Rais Magufuli toa onyo kuhusu mavazi ya dada zetu, ni aibu tupu

Mh. Rais Magufuli natumai hujambo na ni mwingi wa afya njema, hata mimi mwananchi wako niko salama na wa afya njema nikiendelea kujivunia kuwa mtanzania nnaeheshimika kwa sasa kwa sababu ya uongozi wako mathubuti.

Mh. Rais sitaki nikuchoshe sana acha nikujuze tu jambo hili linalotukera sana huku mtaani japo nafahamu huenda unafahamu pia.

Mh. Rais kwa maadili ya kitanzania na jamii nzima ya watanzania mdada au mwanamke kuvaa nguo zinazobana na kuchola mwili hutafusiliwa ni kukosa heshima kwa jamii, lakini pamoja na hilo dada zetu huku mjini ndio wanazidi kuvaa hivi vinguo vya aibu kiasi kwamba akipita usoni pengine umekaa na mama au baba huenda ukalazimika kufumba macho ili apite kwani ni fedhea na aibu ya aina yake.

Mh. Rais natambua kuwa kauli yako ni sheria kwetu na ukitamka sie lazima tutekeleze hivyo basi nakuomba kwa niaba ya wapenda maadili utoe kauli inayozuia uvaaji huu wa aibu, zaidi nikutakie afya njema na nnazidi kukuombea kwa mungu aendelee kukupa nguvu nyingi na kheri katika utumishi wako.
O
Nenda kwenye nyumba za makumbusho ili uone mila za mavazi ya kitanzania au kiafrika. Wasichana hawakuvaa chochote juu, walijifunga gome la mti chini basi.Kama unataka turudi kwenye maadili ya kitanzania ni hapo kila mtu atakavyokaa uchi. Angalia picha za wasichana wa Swaziland ndivyo wadada wa Tanzania walikuwa wakivaa. Sisi si waarabu wala wazungu wa miaka ya 30s ambao walikuwa wanafunika miili yao yote.
 
Wasukuma bana ni shiiidaaa, ndo maana MWL.Nyerere alikuwa na wasiwasi na kabila hili kupewa mamlaka ya juu katika nchi hii.

Yaani wengi wao huwa wanamisifa, ushamba, na majigambo ya kijinga, kwa hiyo sasa kwao kila tamko la Rais eti ni sheria, upumbavu wa kiwango cha rami huu, ujinga wa kila kitu " ndoho tabhu".
rami=lami. ndoho=ndo. tabhu=tabu.
 
Poleka ushamba wako wa miaka mia moja iliyopita huko. Mwanamke akivaa nguo ya kubana amekubana wewe? Kama wewe ni mkereketwa wa ''kufundisha heshima'' basi fundisha mkeo na watoto wako namna ya kuvaa. Huna mamlaka wala uwezo wa kumpangia mtu avae nini. Hata rais wa nchi hana mamlaka ya kupangia watu wavae namna gani!
mkuu..korea kaskazini wanaume wanaruhusiwa kunyoa stail 27 tu..nje ya hapo ni kosa kisheria...rais ni mungu wa nchi
 
Haya, na hili mnipe jibu. Akinamama wa Kihindi wanavaa maguo mareefuuu lakini tumbo,kitovu,mgongo laiiini nje nje, hawa wapo kundi gani? Ati nguo fupi ni kinyume cha utamaduni wa mwafrika, wakati waafrika walikuwa wanavaa magome ya miti na wengine uchi kabisa, nguo nyingi zilikuwa ni zile za Makhirikhiri! Na kwa nini kuvaa nguo fupi, kudai huyu ama yule yuko uchi ni kwa wanawake tu?
 
Mh. Rais Magufuli natumai hujambo na ni mwingi wa afya njema, hata mimi mwananchi wako niko salama na wa afya njema nikiendelea kujivunia kuwa mtanzania nnaeheshimika kwa sasa kwa sababu ya uongozi wako mathubuti.

Mh. Rais sitaki nikuchoshe sana acha nikujuze tu jambo hili linalotukera sana huku mtaani japo nafahamu huenda unafahamu pia.

Mh. Rais kwa maadili ya kitanzania na jamii nzima ya watanzania mdada au mwanamke kuvaa nguo zinazobana na kuchola mwili hutafusiliwa ni kukosa heshima kwa jamii, lakini pamoja na hilo dada zetu huku mjini ndio wanazidi kuvaa hivi vinguo vya aibu kiasi kwamba akipita usoni pengine umekaa na mama au baba huenda ukalazimika kufumba macho ili apite kwani ni fedhea na aibu ya aina yake.

Mh. Rais natambua kuwa kauli yako ni sheria kwetu na ukitamka sie lazima tutekeleze hivyo basi nakuomba kwa niaba ya wapenda maadili utoe kauli inayozuia uvaaji huu wa aibu, zaidi nikutakie afya njema na nnazidi kukuombea kwa mungu aendelee kukupa nguvu nyingi na kheri katika utumishi wako.

Very idiotic post (sorry for harsh language). Why should the President or any other person determine what people put on their bodies? Na hayo maadili yameandikwa wapi?

Will that bring food on the table?

Please mwambie Rais wetu ahangaikie ajira za vijana, ukusanyaji kodi, huduma bora za afya nk. Hayo yanatuhusu wote na yana tija kwa taifa letu.

As for me, I believe kila mtu ana haki ya kuvaa apendavyo. Siamini katika juhudi wachache kama nyinyi kutaka watu waishi mnavyotaka nyinyi.

Your life your responsibility. My life my responsibility.
 
Kuna baadhi ya vyuo, ofisi na taasisi unarudishwa ukabadilishe nguo kama umeenda kupata huduma za kiofisi sio tu kwa wanawake bali hata wanaume wakivaa trak suti au jinz vimodo
 
Wahache Bro kukosa kujiamini kwao wameona huko ndiko kwenye kutangaza uzuri wao.
Kama wasemavyo zama ujirudia naona wanarudi wakati wa Eva.
 
Yaani avae mwingine alafu aibu uone wewe!! Basi endelea kufumba macho tu.
 
Waambie wazazi waanze kukemea hilo jambo kwa watoto wao. Viongozi wa dini wako wapi? Acha kumbebesha mzigo Rais wetu kwa mambo yanayoweza kufanywa na watu wengine, ikiwemo sisi wananchi.
 
Back
Top Bottom