mcfm40
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 4,452
- 3,152
Mh rais, napenda kukumbusha tu kwamba uliahidi kuhamia Dodoma rasmi kabla ya mwisho wa mwaka huu.
Napenda kukukumbusha kwamba bado tunaikumbuka ahadi yako na tunategemea kukuona ukihamia Dodoma mwaka huu kama ulivyoahidi.
Hata hivyo huku mwaka ukielekea ukingoni hatuoni dalili wala amsha amsha ya maandalizi ya wewe kuhamia Dodoma. Ifahamike kwamba hili ni jambo kubwa sana na la kihistoria. Hivyo tungetegemea katika muda huu mfupi uliobakia tuone maandalizi kabambe. Mfano, hali ya Ikulu ya Dodoma na utayari wake wa kukupokea na mambo mengine kede wa kede.
Kinyume chake kuna ukimya usiokuwa wa kawaida. Sio mkuu wa mkoa wa Dodoma wala mamlaka nyingine zinazohusika zinazohusika wanaonekana kuwa excited na ujio wako Dodoma ndani ya miezi hii miwili.
Pamoja na hayo, ni muhimu sana mh rais uhamie Dodoma haraka kama ulivyoahidi ili kuweza kuokoa kiasi kikubwa cha fedha kinachopotea sasa kwa viongozi wengi kulazimika kurudi Dar kila mara ili kukuunga mkono katika shugjuki unazofanya huku Dar. Mara nyingi makamu wa rais yupo Dar, waziri mkuu yupo Dar( leo yupo anakagua ujenzi wa madaraja ya tazara na ubungo), wakuuu wa majeshi, na viongozi wengi waandimizi serikalini wanalazimika kuwa na route za Dar- Dom kila mara. Yote haya yanatumia pesa nyingi za watanzania bula sababu.
Tafadhali mh kama tumeamua kuhamia Dodoma basi tufanye kweli tukae Dodoma. Ksma bado Dar kutamu nanatamani kuwepo muda wote basi iwe wazi kwamba serikali itakuwa na makao makuu Dar na Dodoma simultaneously. Hapa tutawaelewa.
Tafadhali oneeni huruma kodi zetu, wananchi tunaumia.
Napenda kukukumbusha kwamba bado tunaikumbuka ahadi yako na tunategemea kukuona ukihamia Dodoma mwaka huu kama ulivyoahidi.
Hata hivyo huku mwaka ukielekea ukingoni hatuoni dalili wala amsha amsha ya maandalizi ya wewe kuhamia Dodoma. Ifahamike kwamba hili ni jambo kubwa sana na la kihistoria. Hivyo tungetegemea katika muda huu mfupi uliobakia tuone maandalizi kabambe. Mfano, hali ya Ikulu ya Dodoma na utayari wake wa kukupokea na mambo mengine kede wa kede.
Kinyume chake kuna ukimya usiokuwa wa kawaida. Sio mkuu wa mkoa wa Dodoma wala mamlaka nyingine zinazohusika zinazohusika wanaonekana kuwa excited na ujio wako Dodoma ndani ya miezi hii miwili.
Pamoja na hayo, ni muhimu sana mh rais uhamie Dodoma haraka kama ulivyoahidi ili kuweza kuokoa kiasi kikubwa cha fedha kinachopotea sasa kwa viongozi wengi kulazimika kurudi Dar kila mara ili kukuunga mkono katika shugjuki unazofanya huku Dar. Mara nyingi makamu wa rais yupo Dar, waziri mkuu yupo Dar( leo yupo anakagua ujenzi wa madaraja ya tazara na ubungo), wakuuu wa majeshi, na viongozi wengi waandimizi serikalini wanalazimika kuwa na route za Dar- Dom kila mara. Yote haya yanatumia pesa nyingi za watanzania bula sababu.
Tafadhali mh kama tumeamua kuhamia Dodoma basi tufanye kweli tukae Dodoma. Ksma bado Dar kutamu nanatamani kuwepo muda wote basi iwe wazi kwamba serikali itakuwa na makao makuu Dar na Dodoma simultaneously. Hapa tutawaelewa.
Tafadhali oneeni huruma kodi zetu, wananchi tunaumia.