Rais Magufuli: Wastaafu wengine hawachoki kusema, wanawashwa washwa

Uzi huu hauna lengo la kukashifu wala kuchochea,bali kutaka kujua tu orodha kamili ya kile alichokisema Mheshimiwa sana na mzalendo pekee kwa sasa katika Taifa hili.



Nanukuu sehemu ya hotuba yake ambayo ndio ilibeba dhima nzima ya hotuba yake leo Ikulu...."

"Hawa majaji ni waadilifu sana. Huwezi kumsikia jaji Chande anazungumza chochote au majaji wengine. Tofauti na wastaafu wa sehemu nyingine, wanawashwa washwa sana. Nawapongeza sana waheshimiwa majaji"

Najaribu kuwaza,kuwashwa huko anakokutaja mheshimiwa mtukufu sana ni kule kukosoa utawala wake ama muwasho wa wapi na kwa wakati gani?!

Benjamin Mkapa ambae haishi kuita Watanzania wajinga na wapumbavu ni sehemu ya wastaafu haowanaowashwa washwa?! Ama hahusiki kwa kuwa amekuwa akisifia utawala huu na kwa kuwa kama ni mhunzi basi alishiriki kuchonga kinyago cha sebuleni?!!

Dhana ya wanaowashwa washwa ni kwa wanaosifu utawala huu na raisi wake pia ama ni kwa wakosoaji tu?! Mfano raisi Mwinyi alisema anatamani Magufuli atawale milele,nae alikuwa anawashwa washwa?! Je ni kosa la jinai ama uhaini kuwashwa katika awamu hii?!!!

Watu wakisema raisi hashauriki na wala haambiliki na ukitoa maoni yako tarajiwa kushutumiwa ama kufunguliwa kesi kama za Lissu na ikibidi mitutu juu,ni kosa?!!!

Hotuba hizi za rasha rasha na jumla jumla,huandaliwa na muandishi wa hotuba wa raisi ama ni mahaba yake msemaji kadri imfaavyo?!! Kama ni maneno ya muandishi wa hotuba wa raisi,kwa nini nae asikamatwe na kufunguliwa kesi za uchochezi za kumchochea muongeaji mbele ya umma?! Kama hotuba hizi ni za msemaji mwenyewe,mwandishi wa hotuba wa raisi sio mtumishi hewa?!!

Hahahahahaaaaaa!

Labda tumuulize RZ1 atakuwa ameelewa
 
Ni kweli hawa waheshimiwa hawawashwiwashwi lakini wanafuatilia kwa makini kilicho tokea Kenya. Sifa hizi zitayeyuka tu wakitengua matokeo endapo yale ya Zanzibar na Jecha yakitokea tena.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
God Bless
Uzi huu hauna lengo la kukashifu wala kuchochea,bali kutaka kujua tu orodha kamili ya kile alichokisema Mheshimiwa sana na mzalendo pekee kwa sasa katika Taifa hili.



Nanukuu sehemu ya hotuba yake ambayo ndio ilibeba dhima nzima ya hotuba yake leo Ikulu...."

"Hawa majaji ni waadilifu sana. Huwezi kumsikia jaji Chande anazungumza chochote au majaji wengine. Tofauti na wastaafu wa sehemu nyingine, wanawashwa washwa sana. Nawapongeza sana waheshimiwa majaji"

Najaribu kuwaza,kuwashwa huko anakokutaja mheshimiwa mtukufu sana ni kule kukosoa utawala wake ama muwasho wa wapi na kwa wakati gani?!

Benjamin Mkapa ambae haishi kuita Watanzania wajinga na wapumbavu ni sehemu ya wastaafu haowanaowashwa washwa?! Ama hahusiki kwa kuwa amekuwa akisifia utawala huu na kwa kuwa kama ni mhunzi basi alishiriki kuchonga kinyago cha sebuleni?!!

Dhana ya wanaowashwa washwa ni kwa wanaosifu utawala huu na raisi wake pia ama ni kwa wakosoaji tu?! Mfano raisi Mwinyi alisema anatamani Magufuli atawale milele,nae alikuwa anawashwa washwa?! Je ni kosa la jinai ama uhaini kuwashwa katika awamu hii?!!!

Watu wakisema raisi hashauriki na wala haambiliki na ukitoa maoni yako tarajiwa kushutumiwa ama kufunguliwa kesi kama za Lissu na ikibidi mitutu juu,ni kosa?!!!

Hotuba hizi za rasha rasha na jumla jumla,huandaliwa na muandishi wa hotuba wa raisi ama ni mahaba yake msemaji kadri imfaavyo?!! Kama ni maneno ya muandishi wa hotuba wa raisi,kwa nini nae asikamatwe na kufunguliwa kesi za uchochezi za kumchochea muongeaji mbele ya umma?! Kama hotuba hizi ni za msemaji mwenyewe,mwandishi wa hotuba wa raisi sio mtumishi hewa?!!


