Wakuu habari za muda.
Leo nikiwa hoteli moja maarufu hapa mjini (jina nalihifadhi) kupata chakula cha mchana, nimekuta watu watano ambao walikuwa na maongezi makubwa kidogo.
Watu hawa ambao kwa muonekano ni kama maofisa wa idara ya serikali ambao inaonekana wanafanya katika wazara tofauti nao wakipata chakula cha mchana.
Hoja ambayo ilikuwa mezani ni nani ambaye anaweza kumdhibiti mwezake kati ya Rais Dr Magufuli au Mwenyekiti wa chama Dr Kikwete.
Katika maongezi yao wawili walikuwa wanamuunga mkono kikwete na watatu wanamuunga mkono Magufuli.
Wanaomuunga kikwete walisema, Kikwete ndiye mwenye chama, anaisimamia serikali yake ambayo ni mtoto kwenye chama, hivyo kama mwenyekiti lazima ahakikishe aliyepewa dhamana ya chama kuongoza serikali anafuata ilani na taratibu za chama.
Wakadai kuwa Mwenyekiti ananguvu ya ushawishi ndani ya chama na kama rais atakwenda kinyume na chama kinavyotaka, mwenyekiti anaweza pitisha azimio la kumwondolea uanachama rais na hivyo kuvuliwa urais, hii ni kutokana na katiba ya chama.
Kwa upande wa waliokuwa wanamtetea rais nao walijuwa na hoja zao nzito.
Walidai kuwa Rais ni mkubwa zaidi ya mwenyekiti wa chama, kwani yeye anaongoza hata wasiokuwa wanachama.
Kulingana na katiba ya nchi rais anaweza hata kumweka kizuizini mtu yeyota hata mwenyekiti wake.
Hivyo Mwenyekiti wa chama hafui dafu kwa Rais.
Kutokana na mjadala ulivyokuwa mkali imebidi niulete humu tuone hoja zikipanguliwa.