Ndugu yangu, kosa la Rais Kikwete ni lipi? Hivi kumwambia Rais Kagame azungumze na wabaya wake ili amani itamalaki Rwanda na ukanda huu wote ni kosa la kumshurutisha Rais wetu aombe raidhi? Aombe radhi kwa lipi?
Fikiria, ni kama wewe leo umwambie Rais Kikwete aketi na Chadema wamalize tofauti zao. Je, ni haki Rais Kikwete au Freeman Mbowe kuudhika? Je, watokee watu humu wakushurutishe uombe radhi kwa kauli yako, utakubali?
ndiyo maana nasema, Rais Kikwete ni rais wetu. Linapokuja suala la nchi na nchi, lazima tusimame upande wa Rais wetu hata kama wapo Watanzania wasiompenda. Suala la nchi lazima ushabiki wenu uwe mmoja. Hivi ninavyoandika majibu haya nasikiliza Redio DW ikitangaza kwamba Rais Obama kawatuma maseneta wawili, akiwamo John McCain (wote wa Republican) kwenda Misri kuhakikisha amani inarejea. Obama kafanya hivyo kwa manufaa ya Marekani. Linapokuja suala la nchi, Chadema, CCM, UDP, TLP na wasio na chama sote tunapaswa kuwa kitu kimoja. Rais wetu hawezi kutukanwa halafu tukashangilia. Tukishangilia, tutaonekana mazuzu mbele ya jumuiya ya kimataifa.
Naandika haya kwa kuwa naamini katika matumizi ya diplomasia ya mazungumzo kuelekea upatanishi wa amani ya kweli. Vita ni njia pekee ya mwisho katika kutafuta ufumbuzi wa mgogoro...kama tulivyofanya kwa Uganda ya Idd Amin.
.....kosa la Rais Kikwete ni lipi?
Nina imani kabisa, mkuu, alikuwa anajua serikali ya Rwanda ilikuwa imeanzisha utaratibu wa maridhiano kati ya wahanga wa mauaji ya kimbari mara tu baada ya hali ya amani kutengemaa kiasi nchini humo. Rejea taarifa hizi hapa chini
Background Information on the Justice and Reconciliation Process in Rwanda - Outreach Programme on the Rwanda Genocide and the United Nations
Rwanda’s Gacaca courts: a mixed legacy -- New Internationalist
Mbali na mapungufu machache kulinganisha na faida nyingi za utaratibu huu wa maridhiano ulioanzishwa na serikali ya Rwanda, bado FDRL hawakuonyesha nia ya dhati kushiriki katika utaratibu huu ili waijenge Rwanda ya wamoja.
Kwa kuzingatia haya, mkuu wetu, angeanza kuishauri serikali ya Rwanda irudishe utaratibu wa maridhiano wa Gacaca ambao iliufunga mwaka jana (2012) pia angewashauri FDRL wajumuhike katika mpango wa maridhiano ulioandaliwa na wanyarwanda kupitia serikali iliyopo madarakani nchini humo huku akiwa amehakikishiwa na Kigali kuwa itarudisha Gacaca. Kupitia ushauri huu nadhani maridhiano yangefikiwa kati ya Kigali na FDRL.
Mkuu wetu kuanza kutoa ushauri "alioutoa" huku akipuuza utaratibu ulikuwa imeanzishwa na Wanyarwanda ili waponyeshe vidonda vya mauaji ya kimbari, kwa maoni yangu, mkuu aliteleza ila hakuangua. Kwa maana hiyo anayonafasi kuangalia namna ya kurekebisha hili.
......Suala la nchi lazima ushabiki wenu uwe mmoja.
...Nakubaliana 100% na wewe katika hili. Hata hivyo, tunapokuwa upande mmoja na rais haimaniishi kuwa haturuhusiwi kutoa ushauri kwake ni upande upi atuongoze tusimame naye. Na ninaimani sote tutakuwa na furaha tutakapo simama upande mmoja na rais mahali ambapo huko mbeleni hatutamlaumu...kuwa alituchagulia upande wenye madhara kwa afya ya nchi yetu. Mwanzisha uzi huu katimiza wajibu wake katika hili. Mwanzisha mada anataka tusimame na rahisi mahali pa salama na majirani zetu. Uungwana ni kujua udhaifu wako ...na hapo unaufanyia kazi kuurekebisha udhaifu huo. Si maanishi kuwa lazima tuiombe radhi Kigali lakini tunaweza kutuma "envoy" Kigali kulizungumzia suala hili...najua tunaweza kuunda envoy ambayo inaweza kusimamia hili kama tunavyounda tume mbalimbali yanapotokea majanga.
...Rais wetu hawezi kutukanwa halafu tukashangilia. Tukishangilia...
Envoy tutakayoituma Kigali inaweza kulishughulikia hili pia...wanyarwanda wanaweza nao wakaona umuhimu wa kufuta kauli zao dhidi ya Rais wetu kwa namna ambayo sisi tutaonyesha kujali juhudi zao za kuleta maridhiano nchini mwao. Binafsi sishangilii kutukanwa Rais....au mtu yeyote mwenye nia njema na mwenzake. Kama nilivyoeleza mwanzo,mkuu wetu, ameteleza ila hajaanguka...hivyo tumshauri namna ya kutembea upande wa utelezi ili asiteleze tena na hatimaye kuanguka nasi tukaanguka pamoja naye.
......mazuzu mbele ya jumuiya ya kimataifa
Ukiona jumuiya yoyote ya kimataifa inakona zuzu wakati wewe unaangaika kuleta maridhiano kati ya wale wanaohasimiana au unaamulia ugomvi kwa wanoupigana. Basi ujue jumuiya hiyo ni
"JUMUIYA YA KISHETANI" wala usiisikilize.