Rais Magufuli: Watanzania kuamini kila kitu cha kwenye mtandao ni kutokana na sisi kutoi-control mitandao

Wewe unatakaje?..hakuna kitu kisicho na kasoro hapa duniani..ukiwemo wewe mwenyewe!..Nadhani hulijui lengo la mzee baba..hataki kukosolewa kabisaa..anataka kusifiwa tu!..nakuhakikishia kama watu wangekuwa wanamsifia kwenye mitandao..angekuwa anarukaruka kama ndama na hata angeweza kuzirudia zile pushups za wakati wa uchaguzi kwa furaha!Tunahitaji maelezo ya kutosha 1.5 trilion zimeenda wapi?na sio miamala kuiva sijui nn..slowslow hatutaki porojo!

Sifa tamu jamani hata mimi ukinisifia hapa nadani nitalala usingizi mnono, utani pembeni. Unajuwa ukitaka watu wakusikileze au waendelee kukusikiliza ongea jambo la maana, ukishaaza kuleta uswahili-swahili watu wanakuchukulia huna kitu wanakuweka pembeni. Ndio tatizo la mitandao yetu kila mtu anasema, vingine havina hata haja ya kuvitilia maanani matokeo yake hata huyo JPM mwenyewe anaacha kuwasikiliza watanzania ana kufanya ya kwake. Maana hata yeye akiperuzi mitandao haoni kitu muhimu kinacho waliza watanzania zaidi habari za upotoshaji zinazo jirudia-rudia. Mara watu wasio julikana, mara vyetu feki vya bashite, mara diamond amembusu sijuwi nani. Tunatumia hii mitandai vibaya japo ni huru kwa kila mtu kutumia
 
Rais Magufuli leo akiwaapisha Majaji 10 aliowateua pamoja na Mawakili amesema kuwa Watanzania tunaamini kila kinachoandikwa kwenye mitandao ya kijamii. Hii inatokana na kutoku-control mitandao hiyo wamiliki wako huko wao interest yao ni kutengeneza biashara wala hawajali consequences zitakazotokea

> Rais Magufuli ameongeza kuwa hadhani kama ukienda kwenye nchi kama China utakuta wana 'Google' na 'WhatsApp' kama hizi za kwetu huku

> Rais Magufuli: Kila Mtu anapojifikiria anapost chochote kwenye mitandao ya kijamii

Rais ameelezea tabia ya kuamini mijadala ya mitandaoni kama ugonjwa ambao hafahamu umetoka wapi. Ameeleza kuwa siku moja alikua akisoma mtandaoni kuhusu serikali kuiba Trilioni 1.5 ikabidi ampigie CAG kuuliza kuhusu wizi huo

======
Ikumbukwe kuwa mnamo Septemba 28 mwaka 2016 Rais Magufuli alinukuliwa akisema kuwa ''Anatamani Malaika washuke wazime mitandao ya kijamii, irudi baada ya mwaka 1 ikute hatua kubwa za kimaendeleo tulizopiga''
Hivi Rwanda na Uganda ndiyo China? Kuamini maneno ya kuambiwa nayo si dalili nzuri. Angesema Mama Samia, ningemwelewa. Hizo ni za JK.
 
Pesa zimepotea zimeibiwa whatever the case is CAG ndio muongo au mnatetea kujinufaisha wachache
Raisi asije na majibu mepesi mepesi yeye kama kiongozi hupashwi kujibu ya mtandaoni alipashwa aamuru Bunge lichunguze ukweli sio kusingizia mitandao.
He has to be responsible, own his mistakes period!

Na ndio hapo hata mimi nachangajikiwa, watu wanaimba JPM mwizi sasa militaka atoke ndani anze kujetetea wakati kuna utaratibu wa kamati za bunge kuhoji mapato na matumizi ya serikali. Taarifa ikitoka kwa CAG inepelekwa kwa rais baada ya hapo inakabidhiwa kwa bunge ili pitiwe na kamati husika kujiridhisha. Lakini watanzania kwa kutumia uhuru wao wa mitandaoni wamechukulia kama ndio mwisho na wezi wamesha julika. beleive me, huo sio mwisho na maswala hata hajaanza bado.
 
