Ciprofloxacin.
JF-Expert Member
- Apr 15, 2015
- 1,583
- 2,702
Mungu amejibu maombi yako, na haja ya moyo wako, ni nani asiyejua kuwa wewe hutaki kabisa upinzani Tanzania?
Hujifichi kuonyesha chuki yako hadharani dhidi ya upinzani.
Naomba nikuulize Tafadhali mheshimiwa Rais, Kama nitakukosea nisamehe bure .
Risasi alizomiminiwa Tundu Lissu na watu wanaoitwa "wasiojulikana ". ingekuwa risasi hizo kwa mfano kamiminiwa mkuu wa mkoa au waziri yoyote, hao wahalifu wangekuwa hawajapatikana?
Tuna makovu ya mateso mengi, kuwa mpinzani hapa Tanzania ni kuchagua kifo, bado tunamwomboleza mawazo, Ben Saanane, Kanguye, Azori Gwanda na wengine wengi.
Mheshimiwa Rais, hatutaki kupiga kura ili tukipishe chama chako kitawale milele Kama wewe unavyotaka sasa wakuu wa mikoa na wilaya watatufanyaje?
Tumeamua kupumzika ili nyie mnaopendwa sana muendelee kupendwa na kutawala milele, ajabu tena imekuwa kero.
Na 2020 pia hatutapiga kura, tuache tupumzike, Tafadhali Tumechoka.
Wana CCM wapo wengi watapiga kura na kujipatia ushindi mnono.
Tumeshajua hata tukipiga kura hatushindi kwa sababu CCM huwa inashinda hata kabla ya kupiga kura sasa tunapiga kura za nini?
Tuache tupumzike.
Hujifichi kuonyesha chuki yako hadharani dhidi ya upinzani.
Naomba nikuulize Tafadhali mheshimiwa Rais, Kama nitakukosea nisamehe bure .
Risasi alizomiminiwa Tundu Lissu na watu wanaoitwa "wasiojulikana ". ingekuwa risasi hizo kwa mfano kamiminiwa mkuu wa mkoa au waziri yoyote, hao wahalifu wangekuwa hawajapatikana?
Tuna makovu ya mateso mengi, kuwa mpinzani hapa Tanzania ni kuchagua kifo, bado tunamwomboleza mawazo, Ben Saanane, Kanguye, Azori Gwanda na wengine wengi.
Mheshimiwa Rais, hatutaki kupiga kura ili tukipishe chama chako kitawale milele Kama wewe unavyotaka sasa wakuu wa mikoa na wilaya watatufanyaje?
Tumeamua kupumzika ili nyie mnaopendwa sana muendelee kupendwa na kutawala milele, ajabu tena imekuwa kero.
Na 2020 pia hatutapiga kura, tuache tupumzike, Tafadhali Tumechoka.
Wana CCM wapo wengi watapiga kura na kujipatia ushindi mnono.
Tumeshajua hata tukipiga kura hatushindi kwa sababu CCM huwa inashinda hata kabla ya kupiga kura sasa tunapiga kura za nini?
Tuache tupumzike.