Rais John Magufuli, Masters fake zipo NSSF

Rais John Magufuli, Masters fake zipo NSSF

Hili tatizo LA vyeti ni jipu niliona habari kuwa had wauguzi wanafoji vyeti nikajiuliza huyu siatashindwa hata kuchoma sindano.

Mkuu unazungumzia wauguzi hao ni cha mtoto je, umesahau kisa cha Daktari wa Muhimbili aliye fanya operation kwenye ubongo badala ya mguu - mgonjwa akapata ugonjwa wa kupooza upande mmoja - we fikiria , je, hicho ni kisanga cha kawaida kweli !!
 
Magufuli mwenyewe ana Ph.D fake.

Yea mzee. One can't imagine someone completing an experimental chemistry PhD while holding a cabinet position, and wait for it, finishing it in 3-years! At the time I told myself that he must be some sort of genius, but his public record and utterances since holding the high office say otherwise.
 
Yea mzee. One can't imagine someone completing an experimental chemistry PhD while holding a cabinet position, and wait for it, finishing it in 3-years! At the time I told myself that he must be some sort of genius, but his public record and utterances since holding the high office say otherwise.

Someone should unearth his PhD thesis, watu tufanye review. Watu tumeteseka kupiga PhD kwenye nchi za watu, for 4-years, full-time, biochemistry, upo maabara kila siku ya wiki bila sikukuu, halafu anakuja mtu anasema yeye kapiga ishu kwa miaka mitatu akiwa waziri. C'mon son!
Niliwaambia watu kwa kusema hivyo hivyo, asante kwa kuongezea nguvu hili mkuu.

There is no way Magufuli angeweza kufanya Ph.D ya Chemistry na kuwa waziri anasafiri nchi nzima muda huo huo na anashiriki vikao vya cabinet etc.

Jamaa kafanyiwa kisiasa.
 
MTU unakuta hana uwezo wa kudeliver ila ana elimu kubwa sana, nadhani vyeti fake ni tatizo kubwa na hawa wanaochomekwa unakuta wengi ni kujuana na wanapeana mikakati ya kufoji ili kupata nafasi huko serikalini na sehemu nyeti wengi shule hawana wamefoji, na ndo mana mambo hayaendi.
sio vyeti feki , tatizo mitaala ya elimu
 
Hakuna tabia inayokera kama hii ya mtoa mada yaani analalamika utadhani dominic akifukuzwa mshahara wa dominic atapewa yeye,acha ujinga,ni wapuuz tu huwa wanashangilia anguka la wengine,FANYA YAKO BROO kama we ni mwanaume its shame unatuaibisha
kweli mkuu, watu wana majungu saana
 
Ahaha watanzania bwana hii mambo ya uvyama inaturudisha nyumba sana. Kosa la mtoa mada liko wapi Sasa? Huyu ni raia mwema anatoa taarifa juu ya maovu, sasa povu lenu ni la nini, au na nyinyi ndio walewale wenye vyeti feki?
 
WACHUNGUZWE HAO WADAU WASIJE WAKATOKEMEZA VIINUAMGONGO VYETU, HAKUNA NJIA YA MKATO, CHETI FEKI HATA CHA DARASA LA SABA KWA MWENYE SHAHADA YA UZAMIVU NI FAKE MWANZO MWISHO, PIGA CHINI WAKAE WASAFI KAMA KWELI TUMEDHAMIRIA KUONDOA MAKANDOKANDO.
 
Fake ni fake tu. Kwanini abaki kama ana cheti feki .
 
Mpiganaji Mbwete muacheni yeye sio wa kwanza kuwa na cheti feki.Tumeshaona watu wenye vyeo vikubwa kuliko yeye wakiwa na PhD feki.wapo mawaziri lakini mfano mzuri aliyekuwa VC wa Mzumbe bwana Warioba alikuwa na PhD feki ndio masters ya Mbwete iwe issue?Cha muhimu Mbwete anafanya kazi iliyotukuka kuwasambalatisha pale Nssf.Hivyo mshindwe na mlegee.
 
