VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,006
Jana ilimpasa kuhudhuria,kukabidhiwa Katiba inayopendekezwa na kuhutubu vile. Mh. Rais,kwa sauti na namna wananchi walivyokuwa kimya muda mwingi,hakuridhishwa na mchakato na mambo fulani kutokuwepo kwenye Katiba inayopendekezwa.
Rais alionesha dhahiri kutoufurahia mchakato kwa kumwaga misemo na rai za mara kwa mara juu ya kila jambo kuwa na muda wake na kadhalika. Akadokeza na mkutano wake na TCD bila ya kupunguza kilichoripotiwa.
Rais akagusa akidi. Takwimu ikatolewa. Akaithibitisha akidi. Hakuwa na jinsi. Rais amepokea kilicho tayari. Kisingeweza kubadilishwa Jamhuri Dodoma.
Pamoja na kauli mbalimbali za jana,waelewa wamejua kuwa Rais hakufurahia mchakato. Hata kura ya maoni amesita kuitamka moja kwa moja. Mh. Rais alikuwa pale kupokea tu. Hakuwa na nafasi ya kusema au kufanya vinginevyo. Hakuwa na jinsi.
Wananchi wanauliza,mbona wawakilishi wote wa jana ni 'wetu' kama chama tawala?
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Rais alionesha dhahiri kutoufurahia mchakato kwa kumwaga misemo na rai za mara kwa mara juu ya kila jambo kuwa na muda wake na kadhalika. Akadokeza na mkutano wake na TCD bila ya kupunguza kilichoripotiwa.
Rais akagusa akidi. Takwimu ikatolewa. Akaithibitisha akidi. Hakuwa na jinsi. Rais amepokea kilicho tayari. Kisingeweza kubadilishwa Jamhuri Dodoma.
Pamoja na kauli mbalimbali za jana,waelewa wamejua kuwa Rais hakufurahia mchakato. Hata kura ya maoni amesita kuitamka moja kwa moja. Mh. Rais alikuwa pale kupokea tu. Hakuwa na nafasi ya kusema au kufanya vinginevyo. Hakuwa na jinsi.
Wananchi wanauliza,mbona wawakilishi wote wa jana ni 'wetu' kama chama tawala?
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam