Rais Magufuli anasema hivi kuhusu misaada

Rais Magufuli anasema hivi kuhusu misaada

Halafu mtu anakuja anasema na bado, wengine wazuie misaada yao kwa TZ hivi ana akili huyu? Kumbe mafanikio ya nchi ni ya Magufuli tu? Hovyo kabisa....sikuamini kumuangalia akiongea....

..kinachopaswa kufanyika ni kurekebisha mapungufu yaliyosababisha tufungiwe misaada.

..katika hili tunatakiwa tuwalaumu Raisi Magufuli, Dr.Shein, na Mzee Jecha. kiburi chao ndiyo kimetuingiza ktk matatizo haya.

..ningekuwa mimi ndiyo Raisi ningeifuta sheria ya mitandao, na kwa ZNZ ningewaita UN na EU wasimamie uchaguzi mpya kwa gharama zao.
 
"Wale wanaojitokeza kutupa misaada, nataka niwahakikishie ile misaada ni ya masharti. Unaweza ukapewa masharti kwamba usikohoe na kikohozi kinakujaga tu. Kwa hiyo ni lazima watanzania tujisimamie sisi wenyewe. Na tukisimama sisi wenyewe, Tanzania hii tutavuka. Tanzania hii tuna kila kitu, Tanzania ni matajiri lakini utajiri tumeukalia"
Mm sipingani na wazo la magufuli. Ila kusema kweli kwa kipindi hiki alihitaji hii misaada ili aweze kujenga nafasi ya kujitegemea. Kuikataa hii misaada ni sawa na mtoto kukataa msaada wa ada eti kisa kwao Kuna vyanzo vya mali ambavyo hata kuvitumia hawezi. Ifike mahali tukae na kujadili kama watu tunakjielewa. Kumbukeni pamoja na nguvu za misaada ya zamani, lakini bado watoto wanakaa chini mashuleni. Je tutaweza kujisimamia kama inavyoelezwa?
 
Tatizo nch haikujiandaa kujitegemea! Tutaisoma namba kweli!
 
Sas
Sawa Mheshiwa RAIS, lakini hilo suala ni la long term plan, sio la muda mfupi kiivyo, just take it slow this is process , we can win overnight, mheshimiwa
Sasa kelele za nini si mumuache ashindwe uongozi kwa kukosa hiyo misaada ili tupate kick ya kumuondoa 2020? mbona mnamuonea huruma anayetakiwa kushindwa?
 
Tatizo sio utajiri tatizo ni transformation ya hizo resources kuwa utajiri ,unasema una kila kitu ila India na Kenya ndio wanaongoza kwa uuzaji wa Tanzanite kwenye soko la dunia ,

Jk na Wachina wake sijui wana mikataba yao 16 waliongia na sio bunge wala nani anaijua

Unasema una kila kitu wakati nishati ya umeme tu watu wanamwaga maji makusudi Mtera ili tuingie kwenye mgao ,

Hivyo viwanda sijui mitaji yake itatokana na nini kama nishati tu ni tatizo

Wawekezaji wa ndani walipotaka kuwekeza mkasema wawekeze kwenye juice na mandazi sijui ,sasa sijui unategemea huyo mwekezaji wa nje atafanyaje shuguli zake hapa uchumi ukiyumba,

Tuna wapiga siasa kuliko ma technicians,
Tunasafari ndefu kwa kweli
 
Ni wakati wako sasa kufufua fikira ulizoua za kujitegemea. Fikiria namna ya kuifanya Tanzania nchi inayojitegemea kiasi cha kufikia kutoa misaada kwa nchi nyingine. Kama unaona uwezi kukaa katika Tanzania inayojitegemea anza sasa utaratibu wa kuukana uraia wa Tanzania na kutafuta uraia wa nchi nyingine itakayokidhi matakwa yako. Kwa nini unataka kila kitu ufanyiwe, yaani hata kufikiri unahitaji msaada...!!? Mnaaza kunifanya niandike kwa ukali kwenye jukwaa hili. TUJITEGEMEE muda ndiyo huu.

...
 
Sasa wewe ankoben hayo unayoyasema si ndio tuyapige vita wote yaondoke, naona unajitenga kwani wewe sio mtanzania
 
kuna mambo mengi ambayo magufuli hayajui...anakurupuka...hilo la zanzibar na hiyo heria ya mitandao ..hakuna anachojua...
 
Jamani tumuhurumie raisi wetu, hapo alipo ana mawazo, MCC wamekata mirija, Nchi 10 kati ya 14 zinazochangia budget wamesepa,Bandarini kumezorota, Wafanyabiashara hawaagizi kama kawaida, mapato ya ndani yanaendelea kupungua, kila kinachokusanya kinatumika, Mataifa rafiki hayamuelewi! walimu 50,000 wanatakiwa kuajiriwa, bado pesa za elimu bure ni janga jengine, hata za Mock hamna! nadhani anafikiria kuirudisha kodi ya kichwa sasa
Kansigo nimekuelewa upande wako, lakini ujue hao waliokuwa wanatupa misaada walikuwa wanachangia pale palipokuwa na deficity inayoletwa na watendaji wa serikali kwa kuiba,miradi hewa,michakato isiyokamilika,rushwa kubwakubwa n.k. hizo deficity zikidhibitiwa hela itakayopatikana itatutosha tu.

