Rais Magufuli, ukitoa ushauri unatakaje tena taarifa?

mr yamoto

JF-Expert Member
Oct 2, 2016
923
1,393
INAONEKANA Serikali inahitaji fedha, ndio sababu ya msingi kuongeza hizo siku 7. WAPO waliogoma kurejesha fedha. Kama watuhumiwa 467 wamejitokeza kurejesha bilioni 100 ni wazi wapo "MAPAPA" wamegoma kupiga magoti. Habinder Seth na Rugemalira pekee tuhuma zao ni 306bn. KAZI IPO!

Nimemsikiliza Rais akisema anaongeza siku nyingine 7 kwa watuhumiwa wa uhujumu uchumi kuomba radhi, kukiri kosa na kurejesha fedha, swali la msingi, mashtaka ya uhujumu uchumi, Rais anatajwa wapi katika sheria ya uhujumu uchumi kutoa msamaha kwa washitakiwa?

TAKUKURU wakamkamata Rugemalira, mahakama ya kuu, divisheni ya makosa ya uhujumu uchumi na rushwa ikamnyima dhamana kwa makosa ya uhujumu uchumi 350bn/- Mahakama ya rufaa ikagoma kutoa rufaa, Baadae RAIS anasema "kubali kosa, omba radhi, rejeshe fedha kuwa huru"

Maneno ya James Rugemalira 19.06.2019 mahakama ya rufaa

"kama ndivyo, naondoa rufaa. Sihitaji dhamana. Acha nibaki mahabusu hadi siku ya kusikilizwa shauri langu. Acha nibaki magereza, waache wanifunge kumaliza hili,natuhumiwa kuiba vitu ambavyo sijafanya. Naonewa bila kosa"
Baadae anakuja Rais anamueleza mtu huyu kwamba, akiri kosa, aombe radhi na alipe fedha hizo fedha anazotuhumiwa. UONEVU! DHULUMA! kukamata raia bila ushahidi, kubambikia mashtaka Baadae kuwataka walipe fedha ili waachiwe huru ni DHULUMA na UKATILI. Acheni kuwaonea watu.

Rais wangu nini tatizo.
 
Ruge alivyokuwa anabeba pesa kwenye masandarusi kama mchele alisahau?

Wakati wanakula walikua wanashinda angani kwenda ulaya

Leo wanatafuta huruma kwa Wananchi waliowaibia?

Sisi tulishazoea shida wao wameguswa kidogo tu kelele
Kwani hao wengine wanaorudisha wanatofauti gani nae au kwasababu yeye kasema ukweli.
 
Ruge alivyokuwa anabeba pesa kwenye masandarusi kama mchele alisahau?

Wakati wanakula walikua wanashinda angani kwenda ulaya

Leo wanatafuta huruma kwa Wananchi waliowaibia?

Sisi tulishazoea shida wao wameguswa kidogo tu kelele
Serikali ilishindwa kesi kwenye mahakama ya uwekezaji. Ndiyo maana ikazitoa. Kwani si ni serikali hiyohiyo iliyozuia fedha kwenye akaunti ya escrow? Mbona leo inatafuta kuwanyang' anya? Kwanini wasthibitishe uhalifu wao. Anaekiri kosa no yule aliyelifanya. Sio asiyelifanya. Hoja ya IPTL ilikuwa capacity charge kubwa. Na ilikuwa kimkataba. Ubabe tu.
 
eti anashauri alafu anataka mrejesho wa 'utekelezaji wa ushauri', na antoa na 'dead line'. huyu mtu ana matatizo ya uelewa wa mambo kwa ujumla, ni mtu mwenye akili za wastani na hekima pungufu.
Ombi la mkubwa ni amri! Hiyo ni kanuni ya asili. Ndio maana maombi yanayotoka kwa wakubwa hayakataliwi.
 
Ruge alivyokuwa anabeba pesa kwenye masandarusi kama mchele alisahau?

Wakati wanakula walikua wanashinda angani kwenda ulaya

Leo wanatafuta huruma kwa Wananchi waliowaibia?

Sisi tulishazoea shida wao wameguswa kidogo tu kelele
Ukiongelea kuhusu kuiba kipindi hicho wote walikuwa wezi hata unaemshabikia wewe ukifunuliwa yake yote utalia sana....mana hayasemwi kutokana na alipo ila asingekuwepo hapo ungeyajua yote
 
Ruge alivyokuwa anabeba pesa kwenye masandarusi kama mchele alisahau?

Wakati wanakula walikua wanashinda angani kwenda ulaya

Leo wanatafuta huruma kwa Wananchi waliowaibia?

Sisi tulishazoea shida wao wameguswa kidogo tu kelele
Wakati wabunge walipochachamaa hasa wapinzani wakati ule Bungeni kwenye issue ya ESCROW mpaka wengine wakaitwa matumbili huyo mtoa msamaha unakumbuka alikuwa wapi? Umesikia akipinga chochote?
 
Kweli hawa mafisadi kina seth warudishe pesa za Wananchi
Wakati wabunge walipochachamaa hasa wapinzani wakati ule Bungeni kwenye issue ya ESCROW mpaka wengine wakaitwa matumbili huyo mtoa msamaha unakumbuka alikuwa wapi? Umesikia akipinga chochote?
 
Back
Top Bottom