Rais Kikwete kuhutubia Ijumaa

Rais Kikwete kuhutubia Ijumaa

Sitasahau siku ile niliyo acha baadhi ya majukumu yangu ya kila siku na kutoa macho kwenye TV ili kumsikiliza baba atasema nini juu ya wezi na ukosefu wa madawa kulikochangiwa na wazungu kutunyima misaada kisha nikaambulia hadith za ndezi dume
 
Hana mvuto wala ushawishi tena mbele ya umma kwani kesha poteza political legitimacy ya kuwa kiongozi wa nchi.

Well said, very weak president ever. Mbona haongee na vijana, anakimbilia wazee ambao hawawezi uliza swali hata moja, by the way acha azubae hivyohivyo kwani hao vijana ndo watakitoa chama chake madarakani next year
 
Ni Jakaya Mrisho Kikwete peke yake ndie Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Tujiandae kumsikiliza.
 
Kwani Wazee wa Daslam ni kundi linalotambulika Kikatiba? Mbona kila wakati kwenye mambo serious ya nchi huwa jamaa anakimbilia kuwahutubia hawa wazee? Hivi na Mkapa alikuwa anahutubia hawa wazee kama professori doktore J.K? Nijuzeni, sikuwa bongo wakati huo.
 
Atahutubia taifa kupitia wazee wa dar es salaam Ijumaa wiki hii alasiri.
chanzo: ikulu

Kama hivyo tumeliwa!! maana vitakuwa vijembe; nahau; methali na kuhama hoja kuharibu maudhui ya mada yenyewe kama alivyofanya kwenye bunge la katiba kisha ajitetee kwamba atakuwa anatoa maoni yake kama raia! (akili za mbayuwayu!) none the less; watanzania tumeshajua jinsi ya kuwabomoa hawa wezi wa CCM; tutakaza buti mpaka kieleweke!
 
Anaenda kuaga kwa wazee maana inawezekana asikutane nao tena.
 
Jinsi JK alivyo, anaweza hata kuchomekewa lituhumiwa limoja la ufisadi ndiyo akawa mwenyekiti wa mkutano huo. Kwani si ilishatokea? Miaka kadha iliyopita Iddi Simba alikuwa mwenyekiti wa mkutano wake mmoja na wazee pale PTA Hall wakati akiwa anatuhumiwa kuingiza hela za uuzwaji hisa za UDA katika akaunti yake binafsi.
 
I hope atapata maoni yetu humu ili asituangushe. Ijumaa bado mbali anaweza kubadilisha speech ili kuondoa kiu ya watanzania wengi wanaotaka kusikia mkuu wao anatoa mwelekeo gani wakati tunamaliza mwaka.
 
Si aende hata kuongea na wazee wa pwani kila siku wazee wa dar
inaudhi kweli.
hawezi kanyaga udsm hata kwa fimbo,wadada wanauza papuchi kwa kukosa mikopo wakati watu wamegawana hela ya umma escrow
 
Back
Top Bottom