Majeshi yangu bora ya Afrika 2024

T14 Armata

JF-Expert Member
Mar 7, 2017
10,650
34,938
Ni kazi kubwa sana kupima uwezo wa kijeshi wa nchi, kuna vigezo vingi hutumika na pengine kwa malengo tofauti. Kuna vyanzo ranking huzingatia namba kwamba idadi ya zana na wanajeshi, hii ni rahisi kufanya na hutumiwa pale mtu asipotaka mambo mengi ila sio sahihi. Hakuna ranking inayoweza kutoa majibu 100% kwa usahihi ila ranking nzuri inatoa makadirio yanayoendana na ukweli.

Kwanza kabisa ranking yangu haihusishi majeshi dhidi ya makundi ya waasi, magaidi au makundi ya kiitikadi yanayotaka kujitenga. Hii ni kulinganisha jeshi la nchi endapo lingepigana na jeshi la nchi nyingine.
Nimekwepa mtego huo sababu una mkanganyiko hata kwingineko duniani. Uturuki ina jeshi kubwa, ila ina waasi wa kundi la PKK wanaisumbua. Huwezi sema basi Uturuki haina nguvu sababu PKK hawaiwezi, ile ni ideology sio silaha. Au huwezi sema nchi ya Sao Tome and Principe yenye population ndogo kuliko idadi ya wanajeshi wa Misri, eti ina jeshi bora zaidi ya Misri sababu Sao Tome and Principe wenye wanajeshi less than 1,000 hakuna kundi la kigaidi na Misri kule Sinai kuna magaidi.

Imagine uiambie JWTZ ipigane na Wanyakyusa wakorofi iwaache watulivu. Sasa itajuaje kirahisi huyu Mwaikimba aliyepo Kigoma ni mkorofi, na huyu Mwamakula aliyepo Tanga ni msafi wakati wote wana act ni wasafi. Na Wanyakyusa wakorofi hawana kambi wala ofisi, wala hutakiwi kuua wote sheria za kimataifa zinakataa, na huwezi bomoa nyumba zote za Wanyakyusa utaathiri na wasio na hatia, na ukienda kuwatembelea hata ukihutubia wote wasafi na wakorofi wanakuona, wanajichanganya na wewe na wanakujua sababu umevaa sare unajulikana mwanajeshi wakati wao wamevaa fulana ya klabu au chama cha kisiasa wakati ni wakorofi.

Pia ukiachana na idadi ya silaha & zana na wanajeshi. Nimezingatia;

Ukubwa wa uchumi na rasilimali: Nchi yenye uchumi mkubwa inaweza piga nchi yenye uchumi mdogo. Inaweza kununua silaha bora na nyingi, inaweza chukua mkopo mkubwa wa silaha kama uchumi unaruhusu kulipa, ni suala la kutazama debt to GDP ratio na mambo mengine ya kiuchumi. Hapo usitarajie Rwanda kununua silaha sawa na DR Congo wakati wa shida.
Pia nchi yenye rasilimali nyingi kwa Afrika inaweza ziweka rehani ikakopa au ikaungwa mkono kwa misaada, silaha na kuungwa mkono kidiplomasia kama ambavyo Nigeria ilifanya kwenye vita ya Biafra. Waingereza wakapewa ahadi ya mafuta na USSR wakapewa ahadi ya iron ore, Wamarekani sijui walipewa nini. Kwa pamoja zikaiunga mkono Nigerian Federal government wakati kwa kawaida huwa hazikai pamoja kwenye migogoro na mwanzoni kila mmoja alikuwa upande wake (mojawapo ya sababu Kanali Ojukwu alikuwa na confidence, alijua anaungwa mkono).

Population: Nchi yenye watu wengi inaweza unda jeshi kwa muda wa dharula, ikapata reserves wa kutosha na kuendesha fronts nyingi. Inaweza sustain human loss kwenye vita, POWs, KIA, MIA, deserters.

