Ndugu wewe ni twahil au jahil?Matokeo kubandikwa vituoni hakuondoi kuwa CUF walifanya udanganyifu na ushahidi upo...Pia hujui kuwa kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi Zanzibar mgombea urais kujitangaza kuwa kashinda ni uhaini??.
Msipende kutaka muhurumiwe na kupewa urais kiujanja ujanja kwa kuaminisha watu sababu za uongo...
Unajua maana ya uhaini?
Wambie wenye ushahidi wa udanganyifu wauweke wazi. Ni dhahiri wewe hunao,ungekuwa nao ungeuweka hapa ili wanaokusoma hapa wajiridhishe na ushahidi ulionao. Kama una ushahidi uweke,pokea changamoto hiyo,huna ushahidi unaropoka tu. Wingine wanaita kuropoka, domokaya.
Jiongezee maarifa hapa, huku ukijitayarisha kuleta ushahidi wa udanganyifu waliofanya CUF ulionao.
Tembelea Link Tetesi: - Vikwazo vyanukia kumshinikiza Magufuli aingilie kati ili mshindi atangazwe Zanzibar
Mimi sitaki nipewe uraisi au udiwani. Mimi si mwanasiasa. Ninachotaka mimi ni kuheshimiwa maamuzi ya wapiga kura na demokrasia ichukue mkondo wake.
Link Uchaguzi Zanzibar: Hongera Rais Magufuli kwa msimamo sahihi