Rais Magufuli: Mimi ni mzilankende muyango

Rais Magufuli: Mimi ni mzilankende muyango

Unauliza kabila lake unataka kutambika mkuu
 
Umejichanganya. Ukoo hauwezi kuwa kabila. Kwa hiyo Muyango ni ukoo na Msubi ni kabila. Katika wasubi kuna koo zinazopatikana kote mkoa wa Kagera na Uganda kwa Wanyankole. Mfano Basita, Bayango, Basindi, Bagara, Bahutu, etc. Kumbuka Msubi akiongea Mhaya na Mnyambo watamwelewa. Hii ni pamoja na Wazinza na hata Bakerewe unaelewa lugha yao. Kama labda babu yake alikuja na kufia pale si ajabu labda alikuja kama mpagazi. Kumbuka hawa Wasubi na Wazinza ni jamii ya Watsu au Bahima na si ajabu hata Wahutu kwa hiyo kama alikuja kama mpagazi wa kihutu basi ndo watoto wake wakatawanyikia Biharamulo
Unajua hii taarifa ni classified?
 
Bila kwenda ndani sana ambako mengine si muhimu. Magufuli ni MCHANGANYIKO wa damu kadhaa MIXED BLOOD.
Ana damu ya KISUKUMA na ana damu ya makabila mengine baadhi ya hayo hapo juu.
Wasukuma huwa HAWANA HASIRA kali Magufuli ni MKALI SANA na mwepesi wa KUKASIRIKA!
Hiyo SI hulka ya WASUKUMA!Wasukuma ni WAPOLE!

ACCENT/ LAFUDHI ya Magufuli si PURE KISUKUMA ukimsikiliza kwa makini ana Lafudhi tofauti. kwa sababu ya DAMU mchanganyiko!

Japokuwa Magufuli anakizungumuza Kisukuma vizuri sana lakini si Msukuma kamili.
Japokuwa familia yake the MAGUFULIS huongea KISUKUMA wakiwa nyumbani bado yeye si PURE Msukuma.

Kama ILIVYO KAWAIDA ya Watanzania wengi, Tuko MIXED blood hakuna aliye PURE kabisa labda wa kule ndani sana.
Hata hivyo ukifuatilia BLOODLINE/UKOO utakuta watu wengi si PURE/ KAMILI katika kabila lake

hata Magufuli ni kama WEWE na MIMI. HUO ndo UZURI wa nchi ya Tanzania INTERMARRIAGE /KUOANA makabila tofauti zimevunja UKABILA.

Labda tu umebaki kwa makabila wachache sana WANAOJIBAGUA na KUOANA wao kwa wao!
INTERMARRIAGE kuona nje ya kabila lako kumeisadia Tanzania. Kwa hilo NAJIVUNIA nchi yangu Tanzania!
Mimi ndio usiseme. Hata kujitambulisha napata shida sana. Msambaa nipo, Mzaramo nipo, Mdigo nipo, Msukuma nipo.
 
Heshima kwenu wakuu,

Juzi rais alipotutembelea huku kwetu Kagera, rais Magufuli alijinasibu kwamba yeye ni Muyango yaani "abayango" hujiita Wazilankende. Akadai babu yake alizikwa pale Bukoba mjini Sehemu inaitwa Uswahilini pale karibu na Sanamu la Mayunga. Jina la babu yake limenitoka nikikumbuka ntaedit niweke hapa ila ni kama alisema aliitwa Mzee Mshalila(?).

Huyu mzee Mashalila alizaa watoto watatu, bahati mbaya hawa watoto wapo hadi leo sema akili zao hazipo sawa. Wapo Uswahili pale Bukoba Mjini.

Kwa wasiofahamu sifa ya Wazilankende ngoja nifafanue kidogo. Nkende ni ngedere, sasa hawa wazilankende ni marafiki wa ngedere. Yaani hata akimuona ngedere barabarani inatakiwa awabebe ndizi. Akikuta ngedere amekufa inabidi alie au anaumwa inabidi amtibie. Hao ndo wazilankende.

Hata ukiangalia kwenye hotuba ya Mbunge wa bukoba mjini Mh. Lwakatare wakati anamkaribisha alisema karibu nyumbani Mzilankende "wayanga waija" hatimaye umekuja(kwa tafsiri isiyo sahihi.).

Ndugu zake rais Magufuli waliopo Bukoba ni Oscar Mashalila, Dotto Mashalila watatu nmesahau jina la mtoto wa tatu, sema ni maarufu tu mjini japo hapo sawa.

