Rais Kikwete 'hakuwa na jinsi'

Rais Kikwete 'hakuwa na jinsi'

Kumbe "hakuwa na jinsi" nilikimbilia kusoma nilifikiri "hakuwa na jinsia".
Rais Kikwete ni kawaida yake kutokuwa na jinsi kwenye jambo lolote linalohitaji maamuzi ya mkuu wa nchi.
 
Swali langu ni kwamba hivi kwanini hawa wanasiasa wanataka kutuhadaa sana, je kama ni maoni ya wananchi kwanin walikua wanamkashifu mzee warioba wakisema takwimu zake sio za kweli? nakama yalikua ni maani ya wananchi kwann walikua wanamponda mzee warioba?nashanga na nashindwa kupata jibu sahihi je ni kweli asilimia tajwa ni maoni ya wananchi?
 
Yaani kama Mzee wa watu angelijua kwamba kungelikuwa na fitna za kiwango cha juu namna hii - nafikiri asingelikubali hata kazi yenyewe ya kuongoza hiyo tume.
 
Na hizo 19% ambazo siyo za wananchi zimeongezwa za nini? au za wakina nan?
 
Hujaeleweka mkuu. Eleza hoja then uingize hisia zako. Ni muendelezo wa kulialia na kulalamika
 
Yaani kama Mzee wa watu angelijua kwamba kungelikuwa na fitna za kiwango cha juu namna hii - nafikiri asingelikubali hata kazi yenyewe ya kuongoza hiyo tume.
Kosa la Warioba ni kuendekeza njaa. Alivyoona mshiko wa CHADEMA ndo kajitoa kabisa ufahamu
 
Swali langu ni kwamba hivi kwanini hawa wanasiasa wanataka kutuhadaa sana, je kama ni maoni ya wananchi kwanin walikua wanamkashifu mzee warioba wakisema takwimu zake sio za kweli? nakama yalikua ni maani ya wananchi kwann walikua wanamponda mzee warioba?nashanga na nashindwa kupata jibu sahihi je ni kweli asilimia tajwa ni maoni ya wananchi?

Rais amesema kweli nyie ambao hamjui hesabu ndio mnao sumbuka. Rudi darasani ukajifunze ndipo uje humu jamvini.
 
Jk "katiba hii ni nzuri hakuna mfano wake barani afrika"hivi hii kauli ina ukweli wowote.
 
Jana ilimpasa kuhudhuria,kukabidhiwa Katiba inayopendekezwa na kuhutubu vile. Mh. Rais,kwa sauti na namna wananchi walivyokuwa kimya muda mwingi,hakuridhishwa na mchakato na mambo fulani kutokuwepo kwenye Katiba inayopendekezwa.

Rais alionesha dhahiri kutoufurahia mchakato kwa kumwaga misemo na rai za mara kwa mara juu ya kila jambo kuwa na muda wake na kadhalika. Akadokeza na mkutano wake na TCD bila ya kupunguza kilichoripotiwa.

Rais akagusa akidi. Takwimu ikatolewa. Akaithibitisha akidi. Hakuwa na jinsi. Rais amepokea kilicho tayari. Kisingeweza kubadilishwa Jamhuri Dodoma.

Pamoja na kauli mbalimbali za jana,waelewa wamejua kuwa Rais hakufurahia mchakato. Hata kura ya maoni amesita kuitamka moja kwa moja. Mh. Rais alikuwa pale kupokea tu. Hakuwa na nafasi ya kusema au kufanya vinginevyo. Hakuwa na jinsi.

Wananchi wanauliza,mbona wawakilishi wote wa jana ni 'wetu' kama chama tawala?

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam


Watoto wa mjini wanasema ni mwendo wa vipara tu. Vyama vyote vilialikwa kama hawakutokea ulitaka Rais awafuate maofisini kwao?. Hii thread haina mashiko na ni craaaaaaaaaaaaaap.
 
wananchi tuipinge hii rasmu hata baada ya kupita tuendelee kuipinga na kuufanya ulimwengu uelewe kwamba hii katiba si yetu bali ni ya ccm
 
Katiba ikipigiwa kura itapita utake usitake. CCM utawazidi kwa hoja lakini huwezi kuwazidi katika mbinu za wizi wa Kura.

hivyo Raisi aendelee na msimamo wake kuwa Katiba iwe mwaka 2016. Na Raisi ahakikishe ana usemi wa nani atamridhi kiti chake. hawa wanaomdharau wasiwe wamemshamyang'anya hata maradara ya kumuandaa mrithi

Mimi sina wasiwasi kuwa katiba hii hata ikipigiwa kura itapita.Mimi naona sisi wapinzani tumekosa mwelekeo na hoja ya kusimamia.
 
Jana ilimpasa kuhudhuria,kukabidhiwa Katiba inayopendekezwa na kuhutubu vile. Mh. Rais,kwa sauti na namna wananchi walivyokuwa kimya muda mwingi,hakuridhishwa na mchakato na mambo fulani kutokuwepo kwenye Katiba inayopendekezwa.

Rais alionesha dhahiri kutoufurahia mchakato kwa kumwaga misemo na rai za mara kwa mara juu ya kila jambo kuwa na muda wake na kadhalika. Akadokeza na mkutano wake na TCD bila ya kupunguza kilichoripotiwa.

Rais akagusa akidi. Takwimu ikatolewa. Akaithibitisha akidi. Hakuwa na jinsi. Rais amepokea kilicho tayari. Kisingeweza kubadilishwa Jamhuri Dodoma.

Pamoja na kauli mbalimbali za jana,waelewa wamejua kuwa Rais hakufurahia mchakato. Hata kura ya maoni amesita kuitamka moja kwa moja. Mh. Rais alikuwa pale kupokea tu. Hakuwa na nafasi ya kusema au kufanya vinginevyo. Hakuwa na jinsi.

Wananchi wanauliza,mbona wawakilishi wote wa jana ni 'wetu' kama chama tawala?

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

Unapotosha mkuu, JK ni msanii kama walivyo CCM. Nimepoteza imani kabisa na Rais Kikwete, sijui nani ataiokoa nchi yetu na manyang'au wanaotupeleka shimoni mchana kweupe.

Jana jioni nilisikiliza BBC wakizungumzia na hili la Katiba ya Tanzania. Mchangiaji mmoja wa Kenya akasema kuwa Tanzania haitapata Katiba mpya ya wananchi hadi wachapane kama walivyochapana wao (Kenya). Alizungumza kitu kibaya sana, lakini ulikuwa ni ukweli mtu. Mchangiaji mweingine wa Kenya vilevile, akasema Wanasiasa hawawezi kuwapa Watanzania Katiba wananchi ila wanajitengenezea Katiba yao wenyewe (tafsiri ni yangu).

Vv
 
Back
Top Bottom