Rais Dk. John Magufuli kuhamia Dodoma

Rais Dk. John Magufuli kuhamia Dodoma

Ikulu ndogo ya Chamwino imeanza kufanyiwa Usafi tayari Kumpokea Rais Magufuli. Inasemekana hata Waziri Mkuu ataapishwa katika hii Ikulu ndogo ya Chamwino.

Shughuli nyingi za Rais, zitafanyika kutokea kwenye hii Ikulu.

fIGGANIGGA,....HATA JK alizindua serekali na aliapishia mawaziri chamwino...ngoja tuone
 
Nampa hongera kama ni kweli, lakini itakuwa ni mwendelezo wa kuigiliza aliyokuwa anayaamini Mheshimiwa Lowassa.

Acha uongo mama Anna wa ACT ndie aliyewahi kuahidi kuhamia Dodoma kama angeshinda urais,na si huyo lowasa wenu.
 
Hata ahamie mbinguni watanzania wanataka mabadiliko sio ujanja ujanja na danganya toto

Wewe umekaririshwa neno mabadiliko lakini hauelewi maana yake.Moja ya mabadiliko wanayotaka wananchi nı pamoja na hilo serikali kuhamia katıkati mwa nchi.
 
Kama kweli alikuwa na nia hiyo angeenda kuapishwa Dodoma na mpaka saa hizi alitakiwa awe Dodoma maana kule ndio makao makuu ya Nchi
 
Suala la kuhamia Dodoma lisimpotezee muda, halina umuhimu wowote, asilipe kipaumbele sana, ni la kisiasa tu ndiyo maana hata waanzilishi wake limewashinda kwa kipindi chote kile. Kama lingekuwa na manufaa nini kilizuia kuhamia ? JPM ana kazi kubwa sana inayomkabili kuliko hiyo theory ya kuhamia Dodoma. Kwani TZ inakosa nini kwa kutohamia Dodoma?
 
Bora ahamie tu Dodoma maana Dar haimfai kwani sasa ni jiji la UKAWA.
 
Sawa lakini hata waliokaa ikulu ya magogoni walikuwa na sababu. Wale walioamua makao makuu kuhamia Ddm ingeku ni sasa wasingeamua hivo. It was an outcome of cold war and ubeberu. Iliaminika ddm ni salama. Lkn sasa kukua kwa tkngia si sabb tena

Una uhakika na ulichokiandika? Na kuwa katikati ya nchi kijiografia?
 
Ukitaka mabadiliko zaidi ya kasi anayokwenda nayo Magufuli, basi we zungusha mikono tu, mbele mara 2 na zungusha kurudi nyuma mara 3, vp, unajisikiaje mwilini!? huoni kama kajasho kidogo,! hayo tayari sasa ndio mabadiliko ya malofa.

Hahaha
 
Ikulu ndogo ya Chamwino imeanza kufanyiwa Usafi tayari Kumpokea Rais Magufuli. Inasemekana hata Waziri Mkuu ataapishwa katika hii Ikulu ndogo ya Chamwino.

Shughuli nyingi za Rais, zitafanyika kutokea kwenye hii Ikulu.
Kila mara baada ya uchaguzi mkuu unaompata Rais mpya haya hufanyika. Rais atakaa hapo kwa muda na hasa kama jina atakalopendekeza kuwa waziri mkuu litagonga mwamba! Hii si uthibitisho wa serikali kuhamia Dodoma. Hizi tetesi hazimtendei haki Rais Magufuli, mnamweka kwenye tafrani.
 
Nimepewa tetesi kuwa Rais Magufuli kakataa kuishi Dar na ameagiza kuhamishiwa Dodoma yalipo makao makuu ya nchi.

Mlio jikoni tupeni uhalisia wa hili.

ilikuwa iwe surprise yake ya tatu baada ya kutoka MOI. Lkn wakaomba kuwa hapako vizuri, wakaomba muda kidogo wafanye ukarabati. ndio maana baada ya kutowezekana, ni kama ratiba zake zilivurugwa.

tuone sasa wazir gani atakaa dsm wkt rais yuko dodoma
 
Ukitaka mabadiliko zaidi ya kasi anayokwenda nayo Magufuli, basi we zungusha mikono tu, mbele mara 2 na zungusha kurudi nyuma mara 3, vp, unajisikiaje mwilini!? huoni kama kajasho kidogo,! hayo tayari sasa ndio mabadiliko ya malofa.

Acha ulofa, kwa sababu unaanza kusoma bure kumalizia f4 yako ndio unakuwa lofa hivi?
 
Ni heri ahangaike kuzunguka humu humu ndani ya nchi na kuona shida za wananchi.

Kuliko jamaa yangu yule aliyekuwa akiruka na kula nje kwa nje na kurudi kwenye jiji la kipindupindu.
 
Ujanja ujanja tuu wa CCM watu tunasuburi kazi sipo porojo tuu mara atembelea muhimbili,mara sijui ashtukiza bank kuu.come on ..tunataka mambo ya misingi..Ahamie Dodoma ???? Ni ngumu kuliko alivyobebwa na kuingia Ikulu...
mkuu mlitaka afanye nini ili mfurahi?
wewe na Elli inaonekana mmeguswa kinyume kabisa na magufuli.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom