Rais Magufuli yashamshinda?

Rais Magufuli yashamshinda?

Hivi ni mimi tu au na wengine mpo mnaoona kama vile mambo yashamshinda huyu Magufuli?

Kuna hali fulani hivi naiona ambapo jamaa ni kama anaamka tu kila asubuhi na kutoa maamuzi ya kukurupuka kurupuka.
Yaani yeye ni amri tu....fanya hivi....fukuza huyu....twende kule...nk.

Yapo baadhi ambayo ni mazuri ambapo mtu unaona kabisa hapa nia ni nzuri lakini kuna mengine yenye ukakasi sana hadi kunifanya nianze kuhoji hekima na busara za huyo bwana!

---
Mimi ni mmoja wa watu wanaoamini kuwa rais wetu huyu, mheshimiwa mtukufu Dkt. John Pombe Joseph Magufuli si kiongozi mzuri hata kidogo, hususan katika ngazi ya urais.

Hilo nimekuwa nikilisema kwa muda mrefu sasa. Nakumbuka hata ile siku alipoteuliwa kuipeperusha bendera ya CCM nilisema hivyo humu humu JF.

Kwa kiasi fulani namkubali kwenye usimamizi lakini si kwenye uongozi. Hana kabisa haiba ya kiuongozi. Pia hana sifa za kuweza kuwa kiongozi mzuri.

Ni mtu mwenye jazba. Ana jeuri. Mwenye kuongea bila kufikiria athari za maneno yake[nyakati zingine]. Wengine wanasema eti kuwa hashauriki. Kwa ufupi ni mengi sana yanasemwa juu yake kiasi kwamba mengine ni vigumu kwa watu wa mbali kama sisi kujua kama ni ya kweli au la. Hivyo kwa sisi wa mbali tunaenda na yale tuyaonayo na tuyasikiayo toka kwake yeye mwenyewe.

Sasa kwa jinsi vile mambo yanavyoenda sasa hivi kuna kila dalili huenda nchi imeshamshinda kuiongoza. Hivyo ndivyo niuonavyo mwelekeo.

Hata ndani ya chama chake ukiangalia vizuri utaona nyuso nyingi tu za manung'uniko toka kwa wakereketwa. Wengi wao siku hizi wanashindwa hata kumtetea. Wapo kimyaaaa utadhani wagonjwa. CCM hawana furaha kabisa.

Naamini asipojiangalia na kujifanyia tathmini basi hiyo kazi itamshinda kabla hata hajafikia nusu ya muhula wa hii miaka mitano.

Niliwahi kuandika kuhusu 'a police state'. Jikumbushe....

https://www.jamiiforums.com/threads/a-police-state.1105346/#post-17414170
Hapa unamlaumu mtu alieteuliwa na chamachake na chama kikaona ndio mtu pekee anaefaa.

Wao ccm wanamjua vizuri kuliko wewe, hahaaa nahuyo ndio the best selection wao.

Kama kuna lawama wakulaumiwa ni ccm ndio walio mchagua agombee urais.

The hard way is only way up to 2020.
 
Kabla ya raisi kushindwa majukumu yake, naamini watanzania as a society tulishashindwa mda mrefu. Tumebaki na mipasho, majungu, fitina, udaku na uzombi.

Ukisoma archives za jf(posts za miaka mitano-nane iliyopita) utagundua kuwa hili ni taifal inaloenda kwa mihemko, kuanzia top officials hadi mtu wa chini. In no time issue ya Bashite na vyeti itakuwa historia(actually tangu tupate habari za yeye kuvamia Clouds Media tumesahau kuhusu vyeti).

Hahahaaaa hilo mbona liko wazi...

Vyeti vya Bashite kwisha habari yake.

Sasa hivi habari ni Nape the hero...
 
Mimi ni mmoja wa watu wanaoamini kuwa rais wetu huyu, mheshimiwa mtukufu Dkt. John Pombe Joseph Magufuli si kiongozi mzuri hata kidogo, hususan katika ngazi ya urais.

Hilo nimekuwa nikilisema kwa muda mrefu sasa. Nakumbuka hata ile siku alipoteuliwa kuipeperusha bendera ya CCM nilisema hivyo humu humu JF.

Kwa kiasi fulani namkubali kwenye usimamizi lakini si kwenye uongozi. Hana kabisa haiba ya kiuongozi. Pia hana sifa za kuweza kuwa kiongozi mzuri.

