Manyerere Jackton
JF-Expert Member
- Dec 11, 2012
- 2,436
- 4,429
Kuna habari kuwa DCI ametenguliwa uteuzi wake.
Rais John Magufuli ametengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (Director of Criminal Investigation – DCI), Diwani Athuman Msuya.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi, Rais Magufuli ametengua uteuzi huo leo.
Bila kutoa ufafanuzi wa sababu za mkuu huyo wa nchi kuchukua hatua hiyo, taarifa ya Ikulu imeeleza kuwa Athuman atapangiwa kazi nyingine.
“Kufuatia uamuzi huo, uteuzi wa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai utatangazwa baadaye,” imeeleza sehemu ya taarifa kutoka Ikulu.
Rais John Magufuli ametengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (Director of Criminal Investigation – DCI), Diwani Athuman Msuya.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi, Rais Magufuli ametengua uteuzi huo leo.
Bila kutoa ufafanuzi wa sababu za mkuu huyo wa nchi kuchukua hatua hiyo, taarifa ya Ikulu imeeleza kuwa Athuman atapangiwa kazi nyingine.
“Kufuatia uamuzi huo, uteuzi wa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai utatangazwa baadaye,” imeeleza sehemu ya taarifa kutoka Ikulu.