Jiografia: 'Kiafrika' kuwa na bahari ni faida kijeshi, imports & exports sio rahisi kuzuiliwa na adui. Hapa Uganda ina disadvantage kubwa sababu iko landlocked inategemea Tanzania na Kenya. Ethiopia naona ina hasara kubwa ya kuwa landlocked kuliko nchi zote Afrika.
Pia nchi yenye majirani wengi kama Tanzania sio faida kiusalama kama nchi yenye jirani wachache.

Utawala wa nchi: Serikali za kidikteta hulizingatia sana jeshi hivyo zina majeshi makubwa, imara, yenye bajeti kubwa na utayari zaidi ya serikali za kiraia. Hata hivyo nchi za kiraia hupata support kubwa sana ya wananchi. Hapa Museveni au Kagame wako standby na majeshi ila kuna wananchi wengi sana wanaoamini jeshi ni la watawala wala haliwahusu raia. Kinachotokea mara nyingi kwenye vita na hizi nchi ni ushindi wa muda mfupi wa battles za mwanzoni, kisha nchi ya kiraia iki-gain momentum mobilization ya public inawapa nguvu kufanya counterattack. Yaleyale ya vita ya Kagera.

Pia nchi yenye rushwa, upendeleo wa matabaka, utawala mbovu, uongo na ufisadi iko more likely kuwa disorganized kwenye majeshi. Maofisa wa kamlete hawajawahi kuwa na uwezo mbele ya maofisa wanaojua waliopata kwa kustahili, wanajeshi walioingia ili waibe hela au wapate ajira ni hasara vita ikitokea. Iddi Amin alikuwa na Chief of Staff mpumbavu kwenye vita hadi maofisa waandamizi walipanga wamuue alikwamisha jeshi. Imagine Museveni ana mwanae Muhoozi ni Jenerali, hata akili zake na busara zake haziko sawasawa eti huyo aongoze jeshi.

Bajeti ya jeshi: Bajeti ina mchango wake ingawa exactly ni siri ila makadirio sahihi yapo na kwa sababu. Bajeti ya jeshi hupimwa kwa ratio ya GDP. Unakuta nchi inatumia 9% ya GDP yake kwenye ulinzi, wastani nchi nyingi duniani hazivuki 2%. Nchi Y inaweza kuwa ina $16 billion kama bajeti ya nchi nzima ila ikatumia 4% of GDP kwenye jeshi. Wakati X yenye uchumi mdogo wa $12 GDP inatumia 9% of GDP hivyo X ina bajeti kubwa ya jeshi.
Mazoea ya kuwa na bajeti ndogo kila mwaka husababisha kuwa na poor equipped military, unakuwa na zana za kizee na hazina maintenance nzuri (maintenance ya silaha ni gharama sana). Unakuwa na jeshi ilimradi, kupigia gwaride na kufanyia maonyesho. Hasara kubwa zaidi unakuwa huna uzoefu na silaha, mastering of arms ni suala la mazoea na makosa ya muda mrefu. Sio kama bodaboda unanunua tu kuendesha utajua mbele ya safari, silaha zina logistics zake, compatibility mfano umenunua fighter jets vipi kuhusu air to air missiles na spare parts, order yake ina muda wa kusubiri huendi yard China au Ufaransa ukafunga maboksi kama zana za kilimo, kuna geopolitics nyingi sana mara huyu anaona uko desperate na vita analazimisha ufanye kitu fulani ndio akuuzie silaha kwa bei ghali. Bado silaha zije uanze mafunzo na muda huo vita inaendelea, utapata matokeo mabovu sana ya matumizi. Silaha sio pikipiki kwamba kisa najua kuendesha Boxer basi hata TVS nitajua, yani rubani mzoefu wa Su-30 kwa miaka 7 ukimpa J-17 na mafunzo ya wiki ukamwambia kapigane unampa tiketi ya kifo.

Naishia hapa uzi usijefutika nikaanza upya...... Inaendelea
 
Inaendelea......
Ranking inaenda hivi.

