kivyako
JF-Expert Member
- Feb 2, 2012
- 14,342
- 12,066
Vuta subira siku bado zipo mwaka haujaisha!Vp mchakato umefika wap
Sent using Jamii Forums mobile app
Vuta subira siku bado zipo mwaka haujaisha!Vp mchakato umefika wap
teh teh teh tehAtasema anahujumiwa na mabeberu ili asihamie Dodoma
Kwani bahari ndio kigezo cha kuwa mji mkuu? mbona hatutaki kuelewa. nchi ngapi duniani mpaka nchi kubwa miji mikuu haiko katika fukwe za bahari na miji imeendelea sana tu. lazima tutofautishe mji wa kibiashara na na mji wa kisiasa. Dar utabaki biashara na sio lazima mji mkuu. Europe ndio kabisa miji mingi mikuu sio baharini hata baadhi ya Africa. ingekuwa hivyo basi Newyork ungekuwa mji mkuu au LA maana ndio kwenye biashara na watu wengi.Anatala kuhama na bahari aende nayo Dodoma
Bado siku mbili mwaka uisheRais Magufuli Kuhamia Dodoma Mwaka Huu
![]()
Rais John Magufuli amesema atahamia jijini Dododma kabla mwaka huu haujamalizika kama alivyoahidi serikali yake kuhamia huko.
Rais Magufuli amesema hayo wakati akizungumza katika hafla fupi ya kuwakabidhi hati za viwanja kwa mabalozi wa nchi mbalimbali na wawakilishi wa mashirika ya kimataifa, Ikulu jijini Dar es Salaam leo Jumatatu Julai 30.
Amesema hadi sasa viongozi wengi wa serikali wameshahamia Dodoma akiwamo Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan, mawaziri na viongozi mbalimbali wa kitaifa na kwamba Dar es Salaam amebaki yeye tu.
“Nimebaki mimi tu hapa. Nimepanga kabla mwaka huu haujamalizika nitahamia Dodoma, nilitaka nisihamie huko nikawaacha ndugu zangu wanaowakilisha nchi zao hapa Dar es Salaam, ndiyo mana nikahakikisha mnapata hati.
“Serikali imetoa maeneo mbalimbali jumla ya heka tano bure kwa ajili ya mabalozi, na ninyi ni mashahidi nimetoa hati hizi bila kudai chochote na mmepatiwa bila kusaini chochote, sijasema mhamie kesho, mtahamia wakati wowote mtakaotaka,” amesema Rais Magufuli.
Pamoja na mambo mengine, Rais Magufuli amesema, tayari viongozi wote na watumishi zaidi ya 6,000 wameshahamia hukoa ambapo pia amewatoa hofu mabalozi hao na wawakilishi wa kimataifa kuhusu usalama jijini humo.
“Tunaamini katika hatua tunazochukua mkihamia Dodoma itakuwa safi na kuhusu usalama tumehakikishiwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa.
“Dodoma ni mahali pazuri na ni rahisi kwenda nchi yoyote kwa kuanzia Dodoma. Tunaboresha huduma za usafiri ikiwamo miundombinu na afya kwa Dodoma na mikoa jirani ukiwamo Singida.
“Nimeagiza ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa msalato ili ndege zinazotua Dar es Salaam zitue Dodoma uanze kujengwa mara moja. Nataka niwahakikishie mabalozi Dodoma ni mahali pazuri nina uhakika patakuwa safi sana hasa baada ya ndege kutoka nchi zenu kutua hapa, tunataka kuitengeneza Tanzania mpya, yenye maendeleo na kushirikiana na sekta binafsi,” amesema.
Matendo hukidhi haja marizawa kuliko manenoBado siku mbili mwaka uishe
Umeelewa nilichokimaanisha au umejibu kwa kutumia mihemuko?Kwani bahari ndio kigezo cha kuwa mji mkuu? mbona hatutaki kuelewa. nchi ngapi duniani mpaka nchi kubwa miji mikuu haiko katika fukwe za bahari na miji imeendelea sana tu. lazima tutofautishe mji wa kibiashara na na mji wa kisiasa. Dar utabaki biashara na sio lazima mji mkuu. Europe ndio kabisa miji mingi mikuu sio baharini hata baadhi ya Africa. ingekuwa hivyo basi Newyork ungekuwa mji mkuu au LA maana ndio kwenye biashara na watu wengi.
Hapana hajatumia mihemuko. Alikuwa anajaribu kuelezea anavyovijua na sio kinachoongelewa. Hivi kweli kakuona wewe hata hujui kuwa kuna nchi zingine ni land locked na hivyo bahari is out of suala? Hapana anajua ila alitaka kutufahamisha anachokijuaUmeelewa nilichokimaanisha au umejibu kwa kutumia mihemuko?
Itakua hivyo mkuu maana, si rahisi mtu aweze kuhamisha bahari...Hapana hajatumia mihemuko. Alikuwa anajaribu kuelezea anavyovijua na sio kinachoongelewa. Hivi kweli kakuona wewe hata hujui kuwa kuna nchi zingine ni land locked na hivyo bahari is out of suala? Hapana anajua ila alitaka kutufahamisha anachokijua
Alisema 2019Serikali ya CCM chini ya rais Pombe Magufuli ilitamba Sana na kupiga kelele kwamba kabla mwaka haujaisha rais atakua keshahamia makao makuu ya nchi mjini Dodoma kuungana na Makamu wake na waziri mkuu
Cha ajabu mwaka umebakiza dakika kadhaa uishe zile kelele na mbwembwe za rais kuhamia Dodoma kabla mwaka 2018 haujaisha sijui zimepotelea wapi
Wafia Chama na wajuvi wengine wa hii safari ya Dodoma mnijuze mmefikia wapi.
Haendi popote ng'o ni muongo kama waongo wengine,kwanza yeye ndie mpigadili wa kwanza.Serikali ya CCM chini ya rais Pombe Magufuli ilitamba Sana na kupiga kelele kwamba kabla mwaka haujaisha rais atakua keshahamia makao makuu ya nchi mjini Dodoma kuungana na Makamu wake na waziri mkuu
Cha ajabu mwaka umebakiza dakika kadhaa uishe zile kelele na mbwembwe za rais kuhamia Dodoma kabla mwaka 2018 haujaisha sijui zimepotelea wapi
Wafia Chama na wajuvi wengine wa hii safari ya Dodoma mnijuze mmefikia wapi.