Unataka maji, umeme, barabara au unataka mchungaji/sheikh? Hao viongozi wameteuliwa kuongoza ibada? Na kwanini tunaingelea dini mbili tu (wakristu na waislam) na kuacha Watanzania wa dini nyingine mfano, bohora, dini za asili n.k.?
Na mwisho, Wahindi hawalalamiki kabisa licha ya baraza zima la mawaziri kutokuwa na mhindi hata mmoja. Na hata kutumbuliwa wahindi wanatafuta namna ya kupambana na maisha. Hivi sisi Watanzania weusi tuna kasoro gani? Tumelelewa vibaya? Kwanini umaskini, udini tunaulilia sisi wakati wahindi waliozaliwa hapa hapa wanapiga hatua licha ya kuwa wachache kwenye nafasi ya uongozi?