1. asiende kwenye nyumba za ibada kushawishi apewe kura.
2. asiseme atajenga bara bara na kudumisha afya kwani ni wajibu wa serikali kutenda izo kazi na awatumii pesa yao bali ni kodi za wananchi.. sitoi kura ukija na sera za dizaini hii.
3. tunamtaka raisi ataeinua uchumi wa nchi ikiwa ni pamoja na kutoa vipaumbele kwa elimu, kilimo na viwanda. kwanini? hii itasaidia sana kwa vijana wengi kupata ajira, wakulima kuuza bidhaa zao kwa viwanda vya ndanii. Itasaidia kuinua uchumi wa nchi sana kwa kuuza bidhaa za viwandani ndani na nje ya nchi pia wakulima watauza bidhaa na kupata soko nje na ndani. na watanzania wengi watapata ajira.
4. Asiingize siasa kila sekta mfano mzuri ni sekta ya elimu.. Hii sio sekta ya kufanya mambo ya mzaa kama kufaulisha wanafunzi ili upate kura. Watoto hawajui kusoma wanaenda form one.. Hii italeta madhara kwa nchi sanaa kwani kuna ushindani wa kidunia katika ajira sio ajabu kwa mtanzania kuajiriwa marekani, kenya na popote pale. Ila ukiwa na wajinga wenye vyeti vya ufaulu mzuri madhara yake ni makubwa sana ndani ya taifa ndio yalee tunayoyaona kwa baadhi ya vijana, waheshimiwa flani waliokosa uadilifu. Ili taifa liendelee inabidi kuwe na watendaji wenye upeo. Hata ukishinda kwa kufaulisha watu wewe na familia yako mtapata neema ila Tanzania jee?
5. Raisi awe mjasiri asiye yumbishwa, mzalendo ataeweza kuondoa mfumo ulioko sasa wa kujuana ndio ufanikiwe natoa mifano kidogoo katika soko la ajira uwezi kupata mpaka ujue mtu. pili kwa sasa Tanzania kila kitu mpaka uwe mtoto wa mkubwa ndio ufanikiwe hii imeonekana sanaa sehemu nyingi hata katika shindano la miss tz ambae kafoji vyetii sio hukoo tuu ila wenzangu na mimi tukifojii ndio sheria inafanya kazi.. Hatutaki rais ataeendeleza huo upuuzi kila mmoja awe chini ya sheria.
6. rais mwenye msimamo hasa katika maamuzi yake yakiutawalaa... Kazi ya uraisi ni kazi yenye changamoto kubwa sanaa inabidi uweledi wa hali ya juu sana.. Tunamtaka kiongozi asiekata tamaa akipata changamoto za kiutawala kiasi cha kukimbia madarakani. Viongozi wengi walioachia ngazi baada ya kutoa maamuzii yasiyo na weledi na kuachia ngazi hawafai kabisa kwani atafanya jambo kwa taifa na kukimbia nchi.
7. asiwe na skendo zozote za wizi, ufisadi, uroho wa madaraka, mbinafsi, kinyongo, awe mpenda haki na anaesimamia sheria.
8. afanye mambo kwa maslahi ya taifa na sio kwa ajili ya chama chake sio kiongozi ataewaondoa madarakani wabunge wa chama chake baada ya kuboronga kwa maslahi ya chama bali kwa ajili ya taifa. Na kiongozi akipatikana na kosa lolote mfano la wizii achukuliwe hatua kali ikiwa pamoja na kufungwa kama anastahili.. Sio kusema fedha zirejeshwe na kujiuzulu hapana.. Kwani uraiani ukiiba kuku raia awakwambiii urudishe utafungwa au kuuliwa. Watu woteeee tuwe chini ya sheria na kuwajibika kutokana na matendo yetu.
9. awe na upeo mpana wa kukabiliana na changamoto za kiutalawa, asikie kilio cha wananchi, aweze kushughulikia mambo. Sio kiongozi unaulizwa kwanini nchi yako haina umeme unasema sijui au mimi sio Mungu. Wakati kuna vyanzo vingi vya umeme mfanoo makaa ya mawe, uranium, sio kutegemea umeme wa majii tuu.