1. Misri
Misri haijawahi ondoka kwenye nafasi ya kwanza ya majeshi bora Afrika. Ina historia ya kuleta upinzani wa maana dhidi ya Uingereza mwaka 1951 na 52 baada ya Misri kuvunja mkataba wa Suez na kuimiliki yenyewe. Uingereza na Ufaransa zilitaka kukataa ila kwa ubishi wa Misri na ushawishi wa Marekani ikaachwa. Pia imepigana na Israel mara mbili na kuleta upinzani mkali hasa mara ya pili.

Idadi ya wanajeshi: Zaidi ya 100,000 active wanaovaa sare na kuishi makambini na kulipwa rasmi kama wanajeshi.

Idadi ya ndege: Misri ina ndege zaidi ya 1,000 za kijeshi zikiwemo Dassault Rafale ya Ufaransa 4th generation, F-16 ya Marekani 4th generation, Mikoyan Mig-29M ya Urusi 4th generation, Mirage 2000 ya Ufaransa. Transport aircraft kama Soviet An-74 na American C-130 Hercules. Attack helicopters bora duniani AH-64 Apache ya Marekani, Ka-52 Alligator the best Russia can offer, Mil Mi-17 transport helicopter yenye kuaminika sana duniani kutoka Urusi.
Hapa kwa anga hakuna Mwafrika anajaribu kukaribia Misri.

Melivita: Tuanze na Mistral amphibious ships mbili kutoka Ufaransa, hizi zinabeba helicopters, zinatumika kama hospitali yenye vitanda zaidi ya 50 vya wagonjwa ndani wakati wa vita, zinabeba magari ya kijeshi 100 ndani, zinatumika kama command. Mistral ina tani 20,000 ikijaa. Meli nyinginezo ni kama FREMM frigate ya kisasa, wanayo pia Ufaransa, Italy, Marekani wameagiza, Morocco wanayo. Wana meli nyinginezo na speedboats, jumla wana naval assets zaidi ya 300 ikijumlishwa hata zile ndogo.
Bado Misri ina submarines za Romeo zipo 4 kutoka China, na Type 209 zipo 4 za kisasa na kuaminika kutoka Ufaransa.

Vifaru: Misri wana M1A1 Abrams MBT kutoka Marekani, tena hivi wamefanya co-production. Hii ni geopolitics ya hali ya juu kwao, ingawa Abrams zao ni model tofauti na wanayotumia Marekani mfano haina depleted uranium armour na baadhi ya electronics. Egypt wana Abrams 1,100.

Uchumi: GDP yao ni $1.47 trillion in PPP terms, sio maskini kabisa.

Population: Watu milioni 110+
 
2. Algeria
Algeria huwa inakaa #2 mara nyingi. Walianza fujo wakati wanatafuta uhuru kutoka Ufaransa wakapigana. Baada ya kuwa huru wakapigana muda mrefu kubishana kati ya kuwa secular au non- secular state. Walikuwa na makundi mengi ya kidini ila miaka ya 1990s wakatengamaa. Wamekaa kwa wasiwasi ndani yao, harakati za nchi za Kiarabu pamoja na chuki kubwa sana waliyonayo dhidi ya Morocco majirani zao.
Kuna miaka Algeria walinunua 45% ya silaha zote zilizonunuliwa Afrika.

Idadi ya wanajeshi: est. 320,000
Idadi ya ndege: Helicopters kama Mi-24 Hind, Mi-28 Havoc, Mi-17, Ka-27 za majini. Fighter jets kama Mig-29, Su-30 ambayo ni front line fighter na Su-24 for attack. Wana trainers za kisasa kama Yakovlev Yak-130 trainer bora zaidi ya Urusi, L-39 kutoka Ulaya hii inapendwa sana na nyinginezo. Wana transport aircrafts kama C-130 na Ilyushin Il-76

Melivita: Algeria wako vizuri kwenye Navy, naval assets zaidi ya 200. Kuna muda walikuwa na submarines 14 ila nyingine za zamani na nyingine nina imani ziko retired au mothballed.

Vifaru: Ina vifaru zaidi ya 1,400 vikiwemo vya zamani kama T-55. Wana T-90A zaidi ya 500 na version moja ya T-72 vifaru zaidi ya 300.

Uchumi: $516 billion in PPP.

Population: Milioni 47 hivi. Hawa wanalazimisha kuwa na wanajeshi wengi kinyume na population yao.