Kwenye ripoti yake, CAG hajasema popote kuwa TZS 1.5trn zimeibiwa. Alichosema leo Ikulu ndio msimamo wake uliopo kwenye Taarifa yake ukurasa wa 34. Fedha hizo HAZIONEKANI kwenye matumizi ya Serikali ya mwaka 2016/17.



Ndio maana tunahoji zipo wapi. Tunataka Ukaguzi Maalumu ili kuhakiki majibu ya Serikali na kujua hela zetu zipo wapi. Hilo tu, hakuna lingine.



Vitisho vya hatua za kisheria ni tambo tu za watawala, hazina maana yeyote. Kumsimamisha CAG Ikulu na kumhoji mbele ya Wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama ni kumtisha CAG, ni kinyume na misingi ya Katiba yetu. Ripoti ya CAG ikishakuwa mbele ya Bunge sio Ripoti ya Executive tena. Ni mali ya Bunge. Kama Rais ana majibu aende akayaseme Bungeni mbele ya PAC.



Rais sio wa kumchekea chekea anapovunja misingi ya nchi yetu. Ni lazima ADHIBITIWE na Taasisi za Kikatiba ikiwemo Bunge. Rais leo amekosea. CAG naye amekosea kwenda Ikulu.



Watanzania sikilizeni, mimi nimekuwa Mwenyekiti wa PAC/POAC miaka 8, ninajua kusoma, kuchambua na kutafsiri Taarifa ya CAG. TZS 1.5trn hazina maelezo, hazipo Benki Kuu na Maelezo ya Naibu Waziri Fedha leo ni kujikosha tu.



Nikiwa Mwenyekiti wa PAC, Mwaka 2013 Waziri wa Ujenzi John Pombe Magufuli alikutwa na Hoja ya ukaguzi ya TZS 252 bilioni ya ujenzi wa barabara hewa ambayo mpaka sasa haijajibiwa na utaikuta kwenye Hoja za CAG za mwaka 2016/17. Hivyo ni Kawaida yake kutoheshimu sheria za Fedha na kutojibu Hoja za Ukaguzi.



Kama Serikali ina uhakika kabisa hii hoja ya TZS 1.5trn haipo inipeleke mahakamani hata leo. Nitawashinda hata Jaji akiwa mmoja wa majaji wapya walioapishwa leo.



Mimi siogopi. Nitasema UKWELI daima fitina kwangu mwiko.



Zipo wapi TZS 1.5trn?
Ok. Nimekulewa.
Lakini, km unachosimamia ni kweli kwanini wewe usianze kwenda mahakani? Kwanini unataka mwizi ndio akupeleke? Sijawahi ona au kusikia mwizi anamshitaki aliyemuibia isipokuwa katika akili za zitto pekee.
Km kweli we ni mzalendo na unazo detail zote, ebu nenda kashitaki ili tujue ukweli. Kujigamba na kujisifu kwetu haisaidii kitu. Take action.
 
Usiwe mpumbavu kama bosi wako. Walioanza kupaza sauti wakitetea huu upotevu wa mabilioni ya kodi zetu unawajua vizuri kabisa nao ni mawaziri wake dikteta uchwara.

Jamani upinzani wako kwenye kamati zote za bunge, kama kuna dosari, hawatawaficha. Mbona hatujasikia kauli yoyote toka Chadema au CUF kwani wao hawana uchungu na hizi pesa? jubu ni hapana wanauchungu ila muda huu nadhani wameamuwa kufuata taratibu za kibunge.
 
