Rais ajaye awe na sifa zifuatazo

Rais ajaye awe na sifa zifuatazo

hatujafikia muda wa kuangalia mtu, lengo ni kuifurumusha hili nguruwe pori(ccm) kwanza kwenye utawala wa kihuni
 
hakuna chama bila wanachama na hakuna wanschama bila watu.Anza kuchunguza watu ambao ndio watengenezaji na watekelazaji wa chochote kilichopo kwenye chama
 
Watanzania hatutaki raisi asiye na busara,mwenye majungu,mbinafsi,mwenye chuki binafsi,mwenye visasi na PIA HATUTAKI RAIS AMBAEYE HAJAJIANDAA KISAIKOLOJIA KUWA KIONGOZI WA NGAZI YA JUU KATIKA TAIFA LETU.

Watanzania hatutaki viongozi waimba taarabu majukwaani badala ya kutuambia watatufanyia nini..Watanzania hatutaki viongozi wanaotukana wapiga kura majukwaani..Watanzania hatutaki viongozi wenye ubinafisi,chuki na wenye visasi.

Kikwete ni mbinafsi,ni mtu mwenye chuki na pia ni mtu mwenye visasi...Magufuli ni mbinafsi,ni mtu mwenye chuki na mwenye visasi..hata viongozi wanaofanya nao kazi wamethibitisha hili.

Tuwakatae! Watanzania wenzangu tuwakatae hawa watu wameligawa taifa letu kwa udini na ukabila,na bado wanaendelea kuimarisha huu udini na ukabila..hawafai!

Nina Imani na Lowasa.
Nina Imani na Ukawa.
 
Magufuli anatosha kuliongoza Taifa hili la Tanzania kwakuwa ni Mchapakazi,Muadilifu na Mfuatiliaji #hapakazitu
Magufuli chaguo la wengi
 
Wakuu heshima kwenu
_biashara haijawa kipaumbele cha hili taifa ila serekali inataka kutuzo tu kodi
_imefikia hatua kufanya biashara hasa ya duka hapa Tanzania ni kama anasa hivi maana ukishafungua tu duka serekali yote inaamia kwako
_Lesini ni pesa
_tra ni pesa
_fire ni pesa
_watakuambia ulipie taka
_pango ni pesa
Kwanini sijasikia hata mgombea mmoja akitetea kuinua wafanyabiashara Tanzania?
Wafanyabiashara wanafanya biashara kwa hofu kubwa

Nasema rais atakayeweka kipaumbele cha kuinua wafanyabiashara nitapa kura yangu
 
Wananchi kuelekea October 25 hiki ni kipindi cha kuweka sifa za rais umtake kutumikia kipindi cha miaka 5 watakiwa kuwa makini na kipindi hiki kuelekea October..wantazania wekeni sifa za RAIS mmtakaye afu mwapime wagombea wote kwa vigeZo mvitakavyo.
 
Kiongozi wa Umma lazma yeye na familia yake watumie huduma za Umma za Elimu, Afya na Usafiri.
Kwa sera hii wanafunzi hawatakosa chakula, kukaa chini, kulundikana darasani, kusukumwa kwenye daladala hospital hazitakosa dawa, vitanda, vipimo muhimu n.k.
 
Na utamaduni wetu huu itakuaje ili tusonge mbele?
Na kwanini unataka raisi wako awe lowasa na si magufuli?
 
Heshima yetu kama nchi kwa kiasi kikubwa itatokana na heshima ya Rais wetu. Ndiyo kusema Rais akijiheshimu na akaheshimiwa na sisi pia tunapata heshima. Vivyo hivyo ikitokea Rais akawa haheshimiwi nje ya mipaka yetu sisi pia tunakosa heshima kama nchi.

Akiwa makini tutaonekana makini kama nchi. Akiwa mropokaji tutaonekana waropokaji kama nchi. Akiwa mlevi tutaonekana walevi kama nchi. Akiwa mwizi tutaonekana ni majambazi kama nchi. Akiwa malaya na mzinzi tutaonekana wazinzi na malaya kama nchi.

Kwahiyo urais ni taswira ya Taifa na unabeba dhamana nzito. Ni lazima basi tumtathimini mtu yeyote anayetaka kuwa Rais wetu kwa jicho kali na macho mapana katika kila hali aliyo nayo: maneno yake, matendo yake, haiba yake, akili yake, afya yake, n.k. Ili aweze kukidhi haja ya kiti cha urais sawasawa na sawia, Rais tunayemchagua lazima asiwe mtu wa kawaida. Ni lazima awe ni mtu bora kuliko sisi wote.

Tutafanya makosa makubwa kuchagua mtu wa kawaida, anayefanana na sisi, mwenye tabia kama zetu na mwenye maono kama sisi.

Kwa kuwa Rais si mtu wa kawaida na hapaswi kuwa mtu wa kawaida, ni watu wachache sana wanaoweza kuchukua dhamana ya urais katika nchi yeyote ile duniani. Kwa sababu hii ni muhimu tuwe makini sana tunapochagua mgombea urais kwa vyama vyote ili tushindanishe watu ambao ni bora kabisa katika nchi yetu.

Tukikosea tukachagua mtu wa kawaida huyu ataendesha mambo kikawaida sana. Kwa hiyo kama wananchi walio wengi wamezoea ubabaishaji, uhuni, rushwa, wizi, n.k., tutapata Rais ambaye ni mbabaishaji, mhuni, na mpenda rushwa kama sisi na hatutasogea.

Ninajadili vigezo vya mtu anayefaa kuwa Rais wetu wa tano. Vigezo hivi nimevigawa katika makundi makubwa mawili. Kundi la kwanza linabeba sifa za kihaiba na kundi la pili ni la sifa za kikazi. Leo ninabainisha sifa za kihaiba. Kwa maoni yangu, mgombea urais anapaswa kuwa na vigezo angalau sita vinavyoangukia katika kundi la sifa za kihaiba.

Kigezo cha kwanza ni uaminifu. Ili Rais aweze kukamilisha ajenda yake, ni lazima aaminike kwa watu anaowaongoza. Bila watu kumuamini hakuna atakachofanya na watu wakakikubali. Kama watu hamwamini Rais itasababisha wabunge na vyombo vingine vya dola kuanza kumtilia shaka katika utendaji wake na hii itasababisha programu zake nyingi zikwame kwa sababu ufanisi wake unategemea kuungwa mkono na vyombo vingine vya dola likiwamo Bunge.

Tukumbuke pia kwamba Rais wa nchi ndiye msuluhi
 
1.Mwenye Afya njema
2.Anayepinga Ufisadi na Rushwa
3.Mwenye nia thabiti ya ukombozi wa Taifa hili
4.Anayehubiri Amani
5.Mzalendo wa kweli
6.Asiyetiliwa mashaka katika uadilifu na utendaji wake
7.Anayzijua kwa dhati changamoto za watanzani
8.Asiyebadilika badilika katika maamuzi yake
9.Anayethamini watanzania kwa hali zao
10.Atakayesimamia umoja wetu
 
john pombe Magufuli kiboko ya Mafisadi anatosha sanaaaaaaa,fisadi lowassa hana nafasi ya kutawala hapa
 
Back
Top Bottom