Bila kusahau Algeria wana missile arsenal & rocketry nzuri sana. Hata Iskander missiles wanazo
1000241892.jpg
 
3. South Africa
Hawa wana defense industry nzuri makampuni kama Denel yanaunda silaha za kuuza hata nje. Isingekuwa ujinga wa ANC weusi SA ingekuwa inauza silaha nyingi sana ila waliua viwanda. Wanaunda IFV na APC zao kama Rooikat, Mamba, Badger na Ratel iliyopata umaarufu vitani.

Idadi ya wanajeshi: est. 50,000

Idadi ya ndege: Hawa wamenunua Saab Jas-39 Gripen fighter nzuri sana kutoka Sweden. Wanayo Rooivalk attack helicopter ya kwao wenyewe waliunda, C-130 transport.

Melivita: SA ina melivita zaidi ya 40.

Vifaru: Almost 150 tanks vingine vikiwa in poor condition. Kwenye armoured personnel carriers na infantry fighting vehicles ndipo wana idadi kubwa. Plus vehicles kama za mortars, recovery, ambulance, reconnaissance, etc.

Uchumi: $990 billion PPP

Population: 60 million

South Africa jeshi lake linakufa, miaka michache ijayo litatoka top 5 kirahisi sana. Tangu makaburu waondoke na ambavyo nchi haina maadui kabisa wala haina jirani mwenye nguvu basi walidumaa. Pichani ni munitions zikitengenezwa na kampuni ya Denel
1000241913.jpg
 
4. Morocco
Morocco wana jeshi balanced hawaendi kwa hasira kama maadui zao Algeria. Wanapenda silaha chache ila za kisasa.

Idadi ya wanajeshi: est. 200,000

Idadi ya ndege: Ndege karibia 400 zikiwemo fighters kama F-16 na F-1 za Marekani, Mirage F-5 ya Ufaransa. Helicopters wana CH-47 Chinook ya Marekani kama transport, Ah-64 Apache kama attack, transport aircrafts ni C-130 na C-27 Spartan kutoka Marekani.

Melivita: Hapa wanajitahidi kuwa na meli zenye uwezo kama FREMM, Sigma na Frolean zote kutoka Ulaya. Wana naval bases 7. Naval assets idadi ni 120. Morocco hawana submarine.

Vifaru: Vifaru kama 1,000 variants kama M1A1 Abrams 220, MA12 160, T-72 150 na M60A Patton 400 hivi watakuja kuviacha. Pia wana Chinese VT-1 idadi 150.

Uchumi: $430 billion in PPP

Population: around milioni 40 hivi

Morocco wanazingatia sana artillery, missiles, rockets na drones sababu hawataki kutumia approach ya Algeria ya kuwa na namba kubwa ya silaha. Morocco wanataka precision zaidi. Wanazo HIMARS na Caesar.
Pichani ni melivita zao
1000241924.jpg
 
5. Nigeria
Hakuna nchi ya kukaa nafasi ya tano kama si Nigeria. Wana tatizo la ugaidi ila ni ideology vigumu kupambana nayo. Pia wana shida ya ufisadi jeshini, na morali ndogo sana. Wanajeshi wa Nigeria huliowa kidogo na maofisa wao hujilimbikizia mali.

Idadi ya wanajeshi: 200,000+ ila nina wasiwasi kuna wanajeshi hewa kiasi.

Idadi ya ndege: Rais Buhari alikuza sana military spending na alifanya sana procurement. Nigeria wana Chinese & Pakistani JF-17 4th generation fighter jet cache sana, wana Chengdu F-7 kama Tanzania ila za kwao zinapata sana ajari. Wana ground attack Embraer EMB 314 Super Tucano imependwa kwenye mashambulizi yake dhidi ya Boko Haram. Wana Alpha jets kutoka Ufaransa. Airforce yao ni average kwa nchi masikini ila wana idadi ndogo ya ndege.

Melivita: Wana frigate moja tu na makumi ya meli ndogo ndogo.

