Upinzani bado sio imara japokuwa idadi yao ya wabunge imeongezeka sana baada ya uchaguzi wa mwaka jana. Kama DJ anasema wazo la kuhamia Dodoma ni la kukurupuka wakati ni wazo la tangu miaka ya 70, basi ujue upinzani ni dhaifu. Wakati Mwalimu Nyerere anatoa maagizo ya kuhamia Dodoma, DJ alikuwa mtoto wa shule ya msingi, leo hii anasema ni wazo la kukurupuka, na huyu ni mtu very influential kwenye upinzani, lakini upeo wake wa kujadili mambo muhimu ya kitaifa ndio kama huu. Upinzani bado haujawa na ushawishi wa ziada kwenye jamii, na hawajifunzi. Wanaishi kwa kudhani kwamba mtu wa kawaida kabisa hana hekima wala busara za kuweza kupima mienendo ya viongozi wa upinzani.
Ni wazo la kukurupuka ndyo. Uhitaji wa kuhamia dodoma miaka ya 70 sio sawa sawa na miaka ya sasa.
Mpaka sasa haijulikani sababu au nini kipaumbeke cha kuhamia dodma. Mkiulizwa mnadai et ni mpango wa toka zamani na maraic waliopita walishindwa wa sasa hawezi shindwa.
Serkal kuhamia dodomo itamsaidia nini mtanzania?
Kwanini hii habar ya kuhamia dodoma imekuja baada ya Raic kuwa mwenyekit wa CCM?
Makao makuu ya CCM ipo dodoma. Ikulu ipo dar. Na mkuu hapend kusafir kwa ndege. Shanting za dar to dodoma kaona zitakuwa nying ni bora akaish ddma.
Hamuoni huu mpango upo kiCCM zaidi. Watz hta hamjiongezag.
Ila Magu naye si angeamisha makao makuu ya CCM tu ndyo yakahmia dar!
Gharama za kuhamia dodoma zingeweza jenga hata viwanda 3 vya kuprocess nyanya ili kutengeneza soko la uhakika kwa wakulima. Leo nyanya tenga linauzwa 700 tsh morogoro wakulima wamepiga kazi soko hakuna.
Hta kama nia ni kukuza mji wa dodoma iyo sio right approach. Mji haukuzwi kwa majengo ya serkal mji unakuzwa kwa shughuli za kibihshara.
Wangesema viwanda vijengwe dodoma apo sawa vingesaidia development ya mji.
Mbona Mwanza na Arusha ineendelea kwa kasi bila uwepo wa majengo ya serkal kuu?
Hata dar yenyewe imeendelea tokana na shughuli za kibihshara na sio kwa sababu ya kuwepo kwa majengo ya serkal. Serkal yenyewe ndyo iliyokimbilia dar sababu ya kas ya maendeleo yaliyotokana hasa na bandar.
Kama mgufuli kashindwa kukaa ikulu ya dar kwa sababu anazozijua yeye aende mwenyewe dodoma au akakae hta chato maana tunasikia kwake pamejengwa ikulu tiyar.