Nikukumbushe
JF-Expert Member
- Jun 4, 2013
- 2,602
- 408
Tanzania imebadilika. Kila watanzania wamechafuka kimataifa. Kila wanapobeba paspoti ya Tanzania wanaonekana wauza unga. Nakumbuka Rais, umewahi kutamka hadharani kwamba unayo majina ya wauza madawa ya kulevya lakini kwa bahati mbaya uliamua kuwa kimya. Rais, Kikwete, kwenye kampeni ya Chama Chetu, 2010, hawa wauza unga kwa kiwango kikubwa walichangia kampeni zetu na kutupatia ushindi mkubwa. Licha ya kwamba walitusaidia, mheshimiwa rais, madhara wanayoleta katika taifa hili ni makubwa kiasi kwamba hauwezi tena kuyafumbia macho. Wauza madawa ya kulevya wanakuwa na nguvu za ajabu ndani yah ii nchi. Wanamiliki majumba makubwa humu nchini. Biashara nyingi na kubwa ni zao. Kila sehemu kwenye uchumi wetu wamo. Ni bora ukachukua hatua na kuwashugulikia kisheria kabla hawajaliyumbisha taifa.
Hawezi kuwataja utashangaa kuwa hata yeye yumo kwenye wauza unga au prince Ritz