Rais Magufuli yashamshinda?

Rais Magufuli yashamshinda?

tena atashinda kwa kura nyingi mnoo. hawa wapinzani hawana ajenda pumzi imekata mapema sana. wamebaki kufanya siasa za kinafiki mitandaoni
Duh kazi ya unafiki katika mitandao vijana wa lumumba nimewanyanyulia kofia.
wanstahili kupewa ukuu wa wilaya na bwana mkubwa
 
Hivi ni mimi tu au na wengine mpo mnaoona kama vile mambo yashamshinda huyu Magufuli?

Kuna hali fulani hivi naiona ambapo jamaa ni kama anaamka tu kila asubuhi na kutoa maamuzi ya kukurupuka kurupuka.
Yaani yeye ni amri tu....fanya hivi....fukuza huyu....twende kule...nk.

Yapo baadhi ambayo ni mazuri ambapo mtu unaona kabisa hapa nia ni nzuri lakini kuna mengine yenye ukakasi sana hadi kunifanya nianze kuhoji hekima na busara za huyo bwana!

Hivi tatizo ni Magufuli au ni sisi wananchi? Tunawategemea wanasiasa mno na sasa ndio ukweli unajitokeza maana kila kukicha ni kujadili UKUTA mara polisi wanafanya mazoezi, ili mradi tunaimba nyimbo za wanasiasa! Nasema Magufuli akaze buti maana tumeweka akili kabatini tunatemea wanasiasa watufanyie kila kitu. Go Magufuli go!
 
Watu ambacho hawapendi sio maamuzi anayofanya rais wetu,naomba utuelewe.Style yake ya maamuzi ina ukakasi wa aina fulani hivi.There is something seriously wrong with the style.Tunajua ana nia nzuri lakini the style needs to change.
Nyani Ngabu urais ni taasisi ukimuona rais anatoa maamuzi ujue information zote anazo
 
KWA MAONI YANGU BINAFSI NA BILA KUFUNGAMANA NA CHAMA CHOCHOTE NAONA HII NCHI TUNAPOELEKEA SASA NI KUBAYA...

Ivi kwanini kila kitu cha wanasiasa wa upande wapili kinageuzwa uchochezi, sasa sio wanasiasa tena hadi raia wema wenye maoni na mawazo tofauti na utaratibu wa serikali ya sasa wanaitwa wachochezi, mbona mnaojiona waheshimiwa saana mmekuwa waoga hivyo, kuna yapi nyuma ya pazia?? Kumbukeni katika kundi la watu haiwezikani wote mkawa na mawazo au fikra sawa, tofauti lazma iwepo na Mwenye busara huheshimu tofauti hizo, huheshimu mawazo, fikra na maoni ya wengine bila kujali hadhi au nafasi yao katika jamii...sio kulazimisha kila kitu iwe ndio mzee!!

Nadhani mfumo wa vyama vingi uliletwa lengo kuu ikiwa ni kukuza demokrasia na pia kuondoa umwinyi wa chama kimoja, na kukipa ushindani na changamoto chama kitakachokuwa kinatawala ili viongozi waweze kuwajibika kikamilifu kabla ya chaguzi znazofuata, Nashangaa sasa mbona inakuwa hivi, Viongozi wetu mnalewa madaraka au??
Uhuru wa maoni upo wapi?? ...Acheni hzo uongozi ni dhamana hakuna wafalme bana wala miungu hapa tz, mie naamini inahitajika busara saana na hekima kuwaongoza watu wanaojielewa na sio mabavu wala nguvu na vitisho, mabavu yanamwisho wake!!

Hapa kutoa tu maoni yangu najua mtasema nachochea......Aaaah wapi mie no mtanzania naipenda nchi yang, naipenda familia yang inayonihitaji...ila sipend kabsa hii nchi mnapoipeleka nyie tunaowaita viongozi wetu na walinda amani..

Naamini ni haki yangu km mtanzania kusema hapana pale napoona mambo yanaenda sivyo, na kwenye haki yangu nitapambana had tonye la mwisho....Amina!!

HAYA NI MAONI YANGU BINAFSI NA WALA SIFUNGAMANI NA CHAMA CHOCHOTE!!
 
