Mada yako umeiweka vizuri sana na nimeipenda na ukweli sifa ya kwanza Rais wa awamu ya tano anatakiwa atoke upinzani na kura za serikali za mitaa zimeonesha wazi wimbi la mabadiliko , sasa tutashangaa kuona kama wapiga kura watahamia upande wa magamba club! Rais mpya mkali na mwenye ubavu wa kuwatupa jela majoka yote yenye makengeza kina Chenge , Betina nk, Rais atakaeziba mianya yote ya ufisadi serikali kuu na serikali za mitaa , rais mcha Mungu anaechukia ufisadi, Rais ataezuia ujangili na kuuzwa wanyama hai ili watalii waje nchini, rais ataezuia safari za mawaziri na bongo movie kula bata nje ya nchi, rais atakeleta elimu na afya bure kama enzi za Nyerere manake mabilioni yetu yapo uswisi na escrow , Rais atakaefufua reli zote na viwanda, Rais atakewezesha kupatika maji safi na salama na umeme wa bei nafuu, Rais atakaesaidia kushuka bei ya petrol, Rais atakajali walimu na madaktari na wafanyakazi wengineo, Rais atakaejenga uwanja mpya wa kiwango wa ndege kama Kenya, Rais atakaejenga barabara za juu kama Kenya na Uganda wasiojua zipo bongo no nginjera tu miaka hamsini sana ya umaskini hakuna kitu! viongozi kazi kuiba mali ya umma tu na kusomesha watoto wao nje ya nchi ndo wanachojua!
Kuna mda nimesoma thread flani ya gamba ilikuwa na list ya majina ya wagombea toka magamba club ila bahati mbaya sana yalikuwa majina yenye ukakasi aliyoweka na a nikashangaa eti sikuona jina hata moja la mgombea mwenye sifa ya kuwa Rais wa nchi tajiri inayofilisiwa na magamba, nchi ya kusadikika ya Danganyika! Rais gani anaweza kutoka magamba club? Rais atakeendeleza uongozi wa nchi ambayo raia wake walio wengi wamenyimwa elimu sahihi ya uraia kwa maana hawajui kuwa kulala na njaa au kuugua na kukosa matibabu ni kosa la serikali , hawajui kuwa kura ni mkataba na serikali wa kupata hali bora ya maisha kwa watu na kama serikali haiwezi kuleta hali bora inatakiwa iwapishe wengine au mwananchi kuchagua serikali toka chama kingine , hivi ndivyo ulaya na marekani wameendelea , serikali ikishindwa kuwapa wananchi hali bora inapigwa chini kwenye uchaguzi mkuu! hii inaitwa SOCIAL CONTRACT THEORY, pale Mlimani wanafundisha vizuri sana. Hata raia unapokosa kazi si kwa uzembe unatakiwa kulipwa unemployment benefit na Tanzania imesaini mkataba huo wa kuondoa njaa na magonjwa na tatizo la ajira kwa raia wake na kukubali jukumu la kuwasaidia raia wake wote wenye shida na njaa na magonjwa, mwaka 2002 huko Geneva, hiyo inaitwa SOCIAL PROTECTION FLOORS na wananchi hawana habari hiyo, hawajaambiwa na serikali yao hadi leo kuhusu huo mkataba uliosainiwa na serikali yao kuwapa hali bora na kuwanasua na umaskini wa kutupa!
System ya uendeshaji wa nchi ya Tanzania sasa imeoza, nchi inanuka kwa ufisadi , kuonea raia, rushwa na umaskini uliokithiri, umaskini unaowatesa watu wake millioni 47 wanaokufa kwa njaa na magonjwa , raia wasio na elimu wala ajira huku majoka machache yenye makengengeza kina Chenge , Anna Tibaijuka , Werema ( na wengineo wote wanajijua na Mungu anawangoja wafe awachome moto mkali) , wakijilimbikizia mabilioni ya mali ya umma kwenye akaunti zao na kuleta shida kubwa sana kwa raia wa kawaida ya kupata pesa manake haya majoka yenye makengeza na sumu kali yamezitoa pesa kwenye mzunguko wake!pesa ambazo zingepita mahospitalini, kwa mama ntilie, deiwaka, mashuleni, madukani, serikali za mitaa, wizarani nk na kila raia angeambulia japo kidogo ila watemi kina Chenge wamezikwapua zote bila huruma!jamani mtu ana familia ya watoto watatu wazee kama yeye na mke anakwapua millioni elfu nne na mia sita (1.6B) zote anapeleka wapi kama si ulafi na ushetani tu? wanakwapua mabilioni wasiyoyahitaji katika maisha yao ya kila siku, na cha ajabu sana mabilioni wasiyoyatumia!