Rais John Magufuli masters fake ipo NSSF ya Dominic Mbwete. Mhe Rais alipokuwa kwenye ziara bandarini na siku ya uzinduzi wa ndege mpya alieleza kuwa anawatafuta watu wenye elimu za juu ambao ni fake na wamepewa madaraka. NSSF yupo Acting Director wa DHRA anayedai kuwa masters yake ameipata University of Lincorn UK, hii Masters ina utata.

Waziri Mhagama ndiye waziri ambaye NSSF ipo chini yake, tunamuomba afuatilie uozo huu
We lazma utakuwa mmoja wa waliothibitika na vyeti feki ambao mbwete anawashughulikia
 
Hata cha bwana YULE || kwanza nahis bwabwa hebu tusijambishane
 
Acha majungu.. Kakuchukulia mpenzi wako nini? Hatuangalii elimu.. Tunaangalia uwezo wa kudeliver...

Mawazo ya ki puuzi sana haya, kwa kila wasio na shule ndio hukimbilia huku na hii imekuwa ikifanyika miaka dahali, haya huo uwezo ku deliver uko wapi? Kuna wenye uwezo wa ku deliver na wana vyeti hawapewi nafasi. Kuna wengine eti walikuwa na University yao tu na marafiki zao pale Morogoro, inaitwa ABBO UNIVERSITY, imetoa ma degree, Masters mpaka PHD kwa ma babies na maswahiba. Qualifications za ku join inategemea wewe rafiki yako nani. Sasa hao wote ndio wanaoongoza elimu ya Tanzania kwa sasa. Ona ilipofika sasa halafu wewe unabana pua 'eti wana deliver' karibu nikutukanie bi mkubwa angalau nimefundishwa pia kuheshimu mawazo ya wengine
 
Nchi yetu ina shida kubwa.
Mtoa mada ameamua kuanzisha mapambano kwenye mtandao wa kijamii.
Inaweza kuwa si mahali sahihi pa kuanzia kama ofisi zetu zina nafasi na utaratibu wa kushughulikia masuala yake ya ndani kwa umakini.
Bila kujali kama tuhuma ni za kweli ama hapana bado kunaweza kuwa na utaratibu mzuri wa kufuatilia hili.
Vyeti feki ni janga kwa taifa letu. Kuanikana kwenye mitandao ikishakuwa mazoea inaweza isichukuliwe kwa uzito wake au itakuwa mwanzo wa kuchafuana kwa yaliyo ya kweli na uongo.
Ni vyema taasisi zikawa na utaratibu mzuri wa kujiridhisha zinapoajiri watu.
Tabia ya kuwekana kwenye ofisi ndio chanzo kikubwa cha kutengeneza vyeti feki ili hata yule asiye na sifa apate nafasi kwa ulaghai/kughushi vyeti.
Tujenge Tanzania inayothamini taaluma.
 
Nadhani badala ya kuteteana humu utafutwe ushahidi halali tuu lakini mambo wivu, sijui, umbeya, mara anawabana NSSF hayasaidii hapa yeyote mwenye hoja ni ama alete uhalali wa elimu au mkae kimya na vyeti vyenu fake
 
Rais John Magufuli masters fake ipo NSSF ya Dominic Mbwete. Mhe Rais alipokuwa kwenye ziara bandarini na siku ya uzinduzi wa ndege mpya alieleza kuwa anawatafuta watu wenye elimu za juu ambao ni fake na wamepewa madaraka. NSSF yupo Acting Director wa DHRA anayedai kuwa masters yake ameipata University of Lincorn UK, hii Masters ina utata.

Waziri Mhagama ndiye waziri ambaye NSSF ipo chini yake, tunamuomba afuatilie uozo huu
Ukisikia majungu ndiyo haya. Dhahiri kuna kitu kimetokea kati yenu ndiyo maana unaleta ujinga wako humu. Kwanza huyo unayempelekea hili jungu naye anatuhumiwa kwa kupata Phd fake.
 
Back
Top Bottom