mbona awamu iliyopita tulikuwa vinara wa kuomba na kukopa lakini miradi mingi ilikuwa haiendi mpaka wakandarasi walilipotiwa kujiua?

kama haya mapungufu yakidhibitiwa tutafika tu na asiyetupenda kwa tabia yetu ya kuombaomba na kulialia ugumu wa maisha atatupenda tu.

naamini hata wewe kwa uhakika huna mapenzi na mtu mwenye shida kila siku, akitokea tu au kukupigia simu unajua mizinga tayari aidha unajiandaa ujibu vipi au hupokei simu. nadhani tukitaka tuwe na marafiki basi tusiwe na tabia za njaanjaa

naomba kukosolewa
 
mbona tunaumia sana kunyimwa msaada??? can't we stand by our own hands??????
You can stand if you want to stand!

Binadamu tumepewa uwezo kifikra ili kupambana na mazingira hatarishi.

Better to try and fail than never to try at all!

Hii mentality ya kudhani hatuwezi imepandikizwa kielimu katika fikra zetu ili tuwe na inferiority complex.

Nchi zilizoendelea hazikuwa na maliasili, sisi tuna maliasili lakini bado tunadhani hatuwezi.
 
kila siku anasema nchi hii ni tajiri lakini hapo alipo hajatoa dira ya kule anakotaka tufike..yeye na yule dc wa iringa hawana tofauti...
 
mbona tunaumia sana kunyimwa msaada??? can't we stand by our own hands??????
Bandugu wewe huna miguu? Au ni mcheza sarakasi?
Huku mtaani tunaona wanasarakasi tu ndio wanasimama kwa mikono.
mbd105582_0410_handstand2a_hd.jpg
 
Tatizo la watanzania wengi tunawaza kitumwatumwa, watu wanadai tutaishije bila msaada, huo ni utumwa

Kama ulisoma chuo ulipewa msaada wa mkopo. Jitambue basi? Au ni mmojawapo wa vilaza wanaodai eti tunaweza kujitegemea. Yaani hao wengine woote hawakuliona hili Magu mwenyewe ndiye anaweza. Upuuzi tu
 
Jamani tumuhurumie raisi wetu, hapo alipo ana mawazo, MCC wamekata mirija, Nchi 10 kati ya 14 zinazochangia budget wamesepa,Bandarini kumezorota, Wafanyabiashara hawaagizi kama kawaida, mapato ya ndani yanaendelea kupungua, kila kinachokusanya kinatumika, Mataifa rafiki hayamuelewi! walimu 50,000 wanatakiwa kuajiriwa, bado pesa za elimu bure ni janga jengine, hata za Mock hamna! nadhani anafikiria kuirudisha kodi ya kichwa sasa
Na hiyo ingekuwa poa sqana. Maana Tanzania hii ni yetu sote pamoja na wewe unayefurahia mcc kutotoa msaada wao.
Kwa hiyo kodi nyingi inalipwa na wafanya kazi wa serikali na wakulima pale wanouza mazao. Sasa tungerudi kwenye kodi ya kichwa mapato yangepanda...
 
Watanzania kwani utajiri (rasiliamli) hizi sizilikuwepo miaka yote (awamu zote) ?? Lakini tulikuwa tunapokea misaada na kubebwabebwa kama kawaida......n Leo hii 50 million waTz..
tusubiri hayo mawe,gesi,samaki na udongo yawe ready for market... mmmh na bei kila siku inashuka !!!!? Hii mie naona genocideiiii ya kisiasa (mtazamo tu)
 
"Wale wanaojitokeza kutupa misaada, nataka niwahakikishie ile misaada ni ya masharti. Unaweza ukapewa masharti kwamba usikohoe na kikohozi kinakujaga tu. Kwa hiyo ni lazima watanzania tujisimamie sisi wenyewe. Na tukisimama sisi wenyewe, Tanzania hii tutavuka. Tanzania hii tuna kila kitu, Tanzania ni matajiri lakini utajiri tumeukalia"
Kuwa na kila kitu ni jambo moja na transformation ni kitu kingine tofauti kabisa.
Mfano dhahabu za Geita unaweza kuzichimba na jembe la mkono? (Bahati mbaya hata kiwanda cha kuengeneza majenbe kilishakufa).
Tufanye umeingia gharama na kuzichimba hizo dhahabu, utamuuzia nani kama sio wao!? (Ningeria walifanya budget bei ya pipa la mafuta ikiwa $110 sasa imeshuka mpaka $28 na wao ndio wachimbaji na wanunuzi, ahadi zote za rais Buhari ziko mashakani)
Hivi kuna mswahili hapa (hata ukikusanya maprofesa wote) anaweza kubuni mfumo wake wa elimu bila kuongea Harvard na Oxford!?
Kuna mtu anaweza kubuni ligi yake ya mpira hapa bila kumpeleka Mbwana Samatta ubeligiji na kusikiliza viwango vya Fifa!?
Tuache kudanganyana bwana!
 
Sasa ndugu yangu unafikiri hiyo misaada tuliyokuwa tukipewa ilikuwa inafika kwenye miradi husika, kama sio ilikuwa inaishia kwenye matumbo ya watu
 
Back
Top Bottom