10. Tanzania ni nchi yenye mali nyingi sanaa ikiwamo madini, milima,maji,bahari, mbuga za wanyama na vituo vingi vya kitalii n.k japo ni nchi masikini sana. Tunamtaka kiongozi ataeweka sera nzuri zinazotekelezeka ikiwa ni pamoja na kutunga sheria ya kuzilinda na kuziifadhi kwa ajili ya vizazi vijavyo. Tuipende nchi yetu ikiwa ni pamoja na kuwafikiria wataokuja baada ya kizazi hiki wasikute mashimoo tuu, tembo hakuna, vifaru hakuna wataishi maisha magumu sana kwa ajili ya mababu zao sio jambo jema. Kiongozi bora ni yule anaetaka taifa liwe imara hata baada ya yeye kutoka madarakani.
11. Asimamie katiba iwe katiba itayotoa haki sawa kwa wote bila ubaguzi. Iwe katibaa itayotoa fursa kwa vyama vyote. Hii itasidia sana kwani wananchi wataweza kuwawajibisha vyama na viongozi wao kila uchaguzi unapokuja ila katiba ikiwa inabeba chama kimoja kinashinda hata wakikosea hatutokaa tukaendelea na haina picha nzurii. Ila ukiwa mzalendo wa kweli utaweka mwanya kwa wengine wenye uwezo wa kuendesha nchi.
12. Awe mzalendo na sio mchama kwani chama sio baba wala mama yake pale chama kinapokosea aweze kusema hapana kwa maslahi ya raia wa Tanzania.
13. Kuweza kuweka mfumo utaotoa fursa sawa kwa wote iwe masikini,tajiri, mlemavu, mwanamke, kijana, mwanaume. Tanzania ukimtoa mwalimu jk sioni kiongozi mwingine alietoa fursa sawa kwa wote kama yeye. Mtaani kuna viongozi wengi wazuri hawajapata fursa, kuna wanasayansi wazuri hawajapata fursa, kuna wachezaji wazuri hawajapata fursa kuna vipaji vingi sana vinavyoweza kusaidia nchi ila mfumo uliowekwa wa kujuana unalibomoa taifa kwa kupata wawakilishi wabovu, waatendaji wa bovu sanaa, viongozi wabovu sanaaa. Kuna sekta hawatumiii weledi kabisaaa wengi huko wamewekwa kiundugundugu hata wakiboronga inasafishwa. kwa mtindo huo atutafika kokote kulee. Tutumie talent au vipaji vinavyostahiliii hii itasaidia sanaa ila kwanza tutoe mfumo wa kujuana kwani utaleta madhara sanaa kwa taifa na jamii kiujumla mwisho wa siku. Mwalimu jk angeweza kuweka watoto wake, ndugu zake ila alipenda Tanzania kama nyumba au familia yake.
14, Awe mcha Mungu wa kweli.
15. Tanzania inawahitimu wachache sana wa vyuo vikuu walio na shahada na kuendelea. Tunamtaka kiongozi ataeweza kuwaondolea changamoto ya ajira kwani ni asilimia ndogo sanaa yani 10% haifiki ilaa wakoo mtaani. Kwanini wasifufue viwanda wakati kuna mainjinia waandisi hawana ajira, fani nyingi sanaaa ziko mtaani. Kuna sekta kama ya mambo ya ndani pia inahitaji sana wasomi kule. kwani kuna mambo mengine hayaitaji Nguvu ni akilii na mengine nguvu ila siku zote unaanza kwa kutumia akilii ndio ikishindikana nguvuu.
16. Aweze kuwawajibisha watendaji wake na kuwasimamia ipasavyoo ikiwa ni pamoja na kuweka sekta chache zile za muhimu kwa taifa.
MWISHO. Tanzania ni yetu sotee na kila mmoja anayohaki ya kufaidi matunda ya nchi ikiwa ni pamoja na kuishii kwa Amani na Upendo. Mungu ibariki Tanzania.