Rais Magufuli akutana na Mzee Mkapa!

Rais Magufuli akutana na Mzee Mkapa!

kuna umuhimu gani kumfuata Mkapa nyumbani kwake, na kwa nini akutane na hawa wastaafu (Mkapa, JK, Waryoba, etc.) mara nyingi namna hii? watu wanaweza kutafsiri kwamba ni udhaifu na kutojiamini.
 
Yupi mshindi halali wakati matokeo hayakumalizwa kutangazwa?. Pia tukumbuke uchaguzi ulifutwa. So Seif alimwaga mboga, Jecha akamwaga ugali...turudi uwanji ndio suluhisho...
Hahaha. You made my day. Jecha akaona aaaa unanichezea basi nafuta hayo matokeo kama vipi kajiapishe sasa maana umeshajitangaza.
 
Huyu alisema raisi akipenda ampe kazi yeyote .ampe huo mgogoro wa zanzibar ausuluhishe
Huyo Mkapa mwenyewe alifanya nini kuhusu mgogoro wa Zanzibar wakati wa utawala wake?
 
kuna umuhimu gani kumfuata Mkapa nyumbani kwake, na kwa nini akutane na hawa wastaafu (Mkapa, JK, Waryoba, etc.) mara nyingi namna hii? watu wanaweza kutafsiri kwamba ni udhaifu na kutojiamini.
kaka mimi naona maoni yako ni uchizi fulani. Pamoja sote tunajua Magufuli sio kiongozi bali mtendaji na madhaifu yake kama mwanadamu ila sioni sababu zako zina msingi wowote wa kutojiamini.Nchi haiendeshwi unavyodhania .
 
kuna umuhimu gani kumfuata Mkapa nyumbani kwake, na kwa nini akutane na hawa wastaafu (Mkapa, JK, Waryoba, etc.) mara nyingi namna hii? watu wanaweza kutafsiri kwamba ni udhaifu na kutojiamini.
Ukiona hivyo suala la Zenj linachemka.

Kumbuka Marekani ambaye ni kiranja wa dunia walishalielekeza shirika lao la MCC kuzuia ule msaada wao wa dola za kimarekani milioni 472 kwa Tanzania hadi pale suala la uchaguzi wa Zanzibar litakapopatiwa ufumbuzi, kwa maana ya mshindi aliyepatikana tarehe 25/10/2015 atangazwe.

Sasa kwa kuwa CCM wanajiona kama ndiyo wamepewa hati miliki na Mwenyezi Mungu ya kuitawala nchi hii hadi mwisho wa dunia, wamelazimisha kufanya uchaguzi wao wa marejeo ambao ni batili kisheria.

Sasa kwa kuwa Magu maji yako shingoni kutokana na shinikizo la Jumuiya za kimataifa ambazo zilituma waangalizi wao kwenye uchaguzi uliopita na wakatoa taarifa zao kuwa uchaguzi huo ulikuwa huru na haki, kwa hiyo Magu ameenda kwa Mkapa ili wapeane ushauri namna ya kutafuta solution muafaka kutokana na suala la Zanzibar, ambalo kwa sasa limekuwa suala tete sana.
 
Ukiona hivyo suala la Zenj linachemka.

Kumbuka Marekani ambaye ni kiranja wa dunia walishalielekeza shirika lao la MCC kuzuia ule msaada wao wa dola za kimarekani milioni 472 kwa Tanzania hadi pale suala la uchaguzi wa Zanzibar litakapopatiwa ufumbuzi, kwa maana ya mshindi aliyepatikana tarehe 25/10/2015 atangazwe.

Sasa kwa kuwa CCM wanajiona kama ndiyo wamepewa hati miliki na Mwenyezi Mungu ya kuitawala nchi hii hadi mwisho wa dunia, wamelazimisha kufanya uchaguzi wao wa marejeo ambao ni batili kisheria.

Sasa kwa kuwa Magu maji yako shingoni kutokana na shinikizo la Jumuiya za kimataifa ambazo zilituma waangalizi wao kwenye uchaguzi uliopita na wakatoa taarifa zao kuwa uchaguzi huo ulikuwa huru na haki, kwa hiyo Magu ameenda kwa Mkapa ili wapeane ushauri namna ya kutafuta solution muafaka kutokana na suala la Zanzibar, ambalo kwa sasa limekuwa suala tete sana.
Magu akimsikiliza Lofa atamuingiza chaka.
Anafikiri kile kiburi chake bado kina-apply mpaka sasa
 
Naona kaenda kukutana na shujaa wa chama, maana bila yeye CCM tungekuwa tunaongozwa wa mafisadi fulani hivi. Tunashukuru Mkapa.
 
