Rais Magufuli ahimiza viongozi kuandika vitabu

Magufuli aandike cha kwake aeleze jinsi maiti zilivyokuwa zikiokotwa fukweni, alipo Ben sanane, walipo wasiojulikana, beuya ndege anazoninua kinyemela nk.
 
Hata wakiandika, kuna mambo wataficha kwa maslahi ya Taifa...
 
Hivi Mkapa kaandika kuwa alitengana na Anna Mkapa ? Walirudiana tu Mkapa alipotaka kugombea Urais. Kama hajaandika hili basi katuficha mengi.

Kuna sehemu kagusia kuwa mkewe, Ana Mkapa, ni mvumilivu.

Pia, kagusia kuwa, yeye [Ben] si mtu rahisi kuishi naye...

Labda hapo ndo alikuwa anadokeza magumu ya maisha yake ya ndoa.
 
"Serikali ya CCM na Mamlaka zake za Usimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wameshindwa kuonesha chembe ya ishara ya Haki. Kutarajia Haki itendeke siku ya mwisho katika sanduku la kura ni sawa na kutafuta bikra katika wodi ya Wazazi," Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba
 
Kitabu cha Seif kitakuwa na kurasa nyingi sana!!
maana ana matukio mengi sana ya kueleza....
nadhani pia bifu lake na Lipumba litakuwa ni kurasa/chapter madhubutu.....
 
Katika uzinduzi wa kitabu cha Rais mstaafu Benjamin Mkapa uliofanyika mapema leo, Rais John Magufuli amewahimiza viongozi wastaafu kuandika vitabu vya maisha yao.

Hususan, Rais Magufuli amesema atafurahi kusoma kitabu cha Maalim Seif Sharif Hamad.

Kwa kweli hata mimi nitafurahi sana, mno, kukisoma kitabu cha Maalim Seif.

Harakati zake za kupigania demokrasia zimeanzia mbali sana.

Na kilele chake nadhani kilikuwa ni ule uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi wa mwaka 1995!

Naamini Maalim alishinda urais wa Zanzibar.

Ila kwa inda na figisu ambazo inadaiwa ziliongozwa na Rais mstaafu Nyerere, ushindi wa kupikwa akapewa ‘Komandoo’ Salmin Amour! Hivi yuko wapi huyu mtu siku hizi??

Lakini, kweli Maalim anaweza kuandika kitabu chake na kutiririka kwa uhuru bila ya serikali kutaka kumfanyia cencorship?


Nitakitafuta kitabu cha Baba Mkapa nikisome. Najua hajaelezea mara baada yavkuwa rais alivyokataa pongezi za Kitwana Kondo na kumwambia Mzee Kondo aende kuchapisha pongezi gazetini, wakati huo huo akipokea Range Rover Vogue alilooewa kama zawadi na Andy Chande.

Kuhusu Maalim kupoko ywa urais Zanzibar, CCM ikianza kuiba kura Zanzibar tangu enzi ya chama kimoja.

Katika kura za "Ndiyo" au "Hapana" za 1985, Idris Abdul Wakil, mgombea pekee wa chama pekee cha CCM, alishindwa kupata kura za kutosha za "Ndiyo".

Matokeo yakafika mpaka vyombo vya habari.

Watu wa Daily News wakawa wako tayari kuchapisha, wakaambuwa wasubiri.

Matokeo yakageuzwa, Wakil akatangazwa rais.

Kwa aibu, alivyomaliza kipindi chake kimoja, Idris Abdul Wakil hakugombea tena urais wa Zanzibar mwaka 1990.

Kioindi cha 1988 mpaka 1990 tukiwa tunaangalia Televisheni ya Zanzibar tulikuwa tunaona kuna kada mmoja hakosi kwenye kila taarifa ya habari. Kada huyo aliitwa Salmin Amour Juma. Baadaye tukaja kujua kumbe alikuwa anaandaliwa kuwa rais wa Zanzibar mwaka 1990.

Salmin Amour hasikiki siku hizi, amepata matatizo ya macho ni kama kipofu. Ubabe wote kaishia kuwa mtu anayetegemea msaada wa watu tu, na mpaka mke wake amemkimbia.

Hiyu ni mtu aliyesifika kwa jina la "Commando".

Ama kweli, hujafa hujaumbika.
 
Nitakitafuta kitabu cha Baba Mkapa nikisome. Najua hajaelezea mara baada yavkuwa rais alivyokataa pongezi za Kitwana Kondo na kumwambia Mzee Kondo aende kuchapisha pongezi gazetini, wakati huo huo akipokea Range Rover Vogue alilooewa kama zawadi na Andy Chande.

Kuhusu Maalim kupoko ywa urais Zanzibar, CCM ikianza kuiba kura Zanzibar tangu enzi ya chama kimoja.

Katika kura za "Ndiyo" au "Hapana" za 1985, Idris Abdul Wakil, mgombea pekee wa chama pekee cha CCM, alishindwa kupata kura za kutosha za "Ndiyo".

