MOTOCHINI
JF-Expert Member
- Jan 20, 2014
- 27,580
- 30,025
Rais John pombe Magufuli leo amesema Rais wa Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta alimpigia simu na kumpa pole
Pia Rais Magufuli amesema kuwa wamezungumzia mgogoro ulipo mipakani mwa nchi hizi mbili na kuamua mawaziri wa pande zote mbili wanaohusika na Uchukuzi kukutana.
---
Kenyatta alinipigia simu nikiwa Chato. Leo pia kanipigia tumezungumza pia. Tumezungumza kama migogoro kule mipakani. Kenya ni marafiki zetu. Tumekubaliana mawaziri wetu wa uchukuzi na wakuu wa Mikoa watakutana mpakani na Kenya wazungumze hili walimalize.
Hii korona isiwe chanzo cha migogoro. Haiwezekani kila dereva anayekwenda huko awe na korona. Nawaomba viongozi wa mikoa inayopakana na Kenya wasitatue matatizo yao kwa jazba. Wazingatie uchumi wa nchi zetu.
Ninafahamu mtu ukichokozwa kidogo ukanyamaza, na wewe unachokoza kidogo. Nataka Wakenya na Watanzania wafanye biashara vizuri”
Naomba, na kwakuwa tumezungumza vizuri na Mheshimiwa Kenyatta, sisi tumeyamaliza.
Haiwezekani mtu anasafiri anaenda nchi jirani anaambiwa akae mpaka sijui siku ngapi wakati amepakia bidhaa
Korona haikuwanzia Afrika. Na imewakoromea wote hata wale wenye uwezo.
Pia Rais Magufuli amesema kuwa wamezungumzia mgogoro ulipo mipakani mwa nchi hizi mbili na kuamua mawaziri wa pande zote mbili wanaohusika na Uchukuzi kukutana.
---
Kenyatta alinipigia simu nikiwa Chato. Leo pia kanipigia tumezungumza pia. Tumezungumza kama migogoro kule mipakani. Kenya ni marafiki zetu. Tumekubaliana mawaziri wetu wa uchukuzi na wakuu wa Mikoa watakutana mpakani na Kenya wazungumze hili walimalize.
Hii korona isiwe chanzo cha migogoro. Haiwezekani kila dereva anayekwenda huko awe na korona. Nawaomba viongozi wa mikoa inayopakana na Kenya wasitatue matatizo yao kwa jazba. Wazingatie uchumi wa nchi zetu.
Ninafahamu mtu ukichokozwa kidogo ukanyamaza, na wewe unachokoza kidogo. Nataka Wakenya na Watanzania wafanye biashara vizuri”
Naomba, na kwakuwa tumezungumza vizuri na Mheshimiwa Kenyatta, sisi tumeyamaliza.
Haiwezekani mtu anasafiri anaenda nchi jirani anaambiwa akae mpaka sijui siku ngapi wakati amepakia bidhaa
Korona haikuwanzia Afrika. Na imewakoromea wote hata wale wenye uwezo.