Vifaru: Wana VT-4 MBT kutoka China idadi 30 walichukua, T-72 kutoka Urusi walichukua miaka ya hivi karibuni. T-54 ya zamani na Vickers kutoka Uingereza, kutokana na historia yao ya utunzaji mbovu itakuwa Vickers vina hali mbaya maana hata spare parts ni shida kupata.
Pia wana IFV na APC na vehicles nyinginezo kwa idadi nzuri.

Uchumi: $ 1.1 trillion

Population: More than 200 million

Baadhi ya silaha zao
1000241939.jpg
1000241938.jpg


MWISHO
 
5. Nigeria
Hakuna nchi ya kukaa nafasi ya tano kama si Nigeria. Wana tatizo la ugaidi ila ni ideology vigumu kupambana nayo. Pia wana shida ya ufisadi jeshini, na morali ndogo sana. Wanajeshi wa Nigeria huliowa kidogo na maofisa wao hujilimbikizia mali.

Idadi ya wanajeshi: 200,000+ ila nina wasiwasi kuna wanajeshi hewa kiasi.

Idadi ya ndege: Rais Buhari alikuza sana military spending na alifanya sana procurement. Nigeria wana Chinese & Pakistani JF-17 4th generation fighter jet cache sana, wana Chengdu F-7 kama Tanzania ila za kwao zinapata sana ajari. Wana ground attack Embraer EMB 314 Super Tucano imependwa kwenye mashambulizi yake dhidi ya Boko Haram. Wana Alpha jets kutoka Ufaransa. Airforce yao ni average kwa nchi masikini ila wana idadi ndogo ya ndege.

Melivita: Wana frigate moja tu na nakumiss ya meli ndogo ndogo.

Vifaru: Wana VT-4 MBT kutoka China idadi 30 walichukua, T-72 kutoka Urusi walichukua miaka ya hivi karibuni. T-54 ya zamani na Vickers kutoka Uingereza, kutokana na historia yao ya utunzaji mbovu itakuwa Vickers vina hali mbaya maana hata spare parts ni shida kupata.
Pia wana IFV na APC na vehicles nyinginezo kwa idadi nzuri.

Uchumi: $ 1.1 trillion

Population: More than 200 million

Baadhi ya silaha zao View attachment 2893145View attachment 2893148

MWISHO
Ungeenda mpaka 10 bora.
 
Ni kazi kubwa sana kupima uwezo wa kijeshi wa nchi, kuna vigezo vingi hutumika na pengine kwa malengo tofauti. Kuna vyanzo ranking huzingatia namba kwamba idadi ya zana na wanajeshi, hii ni rahisi kufanya na hutumiwa pale mtu asipotaka mambo mengi ila sio sahihi. Hakuna ranking inayoweza kutoa majibu 100% kwa usahihi ila ranking nzuri inatoa makadirio yanayoendana na ukweli.

Kwanza kabisa ranking yangu haihusishi majeshi dhidi ya makundi ya waasi, magaidi au makundi ya kiitikadi yanayotaka kujitenga. Hii ni kulinganisha jeshi la nchi endapo lingepigana na jeshi la nchi nyingine.
Nimekwepa mtego huo sababu una mkanganyiko hata kwingineko duniani. Uturuki ina jeshi kubwa, ila ina waasi wa kundi la PKK wanaisumbua. Huwezi sema basi Uturuki haina nguvu sababu PKK hawaiwezi, ile ni ideology sio silaha. Au huwezi sema nchi ya Sao Tome and Principe yenye population ndogo kuliko idadi ya wanajeshi wa Misri, eti ina jeshi bora zaidi ya Misri sababu Sao Tome and Principe wenye wanajeshi less than 1,000 hakuna kundi la kigaidi na Misri kule Sinai kuna magaidi.