Na ndio hapo hata mimi nachangajikiwa, watu wanaimba JPM mwizi sasa militaka atoke ndani anze kujetetea wakati kuna utaratibu wa kamati za bunge kuhoji mapato na matumizi ya serikali. Taarifa ikitoka kwa CAG inepelekwa kwa rais baada ya hapo inakabidhiwa kwa bunge ili pitiwe na kamati husika kujiridhisha. Lakini watanzania kwa kutumia uhuru wao wa mitandaoni wamechukulia kama ndio mwisho na wezi wamesha julika. beleive me, huo sio mwisho na maswala hata hajaanza bado.
Hapa ndio tunapopishana 'kwa nini report iendee kwa raisi na sio Bunge
Pesa zimepotea ziko wapi ndio swali weather ni nani amefuja swali pesa zipo wapi
Social Media ni sauti ya WaTz ambao ndio wenye mamlaka na hiyo pesa si vinginevyo
Richmond Escrow etc vilizungumzwa hadharani why not hii
Badala ya kujibu aagize uchunguzi ufanyike period sio kutisha watu na kutoa mfano wa China sijui hawana google na whatever. So anataka tuishi kama China hahahhaah he must be joking
Ametunga sheria ya kulipia social media sasa kila mtu atarun blog au social media nje yanTz tuone na sheria uchwara yenu. Acheni watu wahoji
Ajibu swali pesa zipo wapi simple..
 
Sasa tutajuaje kama haukuwa PAC? Huwezi kuchukua kauli ya mtu kama ilivyo halafu unabandika tu bila kumtambua. Kama shule au chuo ni umefeli maana ni wizi wa uandishi na uhuni. Inaitwa Plagirism. Hamna cha dawa kuingia wala nini!


Na hiyoo ya kwako kujiita crocodile inaitwa
palamagambanism
 
Swala muhimu, kuna taratibu za kibunge kuhoji chochote ambacho inakiona sio sawa. Ndio moja ya kazi za kamati za kudumu za bunge. Lakini kuna watu wameamuwa kujichukulia umaarufu wa haraka haraka kwa kupaza sauti pasipo hitaji kupazwa sauti. Hii sio mara ya kwanza bunge kuhoji au CAG kutowa mapungufu kwenye mapato na matumizi ya serikali.
ukihoji kuhusu watu kupaza sauti utakuwa unakosea chief"" mahali popote pale. kitika nchi hii kama unahisi kuna mahali kuna jambo Fulani ambalo haliko sawa "" NI haki yko kupaza sauti ili uweze kufahamishwa"" kumbuka kuwa hiyo nihaki yko kikatiba mkuu"" zito ni mbunge "" na mbunge anapohoji jambo/kitu ndio anakuwa anaitendea vyema CV yake maana kazi yake anayoitumikia inamtaka kufanya hivyo"""
 
Rais Magufuli leo akiwaapisha Majaji 10 aliowateua pamoja na Mawakili amesema kuwa Watanzania tunaamini kila kinachoandikwa kwenye mitandao ya kijamii. Hii inatokana na kutoku-control mitandao hiyo wamiliki wako huko wao interest yao ni kutengeneza biashara wala hawajali consequences zitakazotokea

> Rais Magufuli ameongeza kuwa hadhani kama ukienda kwenye nchi kama China utakuta wana 'Google' na 'WhatsApp' kama hizi za kwetu huku

> Rais Magufuli: Kila Mtu anapojifikiria anapost chochote kwenye mitandao ya kijamii

Rais ameelezea tabia ya kuamini mijadala ya mitandaoni kama ugonjwa ambao hafahamu umetoka wapi. Ameeleza kuwa siku moja alikua akisoma mtandaoni kuhusu serikali kuiba Trilioni 1.5 ikabidi ampigie CAG kuuliza kuhusu wizi huo

======
Ikumbukwe kuwa mnamo Septemba 28 mwaka 2016 Rais Magufuli alinukuliwa akisema kuwa ''Anatamani Malaika washuke wazime mitandao ya kijamii, irudi baada ya mwaka 1 ikute hatua kubwa za kimaendeleo tulizopiga''
Alizima bunge live akidhani atalazimisha watu kusikiliza na kutilia maanani majigambo yake. Hata akizima mitandao ya kijamii, mvuto hautarudi kwake. Hawezi kulazimisha mvuto kama ataendelea na ukandamizaji.
 