Ni mtu mwenye jazba. Ana jeuri. Mwenye kuongea bila kufikiria athari za maneno yake[nyakati zingine]. Wengine wanasema eti kuwa hashauriki. Kwa ufupi ni mengi sana yanasemwa juu yake kiasi kwamba mengine ni vigumu kwa watu wa mbali kama sisi kujua kama ni ya kweli au la. Hivyo kwa sisi wa mbali tunaenda na yale tuyaonayo na tuyasikiayo toka kwake yeye mwenyewe.

Sasa kwa jinsi vile mambo yanavyoenda sasa hivi kuna kila dalili huenda nchi imeshamshinda kuiongoza. Hivyo ndivyo niuonavyo mwelekeo.

Hata ndani ya chama chake ukiangalia vizuri utaona nyuso nyingi tu za manung'uniko toka kwa wakereketwa. Wengi wao siku hizi wanashindwa hata kumtetea. Wapo kimyaaaa utadhani wagonjwa. CCM hawana furaha kabisa.

Naamini asipojiangalia na kujifanyia tathmini basi hiyo kazi itamshinda kabla hata hajafikia nusu ya muhula wa hii miaka mitano.

Niliwahi kuandika kuhusu 'a police state'. Jikumbushe....

https://www.jamiiforums.com/threads/a-police-state.1105346/#post-17414170
Tatizo katiba na mfumo unamfanya rais mungu MTU...
 
Niliwahi kufundshwa nikiwa shuleni kitu kinachoitwa FIXATION. Nadhani kuna mtawala fulani wa Afrika aliruka michezo ya utotoni sasa anaanza kuirudia kipindi umri umeshamtupa.

Watanzania poleni. Siku nyingine mkipata nafasi ya kuchagua kiongozi muwe Sober.
 
Na kwanza tuliosema huyu ni One term president inawezekana hata asikamilishe One Term

Ofcourse sio lazima akae madarakani miaka 5.

55f14aaf4c0c22d996a136df8b8db2ae.jpg
 
HUYU MAGUFULI NDIO RAIS SHUPAVU.NI MAMBO GANI SASA YALIOMSHINDA MAGUFULI ? MAHALI TANZANIA ILIKUWA IMEFIKIA,ILIMUHITAJI RAIS DESIGN YA MAGUFULI.NYIE MNAOMCHUKIA NA KUMKOSOA KILA MARA,MKO WACHACHE SAANA KULIKO SISI TUNAOMUUNGA MKONO.RAIS WETU TUNAKUPA MOYO, ENDELEA KUWATUMBUA HAWA NDUMILA KUWILI AMBAO HAWAJALI WALA KUZISOMA ALAMA ZA NYAKATI.WANAFANYA KAZI KWA MAZOEA. HAWATAKI KUKUBALI KWAMBA KILA UTAWALA UNA STYLE YAKE YA KUTAWALA.AKHSANTE MAGUFULI KWA KUWA NA MSIMAMO THABITI.
 
CHADEMA ingekuwa imara kama zamani huyu easily angeondoka 2020
Lkn kwa upinzani huu wa hovyo hovyo wa kutowasikiliza wanachama na kujiona viongozi kama Mungu watu
Wapinzani wanawatumia wanachama wao kwenye maadamano tu
Kwenye teuzi wanapuuzi kauli za wanachama wa kawaida
Wao na CCM hamna tofauti
Magufuli atashinda 2020 hata kukiwa na TUME HURU
Mark my words
Subutu yake... Ndoo mnavyojiongopea sio eeeeeehh? hana nani huyuu nabii wenu mpaka usawa huu zaid yenu mamluki nyie??
 
mlisema Kikwete hatamaliza mda wake wa urais lkn leo ni rais mstaafu tena kastafu kwa Heshima.
hizi kelele zenu tushazizoea. Magufuli anazidi kuchanja mbuga,
Nyoooo ukizoea kupakatwa hii ndiio taabu yake;;!!![
 
NN chukua time,nyie na wenzio ndio mnamdemoralize rais wetu,kulalamika tu wala hamsuggest nini kifanyike,mapambano ya kweli chukua chama cha upinzani,uweke ideas zako huko zooote,tuachieni rais wetu!
 
NN chukua time,nyie na wenzio ndio mnamdemoralize rais wetu,kulalamika tu wala hamsuggest nini kifanyike,mapambano ya kweli chukua chama cha upinzani,uweke ideas zako huko zooote,tuachieni rais wetu!
Ooh Becky...take that...

 
Back
Top Bottom