Imagine uiambie JWTZ ipigane na Wanyakyusa wakorofi iwaache watulivu. Sasa itajuaje kirahisi huyu Mwaikimba aliyepo Kigoma ni mkorofi, na huyu Mwamakula aliyepo Tanga ni msafi wakati wote wana act ni wasafi. Na Wanyakyusa wakorofi hawana kambi wala ofisi, wala hutakiwi kuua wote sheria za kimataifa zinakataa, na huwezi bomoa nyumba zote za Wanyakyusa utaathiri na wasio na hatia, na ukienda kuwatembelea hata ukihutubia wote wasafi na wakorofi wanakuona, wanajichanganya na wewe na wanakujua sababu umevaa sare unajulikana mwanajeshi wakati wao wamevaa fulana ya klabu au chama cha kisiasa wakati ni wakorofi.

Pia ukiachana na idadi ya silaha & zana na wanajeshi. Nimezingatia;

Ukubwa wa uchumi na rasilimali: Nchi yenye uchumi mkubwa inaweza piga nchi yenye uchumi mdogo. Inaweza kununua silaha bora na nyingi, inaweza chukua mkopo mkubwa wa silaha kama uchumi unaruhusu kulipa, ni suala la kutazama debt to GDP ratio na mambo mengine ya kiuchumi. Hapo usitarajie Rwanda kununua silaha sawa na DR Congo wakati wa shida.
Pia nchi yenye rasilimali nyingi kwa Afrika inaweza ziweka rehani ikakopa au ikaungwa mkono kwa misaada, silaha na kuungwa mkono kidiplomasia kama ambavyo Nigeria ilifanya kwenye vita ya Biafra. Waingereza wakapewa ahadi ya mafuta na USSR wakapewa ahadi ya iron ore, Wamarekani sijui walipewa nini. Kwa pamoja zikaiunga mkono Nigerian Federal government wakati kwa kawaida huwa hazikai pamoja kwenye migogoro na mwanzoni kila mmoja alikuwa upande wake (mojawapo ya sababu Kanali Ojukwu alikuwa na confidence, alijua anaungwa mkono).

Population: Nchi yenye watu wengi inaweza unda jeshi kwa muda wa dharula, ikapata reserves wa kutosha na kuendesha fronts nyingi. Inaweza sustain human loss kwenye vita, POWs, KIA, MIA, deserters.

Jiografia: 'Kiafrika' kuwa na bahari ni faida kijeshi, imports & exports sio rahisi kuzuiliwa na adui. Hapa Uganda ina disadvantage kubwa sababu iko landlocked inategemea Tanzania na Kenya. Ethiopia naona ina hasara kubwa ya kuwa landlocked kuliko nchi zote Afrika.
Pia nchi yenye majirani wengi kama Tanzania sio faida kiusalama kama nchi yenye jirani wachache.

Utawala wa nchi: Serikali za kidikteta hulizingatia sana jeshi hivyo zina majeshi makubwa, imara, yenye bajeti kubwa na utayari zaidi ya serikali za kiraia. Hata hivyo nchi za kiraia hupata support kubwa sana ya wananchi. Hapa Museveni au Kagame wako standby na majeshi ila kuna wananchi wengi sana wanaoamini jeshi ni la watawala wala haliwahusu raia. Kinachotokea mara nyingi kwenye vita na hizi nchi ni ushindi wa muda mfupi wa battles za mwanzoni, kisha nchi ya kiraia iki-gain momentum mobilization ya public inawapa nguvu kufanya counterattack. Yaleyale ya vita ya Kagera.

Pia nchi yenye rushwa, upendeleo wa matabaka, utawala mbovu, uongo na ufisadi iko more likely kuwa disorganized kwenye majeshi. Maofisa wa kamlete hawajawahi kuwa na uwezo mbele ya maofisa wanaojua waliopata kwa kustahili, wanajeshi walioingia ili waibe hela au wapate ajira ni hasara vita ikitokea. Iddi Amin alikuwa na Chief of Staff mpumbavu kwenye vita hadi maofisa waandamizi walipanga wamuue alikwamisha jeshi. Imagine Museveni ana mwanae Muhoozi ni Jenerali, hata akili zake na busara zake haziko sawasawa eti huyo aongoze jeshi.

