Rais Magufuli ameshinda vita dhidi ya Corona

Kalamu Nzito

JF-Expert Member
Aug 13, 2015
318
662
Rais Magufuli ameshinda vita dhidi ya Corona. Ndio, ameishinda kisiasa. Lakini tufahamu kua Vita dhidi ya Corona sio Vita ya kisiasa. Ninasikitika sana matabibu hawajapewa nafasi kuzungumza hali halisi ya suala hili.

SIASA IMEVAA KOTI LA KITABIBU. Nafahamu wazi kuwa jukumu la kutangaza hali halisi ilikua juu ya wizara ya afya, waziri mkuu na msemaji mkuu wa serikali.

Lakini ukitazama hawa wote wako chini ya mwamvuli wa siasa. Nasikitika tena sana kuona matabibu hawajapewa nafasi kabisa kutueleza ukweli.

Nafahamu wafanyakazi wa Serikali hula kiapo kulinda siri za serikali, lakini sifahamu kama takwimu halisi za maambukizi ya gonjwa la corona ni siri za serikali au la?!

Kusimamishwa kazi kwa wanamaabara katika maabara kuu kupisha uchunguzi ni ushindi kwa mwanasiasa. Ataonekana anachapa kazi hasa pale atakapokimbilia vyombo vya habari kulieleza hili katika upande wake tu.

Lakini je, tumepewa nafasi kuwasikiliza wanamaabara wale wana nini cha kueleza? Tuendelee kuchukua tahadhari. Kisiasa Corona tumeishinda.

Kitaalamu bado tuna vita ya kupambana.

Mungu ibariki Tanzania!
 
Wazo la waziri wa katiba na sheria la kuficha data lime pokelewa

Dark Side
 
hv hao waliopona wanapimwa kwa kipimo kipi..?
Maana nakumbuka maabara zlifungwa kwa ajili ya uchunguzu
 
Watanzania wengi huishi kwa kula uongo na ujinga ndio maana hawawezi kutofautisha ukweli na uongo, werevu na ujinga.
 
Tufungue tu vyuo tukamalize kusoma, huku mtaani tunaishi kama vile hakuna CORONA yaani tokea tumefunga vyuo nimerudi home mwanza, daily nipo uwanjani nacheza mpira nimecheza ndondo (kulipwa ) mpaka huko Magu lakini sijawai kupata matatizo na hao marafiki zangu sijawai kusikia wana matatizo, ukipita mtaani watoto wanacheza kila siku mpira, vyuo vifunguliwe tu CORONA ninayoisikia tu ni ya mitandaoni ila huku tunaishi kama vile hakuna kinachoendelea.
 
Hivi mtu kama wewe utaepukaje kutawaliwa kimwili na kiroho,hivi ukitawalia utamlaumu mtawalaji wakati akili yako umeityuni kutawaliwa
 
Back
Top Bottom