Ukichungulia kwa Nyuma unaona Bahati ya hindi kumbe Mzee kajenga kwny Fukwe!!!
Shati la Mzee Ben nadhan ni special order!
Kichwani Ben alikuwa vizuri sana kuliko alivyo leo Magu, ila kuishi Dar miaka mingi pamoja na kuoa kule kwa kina Fulani kulimfanya akawa mjanja fulani kitu ambacho hatukitegemei kwa Dr.Pombe aliehamia Dsm kwa mara ya kwanza 1995 alipoteuliwa kuwa Naibu waziri wa Ujenzi kwa vijiwe kama cha Palm beach vya mkapa au Vya saigon kwa kikwete hajawahi kukanyaga hivyo hatutegemei akina Machaprano kwenda kumsalimia Ikulu

Mkuu, umenikumbusha sana mzee Ben pale kijiweni Palm Beach ndio alikuwa akisuka timu yake na JPM alikuwa anahudhuria mezani, si unakumbuka kauli yake baada ya uchaguzi wa 1995 alisema amechagua baraza mawaziri akawaita askari wa miavuli?

Tena hata yule wa Hanang alijitahidi kujifichaficha pale Sea-View akiwa waziri mdogo lakini akavutwa na mzee Ben mezani Palm Beach na kuaminiwa Uwaziri mkuu na timu ikakamilika.

Nafikiri kwa sasa mission imekuwa accomplished ila hawa jamaa wawili hawana masihara kwenye masuala ya kazi.
 
Yupi mshindi halali wakati matokeo hayakumalizwa kutangazwa?. Pia tukumbuke uchaguzi ulifutwa. So Seif alimwaga mboga, Jecha akamwaga ugali...turudi uwanji ndio suluhisho...
Matokeo ya uchaguzi yalishatangazwa na kubandikwa vituoni,majimboni.
Kila chama ina nakala za hayo matokeo. CCM inajua iliangukia pua na hivyo iliamua kutengeneza "Mkwamo" kwa kutumia JWTZ, Polisi na Jecha.

Jecha amalizie kuyatangaza tu hakuna namna.
Jecha alishayatangaza majimbo 31...kisheria hawezi kufuta matokeo hayo. Ni mahakama tu ndio inaweza kutengua matokeo hayo na kuamuru re-run ya uchaguzi kama matokeo yatapingwa mahakamani.
Jecha aimeitia nchi aibu kubwa.CCM kushabikia uamuzi batili wa Jecha ni kufilisika kisiasa.
 
Raisi Magufuli alipokwenda nyumbani kwa Mzee Mkapa Masaki kumtembelea!

DSC_9103.JPG
2.jpg

Link Rais Magufuli Akutana Na Kufanya Mazungumnzo Na Rais Mstaafu, Benjamini Mkapa Na Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Warioba Ikulu Jijini Dar Es Salaam | MPEKUZI

Ni juzi tu Mkapa alienda IKULU kumpongeza Magu na kumtakia heri ya mwaka mpya na kumsihi asitumbue jipu la Kiwira na EPA.

Msimamo na masikitiko ya mabalozi wa US, Canada, EU kuhusu suala la Zanzibar linamuelemea Magu. Magu ameenda kwa Mkapa,( Ze Al Pacino) kuomba maelezo ya nini kifanyike.

Huyu mtu anasalimiwa kwa misingi ipi wakati yeye ni mwizi wa kutupwa? Huyu na mwenzake Mwinyi bila kumsahau pilot asiye na license (JK) yabidi wakamatwe na kufunguliwa mashitaka ya ufisadi. Very useless.

 
Huyu alisema raisi akipenda ampe kazi yeyote .ampe huo mgogoro wa zanzibar ausuluhishe
Kumpa Mkapa kutatua mgogoro wa Zanzibar ni sawa na kuweka mafuta kwenye moto.
Wanzanzibar bado wanamlaumu yaliyofanywa na polisi kipindi cha utawala wake na yeye aliwahi kukiri alifanya kosa.
 
Matokeo ya uchaguzi yalishatangazwa na kubandikwa vituoni,majimboni.
Kila chama ina nakala za hayo matokeo. CCM inajua iliangukia pua na hivyo iliamua kutengeneza "Mkwamo" kwa kutumia JWTZ, Polisi na Jecha.

Jecha amalizie kuyatangaza tu hakuna namna.
Jecha alishayatangaza majimbo 31...kisheria hawezi kufuta matokeo hayo. Ni mahakama tu ndio inaweza kutengua matokeo hayo na kuamuru re-run ya uchaguzi kama matokeo yatapingwa mahakamani.
Jecha aimeitia nchi aibu kubwa.CCM kushabikia uamuzi batili wa Jecha ni kufilisika kisiasa.
Matokeo kubandikwa vituoni hakuondoi kuwa CUF walifanya udanganyifu na ushahidi upo...Pia hujui kuwa kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi Zanzibar mgombea urais kujitangaza kuwa kashinda ni uhaini??.

Msipende kutaka muhurumiwe na kupewa urais kiujanja ujanja kwa kuaminisha watu sababu za uongo...
 
Back
Top Bottom