Rufiji dam
JF-Expert Member
- Feb 20, 2020
- 3,804
- 8,797
Waungwana nawasalimia.
Leo kuna rafiki yangu yeye ni Mfanyakazi wa Serikalini maskani yake ya kazi ni Dodoma.
Leo kanifuta kuomba nimpe loan ya laki 5 ana shida nayo ya haraka sana. Sikutaka kumpa mpaka nijue ni haraka gani imempata ndio akaja na habari ya kushangaza kabisa kuwa namkopea rafiki yake wa kike ambaye ni mke wa mtu. Nilimuangalia jamaa yangu wala sikuelewa kakamatwa na nini.
Nikamuuliza huyo dada ambaye ni mke wa mtu wanajuana akasema hapana. Ila wanachati kupitia META ila hawajawahi kuonana! Sijui huyu jamaa karogwa na nini maana namjua kichwani yupo mzima hasa.
Nikasema acha nimtengenezee mazingira magumu. Nikamwambia pesa ipo ila ina riba ya 20% ndani ya wiki mbili pia aniachie kadi ya gari lake. Nimempa sharti gumu na nimpe ushauri wa kina sana. Afanye uchunguzi wa kina. Nimemtahadharisha matokeo hasi ya kumkopesha pesa mke wa mtu.
Nimemwambia pia kama ni kweli wana urafiki tu na sio mahusiano ya kimapenzi amshirikishe mumewe. Sijui kuna watu wana wazimu, unakutana na mtu META ama hapa JF mnaanza kukopeshana? Mungu ampe ufunuo ndugu yangu aachane na hio habari maana kaaondoka kanuna sana.
Leo kuna rafiki yangu yeye ni Mfanyakazi wa Serikalini maskani yake ya kazi ni Dodoma.
Leo kanifuta kuomba nimpe loan ya laki 5 ana shida nayo ya haraka sana. Sikutaka kumpa mpaka nijue ni haraka gani imempata ndio akaja na habari ya kushangaza kabisa kuwa namkopea rafiki yake wa kike ambaye ni mke wa mtu. Nilimuangalia jamaa yangu wala sikuelewa kakamatwa na nini.
Nikamuuliza huyo dada ambaye ni mke wa mtu wanajuana akasema hapana. Ila wanachati kupitia META ila hawajawahi kuonana! Sijui huyu jamaa karogwa na nini maana namjua kichwani yupo mzima hasa.
Nikasema acha nimtengenezee mazingira magumu. Nikamwambia pesa ipo ila ina riba ya 20% ndani ya wiki mbili pia aniachie kadi ya gari lake. Nimempa sharti gumu na nimpe ushauri wa kina sana. Afanye uchunguzi wa kina. Nimemtahadharisha matokeo hasi ya kumkopesha pesa mke wa mtu.
Nimemwambia pia kama ni kweli wana urafiki tu na sio mahusiano ya kimapenzi amshirikishe mumewe. Sijui kuna watu wana wazimu, unakutana na mtu META ama hapa JF mnaanza kukopeshana? Mungu ampe ufunuo ndugu yangu aachane na hio habari maana kaaondoka kanuna sana.