Hapa ndio tunapopishana 'kwa nini report iendee kwa raisi na sio Bunge
Pesa zimepotea ziko wapi ndio swali weather ni nani amefuja swali pesa zipo wapi
Social Media ni sauti ya WaTz ambao ndio wenye mamlaka na hiyo pesa si vinginevyo
Richmond Escrow etc vilizungumzwa hadharani why not hii
Badala ya kujibu aagize uchunguzi ufanyike period sio kutisha watu na kutoa mfano wa China sijui hawana google na whatever. So anataka tuishi kama China hahahhaah he must be joking
Ametunga sheria ya kulipia social media sasa kila mtu atarun blog au social media nje yanTz tuone na sheria uchwara yenu. Acheni watu wahoji
Ajibu swali pesa zipo wapi simple..

Taarifa kwenda Ikulu halafu bungeni ni taratibu za siku nyingi wala sio jana wala juzi. Serikali ndio inamtuma CAG akaguwe vitabu ya hesabu vya serikali, serikali inachukuwa hivyo vitabu inavikabidhi kwa bunge ili bunge lijiridhishe kama walicho idhinisha kimetumika vilivyo au la. Tatozo watanzania tena wale walio hemkia siasa siku za karibuni kuna mengi hasa hasa taratibu za kiserikali hawazijuwi na ndio maana kuna kuwa na upotoshaji mwingi mitandaoni. Nimesema acha kamati za bunge zijiridhishe na majibu ya serikali halafu ndio tutajuwa kama fedha zimepotea au la.
 
Rais angekuwa na chembe ya busara ya kawaida angewaachia mawaziri wake wamtetee kama wana moyo huo!
Watanzania tunadai triliont 1.5 .
Kwani Rais ni mhasibu?
Yeye aendelee kuzindua miradi ya wenzake ameshaiba asirudie tena!
 
ukihoji kuhusu watu kupaza sauti utakuwa unakosea chief"" mahali popote pale. kitika nchi hii kama unahisi kuna mahali kuna jambo Fulani ambalo haliko sawa "" NI haki yko kupaza sauti ili uweze kufahamishwa"" kumbuka kuwa hiyo nihaki yko kikatiba mkuu"" zito ni mbunge "" na mbunge anapohoji jambo/kitu ndio anakuwa anaitendea vyema CV yake maana kazi yake anayoitumikia inamtaka kufanya hivyo"""

Mimi sikatai kwa mtu au mwanachi yoyote kupaza sauti, sauti zikipazwa ndio tutafichuwa na mengine tusio yajuwa. Lakini unapo paza sauti wakati unajuwa utaratibu unaotumika kutoa malalamiko yako hapo utakuwa una nia nyingine ya kupaza sauti tofauti na unachokipazia sauti. Sijuwi kama umenielewa,
 
Rais Magufuli leo akiwaapisha Majaji 10 aliowateua pamoja na Mawakili amesema kuwa Watanzania tunaamini kila kinachoandikwa kwenye mitandao ya kijamii. Hii inatokana na kutoku-control mitandao hiyo wamiliki wako huko wao interest yao ni kutengeneza biashara wala hawajali consequences zitakazotokea

> Rais Magufuli ameongeza kuwa hadhani kama ukienda kwenye nchi kama China utakuta wana 'Google' na 'WhatsApp' kama hizi za kwetu huku

> Rais Magufuli: Kila Mtu anapojifikiria anapost chochote kwenye mitandao ya kijamii

Rais ameelezea tabia ya kuamini mijadala ya mitandaoni kama ugonjwa ambao hafahamu umetoka wapi. Ameeleza kuwa siku moja alikua akisoma mtandaoni kuhusu serikali kuiba Trilioni 1.5 ikabidi ampigie CAG kuuliza kuhusu wizi huo

======
Ikumbukwe kuwa mnamo Septemba 28 mwaka 2016 Rais Magufuli alinukuliwa akisema kuwa ''Anatamani Malaika washuke wazime mitandao ya kijamii, irudi baada ya mwaka 1 ikute hatua kubwa za kimaendeleo tulizopiga''
Hii kauli maana yake ni kwamba .mitandao ni adui mpya kwa sasa .Ilo ni agizo tusubiri tuu sasa mashambulizi .Mungu tusaidie hii safari ya kuelekea North Korea isifanikiwe .duuh nchi imekuwa nyumbani kwa mtu
 
Back
Top Bottom