Huo ulikuwa ni utangulizi. Swali langu ni;

Rais Magufuli ni nani?
1. Mzilankende
2. Msubi,
3. Msukuma
Au Muyango?

Kusema kweli mtakuwa mumenaidia sana.

Awe nani sisi tunajua moja tu. Ni raisi wa Tanzania hadi 2025.
 
Aiseee wahaya kama mnamtaka mchukueni tu sie wasukuma hatuna watu wa aina yake wenye kuchomokwa na maneno... wasio wapole wanyenyekevu wenye jazba mi nadhan kwel ni mzilankende mchukueni tu alishatuchosha sie inawezekana aliitwa msukuma ili apat kura za wasukuma... lakin kama mnamchukua ilu muonekane mmetoa raisi na nyie kabilA lenu utakula kwenu kwani atawanyea tu pyaaa hana breki mjomba
 
Huyu hana kabila, wakatinakiwa nkome Geita alisema babu zake wamezikwa hapo na makabuli alituonesha., wakati akiwa Misungwi alisema babu yake alizikwa hapo, Leo yupo Bukoba anasema babu yake amezikwa hapo, nadhani huyu hana kabila.
 
Sijui mtoa mada unataka kufikisha umjumbe gani maana sioni kipi unataka kutwambia.
 
Mimi MUHUNGA mzilachiherere (chiherere ni pimbi) luganda rwechikele ( chikere ni chura). Mtabani wa bayambo owakaragwe..!
 
Bila kwenda ndani sana ambako mengine si muhimu. Magufuli ni MCHANGANYIKO wa damu kadhaa MIXED BLOOD.
Ana damu ya KISUKUMA na ana damu ya makabila mengine baadhi ya hayo hapo juu.
Wasukuma huwa HAWANA HASIRA kali Magufuli ni MKALI SANA na mwepesi wa KUKASIRIKA!
Hiyo SI hulka ya WASUKUMA!Wasukuma ni WAPOLE!

ACCENT/ LAFUDHI ya Magufuli si PURE KISUKUMA ukimsikiliza kwa makini ana Lafudhi tofauti. kwa sababu ya DAMU mchanganyiko!

Japokuwa Magufuli anakizungumuza Kisukuma vizuri sana lakini si Msukuma kamili.
Japokuwa familia yake the MAGUFULIS huongea KISUKUMA wakiwa nyumbani bado yeye si PURE Msukuma.

Kama ILIVYO KAWAIDA ya Watanzania wengi, Tuko MIXED blood hakuna aliye PURE kabisa labda wa kule ndani sana.
Hata hivyo ukifuatilia BLOODLINE/UKOO utakuta watu wengi si PURE/ KAMILI katika kabila lake

hata Magufuli ni kama WEWE na MIMI. HUO ndo UZURI wa nchi ya Tanzania INTERMARRIAGE /KUOANA makabila tofauti zimevunja UKABILA.

Labda tu umebaki kwa makabila wachache sana WANAOJIBAGUA na KUOANA wao kwa wao!
INTERMARRIAGE kuona nje ya kabila lako kumeisadia Tanzania. Kwa hilo NAJIVUNIA nchi yangu Tanzania!
Intermarriage hipi hiyo inayomfanya mtu apoteze kabila lake...maana katika tamaduni za Afrika sehem kubwa watoto wanaridhi koo za upande wa baba...Labda nchi nyingi zinaongozwa na watu wasio wazawa
 
Minachojua na hata ukifatilia wahaya ambao nikoo la bayango kiujumla niwatu wenye akili sana kulko koo nyingine ndan ya Kagera na ni malanyingi sana mh kujiita mzirankende so yawezekana kweli akawa anatoka ukoo huo wa bayango ,hii ya kua msukuma yy ndoanajua nature yake coz awez kua anajiita mzirankende bila sababu bt all in all watanzania ni wamoja.
 
Intermarriage hipi hiyo inayomfanya mtu apoteze kabila lake...maana katika tamaduni za Afrika sehem kubwa watoto wanaridhi koo za upande wa baba...Labda nchi nyingi zinaongozwa na watu wasio wazawa
Nafikiri hata Magufuli ni afadhali at least anazungumuza moja ya lugha.
SWALI
Ni watanzania wangapi wanaoweza kuongea lugha zao kifasaha pasipo KUCHANGANYA na KISWAHILI?
 
Back
Top Bottom