Rais Magufuli azindua rada ya kuongozea ndege

Rais Magufuli azindua rada ya kuongozea ndege

Wakija itakuwa vizuri labda mikurupuko itapungua
Anamsifia Johari na Kamwele kwa kuwahujumu fastjet ,Fastjet msingewahujumu zile ATR zao kwa ajli ya kigoma,Tabora na bukoba mngefunga shirika lenu,unavyomsifia unataka aendelee kuhujumu mashirika mengine ili waendelee kusavaivu Mkuu.

Dream liner imekuja hapa imeanza route bila kufanya Demo flight,hata Airbus wakati Fastjet kila ndege ikija hapa lazima wafanye Demo flight na usumbufu mkubwa lakini shirika la magufuri wanafumba macho.TCAA wajiangalie,ICAO watakuja kufanya yao.
 
Naona spika ndugai anaendeleza siasa hata pasipostahili...
Kamtambulisha kwa rais mbunge wa singida mashariki na kusema kuwa eti wananchi wa "wilaya ya ikungi sasa wana mwakilishi baada ya muda mrefu kupita bila kuwa na mbunge...."
Sasa ni uongo?
 
WANAFIKI WAKUBWA!

Wakati mnaiona kashfa ya fisadi Mkapa kununua Rada lakini wakati huo huo hamzioni kashfa mbali mbali za huyo kubwa la majizi ikiwemo KUKWAPUA 1.5 trillions kutoka hazina.

Fuatilia kupitia TBC1 na Ikulu Online Tv. Mgeni Rasmi ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli. Rada hiyo ni kwa ajili ya kuongozea Ndege katika viwanja vya Ndege vya Dar es Salaam, Mwanza, kilimanjaro na Songwe



=> Mh. Rais kutoka bungeni tumekuja na wabunge kutoka mkoa wa Dar es Salaam na kwengineko wa kamati ya ujenzi, miongoni mwa wabunge hao kuna mwana kamati mpya ambaye ni mbunge Mtaturu - Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai

=> Mh. Rais miaka kumi iliyopita ilinunuliwa Rada ambayo iliambatana na kashfa katika ununuzi wake kupitia kampuni moja kubwa sana ya mitambo ya uangalizi wa anga - Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai


=> Mh. Rais mimi na timu yangu tulienda Uingereza kupambania kurejeshwa kwa fedha zetu paundi milioni 75 na tukafanikiwa, naomba nikupongeze wewe kwani kipindi chako imenunuliwa rada bila rushwa yoyote - Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai

=> Mh. Rais kipekee kabisa napenda kukupongeza kwa kukubali kuhudhuria uzinduzi huu - Waziri wa uchukuzi, Isack Kamwelwe

=> Mh. Rais ili kuhakikisha kuwa mifumo ya rada zote zinafanya kazi kwa ufanisi tumeingia mkataba utaowezesha vipuri kupatikana kwa uhakika katika kipindi cha miaka 15 - Waziri wa uchukuzi, Isack Kamwelwe

=> Nyote huwa mnajua mimi huwa sipendi kabisa miradi inayoishia njiani, na ndio maana leo nimefurahi sana - Rais wa Jamhuri ya Tanzania, John Pombe Magufuli

=> Naomba nimpongeze kwa dhati mkurugenzi mkuu wa TCAA Johari, sina zawadi ya kumpa ila mwaka huu akitaka kwenda hija nitamlipia gharama - Rais wa Jamhuri ya Tanzania, John Pombe Magufuli

=> Kwakweli Johari wewe ni johari kweli kwenye kazi, yaani kwenye ufanisi wa kazi yupo makini sana, ningekuwa na binti ningempa - Rais wa Jamhuri ya Tanzania, John Pombe Magufuli

=> Aliyetuuzia rada kule Uingereza alijiuzuru, lakini wa kwetu hapa sijui kama kuna mtu alijiuzuru labda siku zijazo waamue kufanya hivyo - Rais wa Jamhuri ya Tanzania, John Pombe Magufuli

=> Shirika letu la ndege linafanya vizuri sana mkiona ndege zetu zinakamatwa msishangae - Rais wa Jamhuri ya Tanzania, John Pombe Magufuli

=> Ushahidi wa kwamba shirika letu linafanya vizuri, siku za nyuma tulikuwa tunamiliki asilimia 3 tu lakini hivi sasa tunamiliki asilimia 70 ya safari zote za Anga - Rais wa Jamhuri ya Tanzania, John Pombe Magufuli
 
Back
Top Bottom