Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,288
- 9,719
Ndugu zangu Watanzania,
Mheshimiwa Paul Makonda Katibu wa itikadi, uenezi na mafunzo wa CCM Taifa hapo jana huko babati Mkoani Manyara ametoa hotuba ya mwaka,hotuba iliyoteka na kugusa hisia za watu,hotuba iliyowafanya watu washindwe kujizuia machozi na hivyo kujikuta wakibubujikwa na kutiririka machozi kutoka katika macho yao,hotuba iliyoacha historia na kuwatia moyo wana babati.
Ni baada ya kusema kuwa Ukimchukia Rais Samia unakuwa Unamkosea Mungu Mwenyewe,kwa kuwa Rais Samia alijipangia kuishi maisha ya kawaida kabisa na wala hakuwahi kupanga wala kuwaza kuwa makamu wa Rais wala Rais wa Tanzania.lakini Mungu na mipango yake alipanga iwe hivyo kwa kumuinua na kumpa umakamu wa Rais na baadaye Urais.
Mheshimiwa Makonda aliendelea kusema kuwa hata yeye hapo alipo kwa sasa ni mipango ya Mungu Mwenyewe aliye juu na wala siyo mipango yake,maana alikuwa tayari yupo nje ya msitari. Aliendelea kuzungumza huku wananchi wakitekwa na hotuba hiyo iliyojaa hisia kali sana na mguso wa aina yake kwa kusema kuwa hata wao wasikate tamaa na wajipe moyo na wala wasiumie wanapodharauliwa na mtu.
Kwa hakika Mheshimiwa Makonda ni mtu ambae ukisikiliza hotuba zake lazima uguswe sana ndani ya moyo wako, ni mtu anayezungumza toka ndani kabisa ya moyo wake, ni mtu anayeongea na kuzungumza kwa kugusa hisia za watu,anaongea uhalisia wa maisha, anazungumza kile kinachogusa yale yaliyopo kwa watu na wananchi.ndio maana watu wanafurika na kumiminika sana kwenye mikutano yake.
Ni mtu ambae ukimsikiliza unapata matumaini na nguvu kubwa sana ya kusonga mbele kimapambano, maana anatia moyo na faraja sana ya kutokukata tamaa wala kujikatia tamaa wala kukatishwa tamaa na mtu yeyote yule.
Ni mtu ambaye anakuonyesha na kukupa nguvu kuwa ujapodharaulika leo mbele za wanadamu lakini mbele za Mungu una thamani sana na unaweza inuliwa na Mungu wakati wowote ule kutoka chini na kukuketisha mahali pa juu na mahali pa heshima,bila kujali historia yako,kipato chako wala familia uliotokea.kikubwa ni kuwa na imani, mnyenyekevu,tabia njema,ucha Mungu na hofu ya Mungu.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.
Mheshimiwa Paul Makonda Katibu wa itikadi, uenezi na mafunzo wa CCM Taifa hapo jana huko babati Mkoani Manyara ametoa hotuba ya mwaka,hotuba iliyoteka na kugusa hisia za watu,hotuba iliyowafanya watu washindwe kujizuia machozi na hivyo kujikuta wakibubujikwa na kutiririka machozi kutoka katika macho yao,hotuba iliyoacha historia na kuwatia moyo wana babati.
Ni baada ya kusema kuwa Ukimchukia Rais Samia unakuwa Unamkosea Mungu Mwenyewe,kwa kuwa Rais Samia alijipangia kuishi maisha ya kawaida kabisa na wala hakuwahi kupanga wala kuwaza kuwa makamu wa Rais wala Rais wa Tanzania.lakini Mungu na mipango yake alipanga iwe hivyo kwa kumuinua na kumpa umakamu wa Rais na baadaye Urais.
Mheshimiwa Makonda aliendelea kusema kuwa hata yeye hapo alipo kwa sasa ni mipango ya Mungu Mwenyewe aliye juu na wala siyo mipango yake,maana alikuwa tayari yupo nje ya msitari. Aliendelea kuzungumza huku wananchi wakitekwa na hotuba hiyo iliyojaa hisia kali sana na mguso wa aina yake kwa kusema kuwa hata wao wasikate tamaa na wajipe moyo na wala wasiumie wanapodharauliwa na mtu.
Kwa hakika Mheshimiwa Makonda ni mtu ambae ukisikiliza hotuba zake lazima uguswe sana ndani ya moyo wako, ni mtu anayezungumza toka ndani kabisa ya moyo wake, ni mtu anayeongea na kuzungumza kwa kugusa hisia za watu,anaongea uhalisia wa maisha, anazungumza kile kinachogusa yale yaliyopo kwa watu na wananchi.ndio maana watu wanafurika na kumiminika sana kwenye mikutano yake.
Ni mtu ambae ukimsikiliza unapata matumaini na nguvu kubwa sana ya kusonga mbele kimapambano, maana anatia moyo na faraja sana ya kutokukata tamaa wala kujikatia tamaa wala kukatishwa tamaa na mtu yeyote yule.
Ni mtu ambaye anakuonyesha na kukupa nguvu kuwa ujapodharaulika leo mbele za wanadamu lakini mbele za Mungu una thamani sana na unaweza inuliwa na Mungu wakati wowote ule kutoka chini na kukuketisha mahali pa juu na mahali pa heshima,bila kujali historia yako,kipato chako wala familia uliotokea.kikubwa ni kuwa na imani, mnyenyekevu,tabia njema,ucha Mungu na hofu ya Mungu.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.