Salamu,
Mimi kabwela mlalahoi, nachukua nafasi kuwawakilisha makabwela wote popote walipo kuwa sasa tumechoka na siasa za kujenga matumbo ya wachache tunaviomba vyama vituteuliye mtu ambaye anahudhunika kutuona makabwela tukizunguka pembezoni na katikati ya majalala mwanasiasa anayekelwa kuona mayatima wakilala ndani ya mapumba ya mchele, msituchaguliye mtu kutokana na urafiki wenu, undugu wenu au utajiri wake bali anayekidhi vigezo vyakutupigania.
Msihofu kumchagua mtu eti kwasababu ya chuki na migogoro yenu kama anauwezo tuleteeni huyo huyo atufanyie kazi,nendeni kila kona mkihubiri habari ya rushwa na ufisadi kahubirini habari ya uhadilifu hubirini habari njema juu ya haki maana makabwela wengi hatunahaki juu ya taifa hili nendeni mkahubiri habari ya uzalendo na mioyo ya kulipenda taifa lao.
Nendeni kila kona ya dunia mkitafuta wataalamu waje kutuelimisha ilinasi tukue kitechnologia ondoeni syllabus za kutupumbaza na kutufanya tusiwe chochote ktk elimu, semeni kila mahali kuwa Tanzania bila viwanda haiwezekani, semeni Wazawa bila madini na maliasili haiwezekani fanyeni hivyo.
By sauti ya mtu aliayenyikani.