Rais ajaye awe na sifa zifuatazo

Rais ajaye awe na sifa zifuatazo

"Ndugu zangu nafarijika sana kwa kauli zenu lakini hili suala la urais ni kubwa, tumuache huyu aliye juu (Mungu), yeye akiamua liwe linakuwa," By Lowassa........ Mtanzania tarehe 9.2.2015

Kiburi cha fedha bwana, acha tu, kuwa mtu anamua kukejeli hata muumba wake. Huku anahangaika kununua na kuhonga watu, huku anadanganya Mungu ndie atakaye amua. Mshindwe na mlegee muache kumkejeli Mungu.
 
Wapendwa wana Jf na watanzania wenzangu, nimekaa na kutafakari nimefika mahali naona,huenda ya faa sasa tuongozwe na mtanzania mwenye hofu ya Mungu? Hapa namaanisha mcha Mungu, pasipo kujari anatoka dini gani.

Pasipo shaka ni imani yangu mtu mwenye hofu ya Mungu hakika ana hekima na busara, vinavyo ongozwa na upendo. Mtu huyu hakika hatasema mimi, bali atasema sisi. Pasipo shaka, ni imani yangu mtu wa aina hii atakuwa mzalendo, atawaza juu ya maslahi mapana ya watanzania.

Je! Ni sahihi tunahitaji mtu wa aina hii sasa?

Angalizo, tafadhali tusiingize udini katika kujadili hili.
 
Hofu ya Mungu haitoshi, (anaweza kukengeuka na kuwaambia raia wake wapigwe tu) hekima na busara alizojaliwa na Mungu ndicho kiini cha taifa kustawi na kuimarika
 
husika na kichwa cha habari hapo juu..
viongozi tuochagua tunawapa kura kwa kuwa wanatupa khanga na kofia na vijihela lakini hawaleti maendeleo

tutampateje rais asiyetokana na mafisadi?
 
Ukawa wamejifungia ktk maombi wakitutafutia rais atakayetufaa.
 
Ni vigumu kumpata rais mwenye tabia zinazomridhisha kila mtu. Lakini za mhimu awe na upendo kwa taifa lake asiwe mhusika na mambo ya ufisadi ktk maisha yake awe na mifano inayoonekana kuwa kuongozi asiwe mpenda kupigiwa makofi ya viongozi wenzake
 
Wana JF.Rais mla rushwa alieingia madarakani kwa rushwa,ina inabidi agawe madaraka na kuwapendelea waliomsaidia kwa rushwa kwa maana msingi wa ushindi wake ni rushwa.Rushwa ni usanii kama walivyo wasanii wa mtaa wa Samora.Nchi kachukua msanii alijiingiza kisanii na kura zilikuwa za kisanii kuhalalisha usanii.Nguvu ya nchi ni vijana,wewe kijana ulielala na kutoijua hata haki yako katika nchi yako AMKA SASA,wewe kijana unaeuza haki yako kwa kipande cha mshkaki na gongo wakati mwenzako anaondoka na almasi yako kwanini usiamke na kutaka mgawane hiki kipande cha almasi? Ikulu ni usanii mtupu,wizara zote ni usanii mtupu.mahosipitali ni usanii mtupu na mahakamani ni usanii mtupu na vituo vya polisi ni usanii mtupu.Unategemea kupata haki kwa mtu aliepata madaraka kwa rushwa? Wananchi wamepumbazwa hushabikia ujinga kuliko vitu vya msingi.Miaka 50 ya uhuru eti hata maji safi hamna? Tuamke jamani.
 
Wana JF.Rais mla rushwa alieingia madarakani kwa rushwa,ina inabidi agawe madaraka na kuwapendelea waliomsaidia kwa rushwa kwa maana msingi wa ushindi wake ni rushwa.Rushwa ni usanii kama walivyo wasanii wa mtaa wa Samora.Nchi kachukua msanii alijiingiza kisanii na kura zilikuwa za kisanii kuhalalisha usanii.Nguvu ya nchi ni vijana,wewe kijana ulielala na kutoijua hata haki yako katika nchi yako AMKA SASA,wewe kijana unaeuza haki yako kwa kipande cha mshkaki na gongo wakati mwenzako anaondoka na almasi yako kwanini usiamke na kutaka mgawane hiki kipande cha almasi? Ikulu ni usanii mtupu,wizara zote ni usanii mtupu.mahosipitali ni usanii mtupu na mahakamani ni usanii mtupu na vituo vya polisi ni usanii mtupu.Unategemea kupata haki kwa mtu aliepata madaraka kwa rushwa? Wananchi wamepumbazwa hushabikia ujinga kuliko vitu vya msingi.Miaka 50 ya uhuru eti hata maji safi hamna? Tuamke jamani.


Mkuu, hoja za msingi hizo. Wanazo wengi tatizo ni uoga wa Kulimbokwa!
 
Nchi ya Tanzania inahitaji Rais mwenye sifa hizi:
1. Muadilifu
2. Asiyefumbia macho uzembe na uvivu
3. Anayejali wanyonge hasa wa vijijini
4. Mkali asiyevumilia uvunjaji wa sheria
5. Mwenye maono ya Tanzania ya miaka 20- 50 ijayo
- Maono kuhusu ajira
- Maono kuhusu Nishati
- Maono hukusu nishati
- Maono kuhusu ulinzi wa rasilimali
6. Anayechukia rushwa,wizi na ubinafsi
Rais huyo ni Prof. Sospeter Muhongo

CHECK KIAMBATANISHO NAMNA WATANZANIA WANAVYOMKUBALI MTAALAMU HUYU . WAMEANZA WAZEE WA SERENGETI, VIJANA TUNAFUATA.
 

Attachments

  • WAZEE WA MILA.jpg
    WAZEE WA MILA.jpg
    140.4 KB · Views: 601
Ni kweli ni mzalendo mgawaji mzuri wa vitalu vya gesi! Hawa wazee wana maono kama ya wizi wa ng'ombe huko kwao maana wanasema ni kuchukuwa tu na siyo kuwa wameibiwa!
 
Back
Top Bottom