Matokeo yakafika mpaka vyombo vya habari.

Watu wa Daily News wakawa wako tayari kuchapisha, wakaambuwa wasubiri.

Matokeo yakageuzwa, Wakil akatangazwa rais.

Kwa aibu, alivyomaliza kipindi chake kimoja, Idris Abdul Wakil hakugombea tena urais wa Zanzibar mwaka 1990.

Kioindi cha 1988 mpaka 1990 tukiwa tunaangalia Televisheni ya Zanzibar tulikuwa tunaona kuna kada mmoja hakosi kwenye kila taarifa ya habari. Kada huyo aliitwa Salmin Amour Juma. Baadaye tukaja kujua kumbe alikuwa anaandaliwa kuwa rais wa Zanzibar mwaka 1990.

Salmin Amour hasikiki siku hizi, amepata matatizo ya macho ni kama kipofu. Ubabe wote kaishia kuwa mtu anayetegemea msaada wa watu tu, na mpaka mke wake amemkimbia.

Hiyu ni mtu aliyesifika kwa jina la "Commando".

Ama kweli, hujafa hujaumbika.

Duh!

Sasa kama mgombea ni mmoja tu, kwenye kupiga kura kunakuwa na option ya ‘ndiyo’ au ‘hapana’ na yeye Bw. Idrisa alipata za ‘hapana’ nyingi kuliko za ‘ndiyo’? Au ilikuwaje?
 
Nitakitafuta kitabu cha Baba Mkapa nikisome. Najua hajaelezea mara baada yavkuwa rais alivyokataa pongezi za Kitwana Kondo na kumwambia Mzee Kondo aende kuchapisha pongezi gazetini, wakati huo huo akipokea Range Rover Vogue alilooewa kama zawadi na Andy Chande.

Sir Andy Chande....nakumbuka alikuwaga kwenye bodi ya wadhamini wa SRSS...
 
Magufuli naye aandike sio afurahie vya watu tu maana ya Mungu mengi anaweza asifike ustaafu,naamini mpaka sasa anayo mengi sana
 
Maalim akiandika kitabu awamu hii lazima kitaletewa zengwe kuuzwa, Mkapa amekiri mauaji yaliyotokea kule Zanzibar yalimuumiza sana, yale mauaji yalisababihwa na uchaguzi na kilichosababisha mauaji ni wizi wa kura za Maalim Seif, hili hakutaka kulidadavua sasa Maalim akiandika lazima litawekwa wazi.
 
Duh!

Sasa kama mgombea ni mmoja tu, kwenye kupiga kura kunakuwa na option ya ‘ndiyo’ au ‘hapana’ na yeye Bw. Idrisa alipata za ‘hapana’ nyingi kuliko za ‘ndiyo’? Au ilikuwaje?
Ndicho kilichotokea, watu wakamsitiri mzee wa watu wametoka naye mbali sana.

Watu waliokuwa wanafanya kazi za juu Daily News mwaka 1985 wanajua haya mambo, ila ndiyo kama wamekula kiapo.

Siku moja nilikuwa nimekaa na balozi mmoja alikuwa mkubwa sana kwenye system.

Sasa tumekaa kifamilia tunapata dinner, akawa ka relax, anaongea kifamilia.

Tukaongea nini sijui, akasema, ule uchaguzi wa Zanzibar Hamad alishinda, CCM ikampokonya ushindi.

Yani mpaka hapo hayo maneno nilikuwa nayasikia sikia tu mitaani na kwa upinzani. Nikawa naweka asilimia kwamba inaweza kuwa kweli, lakini nikawa sijajiridhisha kwa sababu maneno ya wapinzani kila sehemu ni kwamba wameibiwa kura.

Basi huyu baba ambaye basically ni mtoto wa kulelewa na Nyerere ambaye amefanya kazi miaka mingi serikalini, aliposema hivyo, nikaona mpaka huyu kusema hivi, maneno haya ni ya kweli. Maana huyu hana sababu ya kuisingizia serikali maneno ya uongo.
 
Sir Andy Chande....nakumbuka alikuwaga kwenye bodi ya wadhamini wa SRSS...
Alimpa Mkapa Range Rover Vogue tulikuwa tunaliona linapaki Sea View pale.

Nikataka kuona kama Che Nkapa ataligawa au kulirudisha.

Hakugawa wala kurudisha kitu.
 
Alimpa Mkapa Range Rover Vogue tulikuwa tunaliona linapaki Sea View pale.

Nikataka kuona kama Che Nkapa ataligawa au kulirudisha.

Hakugawa wala kurudisha kitu.

Hii stori niliisikia toka kwa reliable source moja hivi miaka ya 96/97 hivi.

Wewe ni mtu wa pili sasa!

Ndo ‘Mr. Clean’ huyo....
 
Back
Top Bottom