Ikumbukwe kuwa umaskini wa Tanzania ni wa kujitakia na unasababishwa na mashetani wachache wenye maumbo ya binadamu, mashetani wenye nyadhifa mbali mbali serikali kuu na serikali za mitaa!. ni ajabu sana wadanganyika wana macho na hawaoni jinsi nchi yao inavyoliwa na mafisadi , waziri anakuja kwenye mkutano wa kampeni na TOYOTA LANDCRUISER GX six cylinder iliyotokana na kodi ambazo ni majasho ya walalahoi manake matajiri wanasamehewa kodi bongo, gari inakunywa mafuta kwa siku moja ni bajeti ya mlalahoi kwa mwaka na wanawatimulia vumbi raia waliokaa juani eti kuwasikiliza huku wakisikia njaa kwa kukosa chakula na waliovaa nguo zina viraka na eti wengine wana sugu kwa kuhangaika na jembe la mkono miaka nenda miaka rudi hadi alama za dole gumba zimefutika ila bado masikini hawa wanachagua hawa matajiri kuwaongoza, hivi watu wasiojua njaa inavyouma watakusaidiaje? hivi raia hamjui kuwa foleni ya Dar ni ya kutengeneza ili raia wasi discuss mambo ya maendeleo manake muda wote watu wa Dar wana discuss foleni na kuwaza foleni, eti mtu anaamka saa kumi kukwepa foleni isimkute eti atachelewa kibaruani na huu miungu watu viongozi wetu wakiwa na safari , piki piki ya usalama inapita kuyaamuru magari yakae pembeni wenye nchi wapite , unadhani hao wanaopita na misafara yao wasiojua adha ya foleni wataondoaje foleni?! jamani amkeni miaka hamsini ya umaskini haitoshi tu!
Wakati huo huo Tanzania ni nchi iliyojaa udikteta uliojificha katika kichaka cha demokrasia iliyoishia kwenye makaratasi manake walalahoi wanaojaribu ku exercise demokrasia wanatekwa na kuteswa, na huku vyombo vyenye jukumu la kulinda usalama navyo vinawapiga watu ovyo, vinaua na kuleta vilema kwa raia wasio na hatia , watu wanaoandamana kudai haki zao za kikatiba! bongo ni nchi ya ajabu sana! viongozi na matajiri wako juu ya sheria , akili zangu zinaniambia wafungwa wengi Tanzania wanafungwa kwa kuonewa tu , kwa kuwa kina Chenge wameiba pesa zote za umma na wananchi wanakosa elimu na huduma za afya na matokeo yake hawana ajira wanaishia kukaba na kuiba na kukamatwa na kufungwa manake wanasikia njaa na hawana namna ya kupata chakula na nguo kihalali kama Panya Road, ikumbukwe sitetei uhalifu kamwe! Magereza zimejaa masikini tu! nawapa pole sana, hata sisi tunaopiga cargo na deiwaka ughaibuni nawaambia ukweli wangu ni effects za kina Chenge pia , manake tumesota sana bongo miaka nenda rudi, tukaanza kuzeekea kwenye umaskini, tumelala na njaa na kukosa matibabu na nguo, tulipopata upenyo bila kuwaza mara mbili mbili tukakimbilia nje!!na wengi wetu hatupendi kabisa kurudi bongo kuona tena nyuso mbaya kabisa za kina Chenge!
Jamani Chenge ni mfano mbaya sana kuwahi kutokea katika historia ya jamii ya Tanzania, ni mfano mbaya sana kwa watoto wa Tanzania. Huyu nyoka mwenye makengeza na sumu kalai anafaa kufundishwa shuleni kama mfano wa raia wahujumu uchumi na vyanzo vya umaskini na uhalifu Tanzania. Chenge ni nyoka mwenye makengeza na sumu kali inayoua raia wa Tanzania , nyoka mbabe alie mstari wa mbele kupeperusha bendera ya ufisadi huku wenzake wakimfuata kwa shangwe nyuma yake. Ndio, yeye na wenzake wote katika chama wanapigana vikumbo kufilisi mali ya wavuja jasho, walalahoi wanaokamuliwa kodi huku matajiri wakipewa misamaha ya kodi.
Chenge na genge lake la majoka yenye makengeza na sumu kali yalio madarakani na yale yaliostaafu tangu uhuru yanaishi kifahari masaki kwa kutumia mali ya umma ambayo ni majasho ya walalahoi wa Tanzania, nani anabisha? Chenge ameonesha wazi stage tuliyofika katika nchi ambapo sasa watawala wetu wako juu ya sheria! mtu ni mwizi wa dhahiri na anagoma kuhojiwa na hafanywi kitu , japo tukumbuke most of viongozi wa Tanzania ni mafisadi na kama huamini taja jina moja lolote na waambie TAKUKURU NA CAG wamkague na utayopata iwe siri yako! Maskini nchi tajiri ya Tanzania iliyojaa rasilimali lukuki imepata bahati mbaya sana kuwa na viongozi mashetani, wezi, walafi, wabinafsi , wasiomjua mungu na madhalimu wakubwa wasiojali mateso wanayopata raia wake. Wananchi shime shime tupigie kura upinzani kwenye uchaguzi mkuu kuyaondoa madarakani majoka haya yenye makengeza na sumu kali inayotuua! gamba mmoja tu akisoma hii comment , i will be extremely happy! . Tanzania bila magamba inawezekana , tumeanza kuona uchaguzi serikali za mitaa!Mungu ibariki Tanzania, Mungu ninakuomba tuondolee mafisadi katika uongozi wa nchi ya Tanzania, Amen