wakereketwa. Wengi wao siku hizi wanashindwa hata kumtetea. Wapo kimyaaaa utadhani wagonjwa. CCM hawana furaha kabisa.

Naamini asipojiangalia na kujifanyia tathmini basi hiyo kazi itamshinda kabla hata hajafikia nusu ya muhula wa hii miaka mitano.

Niliwahi kuandika kuhusu 'a police state'. Jikumbushe....

https://www.jamiiforums.com/threads/a-police-state.1105346/#post-17414170
 
Yani mkuu [HASHTAG]#nyani[/HASHTAG] ngabu uko sawa saaana!! Naona karibu uanatufika hapa!!!
 
Back
Top Bottom