Bajeti ya jeshi: Bajeti ina mchango wake ingawa exactly ni siri ila makadirio sahihi yapo na kwa sababu. Bajeti ya jeshi hupimwa kwa ratio ya GDP. Unakuta nchi inatumia 9% ya GDP yake kwenye ulinzi, wastani nchi nyingi duniani hazivuki 2%. Nchi Y inaweza kuwa ina $16 billion kama bajeti ya nchi nzima ila ikatumia 4% of GDP kwenye jeshi. Wakati X yenye uchumi mdogo wa $12 GDP inatumia 9% of GDP hivyo X ina bajeti kubwa ya jeshi.
Mazoea ya kuwa na bajeti ndogo kila mwaka husababisha kuwa na poor equipped military, unakuwa na zana za kizee na hazina maintenance nzuri (maintenance ya silaha ni gharama sana). Unakuwa na jeshi ilimradi, kupigia gwaride na kufanyia maonyesho. Hasara kubwa zaidi unakuwa huna uzoefu na silaha, mastering of arms ni suala la mazoea na makosa ya muda mrefu. Sio kama bodaboda unanunua tu kuendesha utajua mbele ya safari, silaha zina logistics zake, compatibility mfano umenunua fighter jets vipi kuhusu air to air missiles na spare parts, order yake ina muda wa kusubiri huendi yard China au Ufaransa ukafunga maboksi kama zana za kilimo, kuna geopolitics nyingi sana mara huyu anaona uko desperate na vita analazimisha ufanye kitu fulani ndio akuuzie silaha kwa bei ghali. Bado silaha zije uanze mafunzo na muda huo vita inaendelea, utapata matokeo mabovu sana ya matumizi. Silaha sio pikipiki kwamba kisa najua kuendesha Boxer basi hata TVS nitajua, yani rubani mzoefu wa Su-30 kwa miaka 7 ukimpa J-17 na mafunzo ya wiki ukamwambia kapigane unampa tiketi ya kifo.

Naishia hapa uzi usijefutika nikaanza upya...... Inaendelea
.
IMG_20240202_123417.jpg


Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
2. Algeria
Algeria huwa inakaa #2 mara nyingi. Walianza fujo wakati wanatafuta uhuru kutoka Ufaransa wakapigana. Baada ya kuwa huru wakapigana muda mrefu kubishana kati ya kuwa secular au non- secular state. Walikuwa na makundi mengi ya kidini ila miaka ya 1990s wakatengamaa. Wamekaa kwa wasiwasi ndani yao, harakati za nchi za Kiarabu pamoja na chuki kubwa sana waliyonayo dhidi ya Morocco majirani zao.
Kuna miaka Algeria walinunua 45% ya silaha zote zilizonunuliwa Afrika.

Idadi ya wanajeshi: est. 320,000
Idadi ya ndege: Helicopters kama Mi-24 Hind, Mi-28 Havoc, Mi-17, Ka-27 za majini. Fighter jets kama Mig-29, Su-30 ambayo ni front line fighter na Su-24 for attack. Wana trainers za kisasa kama Yakovlev Yak-130 trainer bora zaidi ya Urusi, L-39 kutoka Ulaya hii inapendwa sana na nyinginezo. Wana transport aircrafts kama C-130 na Ilyushin Il-76

Melivita: Algeria wako vizuri kwenye Navy, naval assets zaidi ya 200. Kuna muda walikuwa na submarines 14 ila nyingine za zamani na nyingine nina imani ziko retired au mothballed.

Vifaru: Ina vifaru zaidi ya 1,400 vikiwemo vya zamani kama T-55. Wana T-90A zaidi ya 500 na version moja ya T-72 vifaru zaidi ya 300.

Uchumi: $516 billion in PPP.

Population: Milioni 47 hivi. Hawa wanalazimisha kuwa na wanajeshi wengi kinyume na population yao.

Bila kusahau Algeria wana missile arsenal & rocketry nzuri sana. Hata Iskander missiles wanazoView attachment 2893075
kwa mara ya kwanza naona ndani ya thread yako umesifu zana za mrusi
big up braza
 
Jeshi letu tuliambiwa ni la sita kwa ubora duniani, inakuwaje hata kwenye Afrika pekee halipo kwenye top 5? 😁😁😁🙌
 
Back
Top Bottom