Wakati Mwingine Tumsikilize Mh. Rais Wetu!
Kila wakati anaomba Tumuombee! Kile Kiti ni Kigumu sana! wewe unasumbuka na wawekezaji! wengine wanasema vileee!
Mungu Amsaidie Rais wetu awe na Moyo wa Uvumilivu na Kuchukuliana na Watanzania! Ni hulka yetu kusema sema.
Lakini ni Haki ya Watu kikatiba! (freedom of expression) kama hawavunji sheria.
Baba Magufuli wakati mwingine Uishinde caliber yako ya Ukali! Mungu akusaidie katika hili.
Mh. Rais Mungu akupe Kifua cha kuvumilia tu! Kusikia na kusamehe!
Kikwete alisemwa sana wakati wa utawala wake akakereka kama wewe! ila yeye hakutumia hayo maneno ya hivyo...
Waziri mmoja waliwahi kuwaambia watu watakula hata nyasi ila ndege ya Rais lazima inunuliwe.
Mzee mmoja wa muda mrefu Bungeni aliwahi kuwajibu wanaopenda kusema sema - Wanawivu wa kike! Aliwahi pia kulaani sana uwepo Jamii Forums.
Mh. Rais Vumilia ndivyo tulivyo Waswahili.
 
Huyu mtu iko siku atamtukana mama yake mzazi.hivi kuna raisi anaudhaifu wa matumizi ya kinywa duniani kama huyu ? Mungu nakusihi na kukulilia Weka kaa la moto kinywani mwa huyu mwovu nebkadreza.hachagui lakusema wala pakusemea ! Hili ni jaribu kubwa na baya kuwahi kutokea nchini.sasa hatujui kumpongeza Uhuru alijenga au ndo katuhatarisha.Uhuru hakupendezwa mtu kwenda kutembea kwa wengine na kuzungumzia ukabila wa wakenya kwa madai ni mpenzi wa mungu,huku ana muuwa Lisu.odinga hakupendezwa kuambiwa uraisi umemshinda mara kadhaa aende akauze nyanya ! Hiki kiburi na uchafu wa kauli mpaka kwa nchi za wengine ni cha kawaida?Mange sasa taratibu tu,wengi tutamuelewa.Mungu beba hili jaribu Wewe mwenye nguvu na uweza wote,huyu mtu asije kutuponza kama nchi tuingie kwenye magomvi na majirani,Amen.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ngosha katimba town anatumia neno lolote bila kujua athari yake...... kuwashwa washwa akiambiwa yeye watu watakuja lalamika hapa
 
Kwani kuwashwa washwa ni neno baya!? Nini hasa lengo lako kuandika hayo yote kunzungumzia Raisi wetu mpendwa!?
Unahitaji kujiongeza na ujicheke... na sio kuja kutafuta kiki humu[/
Sumaye na Lowasa
Itakuwa ni Kikwete, na ile kauli yake kwamba wapinzani siyo maadui. itakuwa imemkera sana JPM. Kwake upinzani, hasa wa chama kikuu cha upinzani, ni maadui namba moja. ndio maana Polisi wako bize na wapinzani, kazi namba moja ya wakuu wa wilaya na mikoa ni kushughulika na wapinzani. ndiyo maana sheria za kuweka mtu kizuizini masaa 48 sasa hivi inatumika hasa kwa wapinzani.
 
The Valiant, umesema kila kitu na tunapata picha ni kwa kiasi gani vyama vya siasa shindani vinavyomkera rais wetu kwa kukosoa uongozi wake. Kwamba hata kauli za akina JK, Mwandosya hawezi kuzivumilia speaks volumes of his character.
 
Kustaafu ni jambo la kheri, Mh. Rais ameamsha tafakuri nzito, nimeona wengine wamebaki hapo wakijadiliana Kuwashwa, lkn kubwa ninaloliona Rais kawauliza mlipokuwa madarakani mlifanya nini ambacho mnataka kutuambia leo, au je mlisahau nini ambacho mnataka kukikamilisha leo?
Fundisho ni,, mliomadarakani leo Jengeni hali njema ya kesho, leo imepita, ili siku mkistaafu muendelee kufurahia mfumo mlioacha, na sio kujenga matarajio yenu kwa kuachia madaraka unae mfahamu, hesabu huwa zinagoma
 
Hii ya kuwashwawashwa ni kali. Ni juzi tu baadhi ya wastaafu walikuwa magogoni wakaambiwa msisite kutushauri. Je, huo nao siyo kuwafanya wawashwe?
 
Back
Top Bottom