Hivi ni mimi tu au na wengine mpo mnaoona kama vile mambo yashamshinda huyu Magufuli?

Kuna hali fulani hivi naiona ambapo jamaa ni kama anaamka tu kila asubuhi na kutoa maamuzi ya kukurupuka kurupuka.
Yaani yeye ni amri tu....fanya hivi....fukuza huyu....twende kule...nk.

Yapo baadhi ambayo ni mazuri ambapo mtu unaona kabisa hapa nia ni nzuri lakini kuna mengine yenye ukakasi sana hadi kunifanya nianze kuhoji hekima na busara za huyo bwana!

Nimekuelewa sana hoja yako, hivi tujiulize ni mambo gani amekurupuka na ni mangapi hajatumia busara?
Katika kipindi cha nyuma watu walilaumu sana viongozi kusita/kuchelewa kuchukua maamzi, pia suala la kuogopana na kulindana lil kuwa kikwazo cha maendeleo, Saizi imekuwa kinyume chake lkn bado unaona mabaya tu.

Sasa lipi zuri?
 
tena atashinda kwa kura nyingi mnoo. hawa wapinzani hawana ajenda pumzi imekata mapema sana. wamebaki kufanya siasa za kinafiki mitandaoni
ishu sio uimara au udhaifuwa upinzani,ishu ni vp rais aliyeko madarakani anavyoongoza nchi
 
Na kwanza tuliosema huyu ni One term president inawezekana hata asikamilishe One Term

Ofcourse sio lazima akae madarakani miaka 5.

Mkuu Ben!
Hiyo probability theory unayotumia kujihoji na kujudge Outcomes umeifanyia analysis?
Ninavyofahamu watu wanaotaka kuwashusha wenzao au kuwaombea mabaya, hayumkini uwaongezea nguvu maradufu.
Kisayansi watu kama nyinyi ni kama Catalysts kwenye tanuli mwisho wa siku mnabaki vivyo hivyo bila kubadilika huku siku zinaenda.
Jamani tubadilike tumuunge Mh. Rais, kuingiza mambo ya siasa kwenye issues za kiutawala na mamlaka ya Urais tuache kwani hata kama tutaendelea haitatusaidia chochote.
 
Rejea hapo juu:Hakua mchezaji basi kocha na bench la ufundi wakaamua kumpa namba baada ya kumtoa striker mahiri aliyekubarika na kuaminika kwamba ataifikisha team iliyokosa mastriker kwa muda mrefu. Kumbuka uwezo wake ilikua ni kucheza nafasi ya ulinzi tena mlinzi tu asiyeweza kupandisha mashambulizi.Basi alivyopewa namba na kupandisha mashambulizi akapewa pasi.Basi mpaka sasa anapiga chenga hili mara kapiga lile kashapiga mengi na mpira unaelekea kumshinda.Kocha na bench la ufundi wanajuta kumpa namba.Mechi ndo kwanza imeanza na utaratibu wa mchezaji kutolewa mpaka kipindi cha kwanza kiishe.Lakini mpaka kipindi kiishe timu ishafungwa magori mengi.Mashabiki wamechoka na mchezo wake.Hari ya mchezo si nzuri naomba aliye karibu na beck striker amwambie mashabiki wanaomba abadilishe style ya mchezo....
 
Upo na dereva anaendesha gari, wewe umekaa kiti cha pembeni yake ghafla gari linaanza kuyumba yumba, dereva anakuuliza mbona gari linayumba yumba litakuwa lina matatizo? Wewe una mjibu hapana angalia uendeshaji wako wa gari ndo utakuwa una matatizo lakini dereva ana kubishia unajua nini kinachokwenda kutokea mbele? Ni kwenda kuliangusha gari.

HUKO NDIKO TUNAKO ELEKEA.
 
Vipi, bado kuna wanaoamini kuwa anaweza?

Au ndo yashamshinda?
 
Msema kweli ni mpenzi wa Mungu, huwezi kufanya maamuzi yakawa sawa yote. Lzm ku accept feedback.
 
Back
Top Bottom