Rais Kikwete awapandisha vyeo makanali


Nafurahi kuona umenielewa mapema sana! Thumb up for you!
 
Kuwapandisha watu vyeo imekuwa nongwa kwani gharama ni kubwa kuliko ile mnayolipana posho huko serikalini? Jeshi lina mambo yake waache
 

Haya nilikuwa siyafahamu!
 
Kwa hiyo akipandisha mwaka huu asipandishe tena. Hawastaaf wala hawafi? Kila mwaka nadhani kupanda vyeo ni lazima kwa baadhi ya watu na kustaafu lazima.

 
Kikwete kafanya hivyo bila kuzingatia mahitaji halisi ya jeshi na uwezo wa nchi kuwahudumua magenerals wengi.
Usilolijua litakusumbua.Raisi ni Amiri jeshi mkuu anajua vizuri mahitaji ya Jeshi kuliko mtu yeyote ambaye sio amiri jeshi.Kuongezeka idadi ya watu,kukua kwa uchumi n.k ni baadhi ya vitu visababishavyo Jeshi kupanuka kila eneo.Jeshi ni fani kama udaktari ilivyo fani tuheshimu fani za watu.Uwezo wa kuhudumia Jeshi upo na kauzingatia kama kimoja cha kigezo cha kuwateua.Pia tujue kuwa kama ilivyo maofisi mengine Jeshini pia hupanda vyeo vigezo vikifikiwa.Hawakai Cheo kimoja milele!!!!!
 

Ni kweli kama anastahili cheo lazima apandishwe mana anastahili. Atatumika wapi hilo ni suala litakalo kuja baadae
 
Hata kwenye majeshi hawamo,inatisha,inabidi wazingatie mawaidha ya Mufti kuwa wasiitupe elimu dunia na kuangalia upande mmoja,watabaki kulalamika kila siku.

Kinyesi at work!!!! mtu kaleta taarifa then wewe unaiangalia kwa RELIGIOUS PERSPECTIVE tena si kwa lengo la kujenga bali KUBOMOA, ukiitwa MCHAWI AU MZANDIKI utakataa? Any way acha nikufananishe na KINYESI.
 
Nikitumia slogan ya book 7, mbona wengi wao ni wa Kaskazini, ina maana Mkuu wa Majeshi naye ni CDM?

Tiba

Wewe, ugojwa wa ukanda unautoa wapi katika mambo muhimu namna hiyo ya nchi? Siyo kila mahali wanafanya kazi kisiasa. Mambo ya jeshi hayana ukanda. Futa kauli yako haraka sana kwa kuwa kichwa chako kina vizusi vya ukanda na ukabila.
 
Hv structure ya jeshi ipoje mpaka mahitaji ya mabregedia iwe kubwa hv?
Mbona makanal 75 % wenyewe ni wa hapa hapa dsm (watakuwa wameoneana aibu)na shart la zaman kipindi cha mkapa na waitara ilikuwa ni lazima waende msata wakapige ile course lkn kuna mmoja tunamjua haendi .
Sasa tunataka operation zaidi
 
ADC kirefu chake tafadhari.
Fidel80,

..ADC ni kifupi cha Aide de camp. kwa Kiswahili tunaita mpambe.

..Aide de camp au mpambe ni yule askari wa JWTZ unayemuona anamsindikiza na kumsaidia Raisi.

..Makamanda wote wa JWTZ kuanzia ngazi ya Brigadier General huwa wanakuwa na aide de camp.


Phillemon Mikael,

..nakubaliana na wewe kwamba Brig Gen ni cheo kikubwa kwa adc.

..huenda JK akapewa adc mwingine kuchukua nafasi ya Brig.Gen.Ibrahim Kimario.

..kama hatapewa brigade ya kuongoza basi Brig.Gen.Kimario anaweza kuteuliwa kuwa Mwambata wa Kijeshi ktk balozi zetu.
 
Last edited by a moderator:
Wewe, ugojwa wa ukanda unautoa wapi katika mambo muhimu namna hiyo ya nchi? Siyo kila mahali wanafanya kazi kisiasa. Mambo ya jeshi hayana ukanda. Futa kauli yako haraka sana kwa kuwa kichwa chako kina vizusi vya ukanda na ukabila.

Mkuu ungeanza kuwakemea hao wenye hiyo slogan. Mimi nimeiga tu. Au hiyo slogan kuna mahali inaruhusiwa kutumika na kwingine hairuhusiwi? Au labda hiyo slogan ina trade mark kwamba wengine si ruhusa kuitumia.

Anyway, I was not serious ila nilikuwa nawachokoza book 7 maana hao ndio mabingwa wa ukabila.

Tiba
 

Niko macho kodo,nataka kuona kama Br. Gen I. Kimario kama ataendelea kuwa A.D.C So far kwa nafasi yake ya sasa kicheo naye anastahili kuwa na A.D.C
 
Niko macho kodo,nataka kuona kama Br. Gen I. Kimario kama ataendelea kuwa A.D.C So far kwa nafasi yake ya sasa kicheo naye anastahili kuwa na A.D.C

..lakini Brig.Gen.Kimario kwa taratibu za kijeshi anastahili kuwa na adc.

..lets wait and see kama Brig.Gen.Kimario atakakuwa retained kama adc wa Raisi, and also kama atapewa adc wake mwenyewe.

cc gobore, Echolima, Moshe Dayan, Phillemon Mikael
 
Last edited by a moderator:
Hongereni makanda. lakini mbona makamanda kama kina Sukambi Mahela, au kina Msindai, Mfikirwa, Msingiri, Mwaya, Masalamado n.k- walioshughulika kule Comoro hawamo? Amiri Jeshi tafadhali wakumbuke!!

Sukambi Cheo kimepanda toka Mwaka jana.Hivi sasa Amekuwa Mkuu wa kanda kijeshi.Hata ile Operation kimbunga yeye Ndio alikuwa anaisimamia akishilikiana na afande Silo kutoka jeshi la Polisi
 
Mila na Desturi Za Kijeshi ..kwa Nchi karibu zote Mkuu wa Nchi anakuwa na ADC Kanali.......,Rais Kikwete kuweka rekodi nyingine ya kuwa Mkuu wa Nchi anayelindwa na Brigedia General ....huu ni muendelezo wa uvunjaji wa destruri Za Kijeshi....,Kama pia ile ya kuwa na Luteni General mmoja kwenye service ambako kuna kipindi walikuwa watano active..na Sasa wamebaki wanne ..Baada ya Sylvester Rioba kustaafu ( wamebaki Lt gen ndomba,Lt gen Kisampa, lt gen makakala..,lt gen Mella)...
Bado Idadi ya Maj Gen imekuwa kubwa Sana kuliko muundo unavyosema...na Hao Brigadia Generals Ndio Hao.. tunatambua..jeshi linapanuka but not at that rate . ...Kama Sasa tunashusha hadhi ya Bregadier General hadi kuwa aDC ..kaz ya colonel...safari ni Ndefu...kazi ya ADC inafanywa na kuanzia cheo cha Maj hadi colonel ..

Kwenye picha anaonekana Brigadier General ( angalia mabegani )
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…