figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,492
- 54,895
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete, amewakabidhi Askari Polisi Magari 399 mapya kati ya 777 yaliyoagizwa
ili kufanikisha Shughuli ya Uchaguzi.Magari haya yatawasaidia Polisi kufika Sehemu Mbalimbali kwa Wakati wa Uchaguzi na baada ya Uchaguzi.
Naye Naibu IGP Abdulrahman Kaniki kamshukuru Rais kwa kuja kuungana nao. Kasema "Kwa wale wachache ambao wanataka kutulazimisha kutumia shuruti, hatutasita kufanya hivyo na hatutakua na ajizi kwa sabuabu hilo ni jukumu letu tulilopewa kisheria na tutahakikisha kwamba sheria inachukua mkondo wake.
Lakini pia nikuhakikishie kuwa, hatutamuonea mtu wala hatutampendelea au Kumuogopa mtu kwa nafasi yake yoyote aliyo nayo. Sisi ni kuhakikisha kwamba sheria inachukua mkondo wake na nchi inaendelea kuwa na amani kama ilivyo kisiwa cha amani.
Vifaa hivi tulivovipata tutahakikisha tunatumia kwa uangalifu na utaratibu uliopo ili vilete tija kwa sababu tunatambua kwamba ni kodi za watanzania zimetumika kupata magari haya na vifaa vingine.
Tunakushukuru kwa kuja kuungana nasi katika tukio hili.
======================================
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongozana na Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe Mathias Chikawe, IGP Ernest Mangu wakati akikagua sehemu ya magari mapya 399 kati ya 777 aliyokabidhi kwa jeshi la polisi leo Jumanne Oktoba 20, 2015 huko katika Chuo cha Polisi Kurasini Dar es salaam.
PICHA NA IKULU
Last edited by a moderator: