Rais Magufuli anasema hivi kuhusu misaada

Rais Magufuli anasema hivi kuhusu misaada

"Wale wanaojitokeza kutupa misaada, nataka niwahakikishie ile misaada ni ya masharti. Unaweza ukapewa masharti kwamba usikohoe na kikohozi kinakujaga tu. Kwa hiyo ni lazima watanzania tujisimamie sisi wenyewe. Na tukisimama sisi wenyewe, Tanzania hii tutavuka. Tanzania hii tuna kila kitu, Tanzania ni matajiri lakini utajiri tumeukalia"
Tunamshukuru mungu kumleta Magufuli katika muda muafaka kabisa, angewaleta wazunguusha mikono nchi ingeshauzwa ulaya na marekani. ASANTE MUNGU
 
"Wale wanaojitokeza kutupa misaada, nataka niwahakikishie ile misaada ni ya masharti. Unaweza ukapewa masharti kwamba usikohoe na kikohozi kinakujaga tu. Kwa hiyo ni lazima watanzania tujisimamie sisi wenyewe. Na tukisimama sisi wenyewe, Tanzania hii tutavuka. Tanzania hii tuna kila kitu, Tanzania ni matajiri lakini utajiri tumeukalia"
Hugo ndio upuuzi wa wanasiasa, anatamka halo huku akizungukwa na watu maskini wa kutupwa ikiwa ni pamoja na ndugu zake wanalalia mlo mmoja ndani ya nyumba za nyasi. Siwapendi wanasiasa. Waongo wote
 
Kansigo nimekuelewa upande wako, lakini ujue hao waliokuwa wanatupa misaada walikuwa wanachangia pale palipokuwa na deficity inayoletwa na watendaji wa serikali kwa kuiba,miradi hewa,michakato isiyokamilika,rushwa kubwakubwa n.k. hizo deficity zikidhibitiwa hela itakayopatikana itatutosha tu.

mbona awamu iliyopita tulikuwa vinara wa kuomba na kukopa lakini miradi mingi ilikuwa haiendi mpaka wakandarasi walilipotiwa kujiua?

kama haya mapungufu yakidhibitiwa tutafika tu na asiyetupenda kwa tabia yetu ya kuombaomba na kulialia ugumu wa maisha atatupenda tu.

naamini hata wewe kwa uhakika huna mapenzi na mtu mwenye shida kila siku, akitokea tu au kukupigia simu unajua mizinga tayari aidha unajiandaa ujibu vipi au hupokei simu. nadhani tukitaka tuwe na marafiki basi tusiwe na tabia za njaanjaa

naomba kukosolewa
Nimeupenda mtazamo wako!

Keep it up bowlibo.
 
Suala la kujitegemea kwa nchi zetu zinazoitwa nchi zinazoendelea ni safari ndefu na ngumu ni kweli nchi hizi zina rasilimali nyingi ikiwemo ardhi nzuri ya kilimo,madini,maliasili nk.lakini shida ni kuwa tunachozalisha bei inapangwa na hao wakubwa,teknolojia yetu pia bado ni duni kiasi kwamba nyenzo za uzalishaji lazima tununue kwa hao wakubwa kwa bei wanazopanga wao.Sijui zile nadharia za miaka ya 80 za kuwa na ushirikiano wa nchi zinazoendelea iliishia wapi?
 
Jamani tumuhurumie raisi wetu, hapo alipo ana mawazo, MCC wamekata mirija, Nchi 10 kati ya 14 zinazochangia budget wamesepa,Bandarini kumezorota, Wafanyabiashara hawaagizi kama kawaida, mapato ya ndani yanaendelea kupungua, kila kinachokusanya kinatumika, Mataifa rafiki hayamuelewi! walimu 50,000 wanatakiwa kuajiriwa, bado pesa za elimu bure ni janga jengine, hata za Mock hamna! nadhani anafikiria kuirudisha kodi ya kichwa sasa
Hewa watu wanavuta bure tu, kwanini msitoze kodi huko?
Kuna mapato mengine sana hapo yanapotea hivi hivi.
Msipende kuukalia hivyo huu Utajiri mlio nao
 
Kwa hali ya Tanzania ilivyo kwa sasa hasa baada ya uchumi kuanza kuyumba, MCC kukata mirija, Nchi 10 kati ya 14 zinazochangia budget kusepa,Bandarini kuzorota, Wafanyabiashara kutoagizi kama kawaida ili tukusanye kodi, mapato ya ndani TRA kuendelea kupungua, kila kinachokusanya kinatumika, kulipia elimu bure kuzidi kuwa kugumu.

