KalamuTena
JF-Expert Member
- Jul 7, 2018
- 13,189
- 17,157
Eeeh, nimekuelewa vizuri sana.Kuna mwanahabari mmoja mkongwe alipata kutukushangaa jinsi tulivyozuzuliwa na mwanasiasa mmoja ambaye hajapata kuandika mawazo kwenye karatasi watu wakasoma na angalau kujua huwa anaweza nini. Hivyo ndivyo wanasiasa wetu wengi walivyo.
Ni matatizo yetu wananchi wenyewe. Wengine tunapiga kura kwa sura ya mtu ilivyo, wengine kwa hadithi tu za kusikia yanayomhusu mgombea bila kudadisi ukweli wa hadithi hizo.
Hata kama tulikuwa tumepiga hatua kidogo kwa kutompigia mtu kura kwa sababu ya kabila lake tu, lakini katika mengine tuko chini sana.