Budget deficit itakuwa kubwa mno,

Nadhani tufikirie kuirudisha kodi ya kichwa sasa ile ya miaka ileeee.
 
Wewe si mtz msaidie rais wako mawazo tutajikwamua vp au hayakuhusu
Mkuu usimkane raia mwenzio kwa hoja yake au mtazamo wake bhana!!

Sasa nikujuuze hapa Ulimwenguni kila nchi uionayo/uisikiayo ina Rasilimali za kutosha (lakini bado masikini kwa kuwa hawana ufunguo wa kufungua !!) kama vile anavyosema Rais wetu JPM kuwa TZ ni tajiri... Sasa Utajiri wenyewe haulipi wala haukui, haunyanyuki... bila kupata lift-up, ufunguo nchi zenye uwezo wa kutunyanyua.. Kwa kifupi kuna gharama na sacrifices lazima zituhusu!!!
GOOGLE Kodi zenyewe zilizokusanywa ni mkupuo wa mara moja/mbili ila kwa longa term itadorora na kudrop!!! (mzunguko wa biashara umepwaya)
 
mpaka leo rais mzma anaongea kana kwamba bado yuko kwenye kampen...bado anaahidi!!!!..ameshaona udhaifu wa watz ulipo...raisi mziam anatafuta media coverage...huu ni mda wa kutekeleza yale aliyoahidi si kuendelea kuahidi....mda si mrefu jk ataonekana alikuwa bonge la rais
 
Kufatia kwa wahisani kuendelea kujitoa kuifadhili bajeti ya selikali ya Tanzania... Selikali itabidi ielekeze nguvu kubwa ya kukusanya kodi na mapato kutoka katika vyanzo vya ndani ya nchi!!? Hivyo basi ni ukweli usiopingika bei ya bidhaa za ndani ya nchi itapanda baada ya ongezeko la kodi!!!!

Maoni yangu watanzania mjipange sana hasa kwa kutumia bidhaa ambazo zitakuwa hajapitia sokoni!!!!!
f10d9dda36e82f3488659da7c97ad615.jpg
 
Mm sipingani na wazo la magufuli. Ila kusema kweli kwa kipindi hiki alihitaji hii misaada ili aweze kujenga nafasi ya kujitegemea. Kuikataa hii misaada ni sawa na mtoto kukataa msaada wa ada eti kisa kwao Kuna vyanzo vya mali ambavyo hata kuvitumia hawezi. Ifike mahali tukae na kujadili kama watu tunakjielewa. Kumbukeni pamoja na nguvu za misaada ya zamani, lakini bado watoto wanakaa chini mashuleni. Je tutaweza kujisimamia kama inavyoelezwa?
Hana jeuri yakuikataa sema wenye nayo wamekataa UHUNI
 
Kwahali ya Tanzania ilivyo kwa sasa hasa baada ya uchumi kuanza kuyumba, MCC kukata mirija, Nchi 10 kati ya 14 zinazochangia budget kusepa,Bandarini kuzorota, Wafanyabiashara kutoagizi kama kawaida ili tukusanye kodi, mapato ya ndani TRA kuendelea kupungua, kila kinachokusanya kinatumika, kulipia elimu bure kuzidi kuwa kugumu.
Budget deficit itakuwa kubwa mno,

Nadhani tufikirie kuirudisha kodi ya kichwa sasa ile ya miaka ileeee.
Very soon mizuka itakata!!! Zile pambio za sifa zitageuka shubiri!! Watu watatafutana na kukimbiana!!! Uchumi ni hesabu sio kelele!!! Uchumi ni namba sio mbwembwe!!! Nchi ambayo 90% ya makusanyo inakwenda kwenye mishahara na madeni kwa hali hii ni kiza kikubwa mbele ya safari!!!

Safari ndo kwanza mbichi ngoja tuone!!!
 
Hahahah kodi yenyewe wanategemea kariakoo, mwaka huu tutakoma haki ya nani
 
Back
Top Bottom